< 2 Thessalonians 2 >
1 Now we beseech you, brethren, concerning the coming of our Lord Jesus Christ, and our being assembled together unto him,
Sasa yahusu kuja kwake Bwana wetu Yesu Kristo na kukusanywa kwetu pamoja tukae naye. Ndugu, tunawaombeni sana
2 that ye be not easily shaken in mind, nor troubled, either by spirit, or by word, or by letter as from us, as if the day of the Lord were close at hand.
msifadhaike upesi moyoni, na wala msitiwe wasiwasi kwa sababu ya madai kwamba Siku ya Bwana imekwisha fika. Labda inadhaniwa kwamba jambo hili limetokana na uaguzi fulani, mahubiri au barua inayosemekana kuwa imetoka kwetu.
3 Let no one deceive you in any manner; for [[that day will not come]] unless the apostasy shall have come first and the man of sin have been revealed, the son of perdition;
Msikubali kudanganywa na mtu yeyote kwa namna yoyote ile. Maana Siku hiyo haitakuja mpaka kwanza ule Uasi Mkuu utokee na yule Mwovu aonekane ambaye mwisho wake ni kuangamizwa kabisa.
4 he that opposeth and exalteth himself above every one that is called God, or worthy of worship, so that he sitteth in the temple of God, showing himself to be God.
Yeye atapinga kila kitu wanachokiona watu kuwa ni mungu, au wanachokiabudu. Naam, hata ataingia na kuketi ndani ya Hekalu la Mungu akijidai kuwa Mungu.
5 Do ye not remember, that, when I was yet with you, I told you these things?
Je, hamkumbuki kwamba niliwaambieni haya yote wakati nilipokuwa pamoja nanyi?
6 And now ye know what restraineth, in order that he may be revealed in his own time.
Lakini kuna kitu kinachomzuia sasa, nanyi mwakijua kitu hicho. Basi, huyo Mwovu ataonekana wakati wake ufaao.
7 For the mystery of lawlessness is already working; only there is one who now restraineth, until he be taken out of the way;
Hata hivyo, Mwovu huyo aliyefichika anafanya kazi sasa, lakini hataonekana mpaka yule anayemzuia aondolewe.
8 and then will the lawless one be revealed, whom the Lord Jesus will consume with the breath of his mouth, and destroy with the manifestation of his coming;
Hapo ndipo Mwovu atakapotokea; lakini Bwana Yesu anapokuja atamuua kwa pumzi ya kinywa chake na kumwangamiza kwa mng'ao wa kuja kwake.
9 [[he, ]] whose coming is after the working of Satan with all power, and signs, and wonders of falsehood,
Huyo Mwovu atakuja na nguvu za Shetani na kufanya kila namna ya miujiza na maajabu ya uongo,
10 and in all deceit of unrighteousness for those who are perishing; because they received not the love of the truth, that they might be saved.
na kutumia udanganyifu wa kila namna kwa wale walio katika mkumbo wa kupotea. Hao watapotea kwa sababu hawakuupokea na kuupenda ule ukweli ili waokolewe.
11 And for this cause God sendeth them a working of delusion, that they may believe the falsehood;
Ndiyo maana Mungu amewaweka chini ya nguvu ya upotovu, wauamini uongo.
12 that they may all be judged, who believed not the truth, but had pleasure in unrighteousness.
Matokeo yake ni kwamba wote wasioamini ukweli, ila wafurahia dhambi, watahukumiwa.
13 But we are bound to give thanks always to God for you, brethren beloved of the Lord, that God chose you from the beginning to salvation in sanctification of the Spirit, and belief of the truth;
Tunapaswa kumshukuru Mungu daima kwa ajili yenu ninyi ndugu, ninyi mnaopendwa na Bwana, kwa maana Mungu amewateua tangu mwanzo mpate kuokolewa kwa nguvu ya Roho mfanywe watu wake watakatifu kwa imani yenu katika ukweli.
14 whereunto he called you by our gospel, to the obtaining of the glory of our Lord Jesus Christ.
Mungu aliwaitieni jambo hili kwa njia ya Habari Njema tuliyowahubirieni; aliwaiteni mpate kupokea sehemu yenu katika utukufu wa Bwana wetu Yesu Kristo.
15 So then, brethren, stand firm, and hold fast the traditions which ye were taught by us, whether by word, or by our letter.
Basi, ndugu, simameni imara na zingatieni yale mafundisho tuliyowafundisheni kwa mahubiri yetu na barua zetu.
16 Now our Lord Jesus Christ himself, and God, our Father, who loved us, and gave us everlasting consolation and good hope through grace, (aiōnios )
Tunamwomba Bwana wetu Yesu Kristo mwenyewe na Mungu Baba yetu ambaye alitupenda, na kwa neema yake akatujalia faraja ya milele na tumaini jema, (aiōnios )
17 encourage your hearts, and establish you in every good work and word.
aifariji mioyo yenu na kuwaimarisheni ili mweze daima kutenda na kusema yaliyo mema.