< 2 Peter 2 >
1 But there arose false prophets also among the people, as there will be false teachers among you also, who will stealthily bring in destructive factions, even denying the Lord that bought them; bringing upon themselves swift destruction.
Palitokea manabii wa uongo kati ya watu, na vivyo hivyo walimu wa uongo watatokea kati yenu. Watu hao wataingiza mafundisho maharibifu na kumkana Bwana aliyewakomboa, na kwa njia hiyo watasababisha ghafla maangamizi yao wenyewe.
2 And many will follow their dissolute ways, by reason of whom the way of truth will be evil spoken of;
Tena watu wengi watazifuata hizo njia zao mbaya, kwa sababu yao, wengine wataipuuza Njia ya ukweli.
3 and in covetousness will they with feigned words make merchandise of you; for whom the judgment long ago ordained lingereth not, and their destruction slumbereth not.
Kwa tamaa yao mbaya watajipatia faida kwa kuwaambieni hadithi za uongo. Lakini kwa muda mrefu sasa Hakimu wao yu tayari, na Mwangamizi wao yu macho!
4 For if God spared not angels that sinned, but cast them down to hell, and delivered them over to chains of darkness, to be reserved unto judgment; (Tartaroō )
Malaika walipotenda dhambi, Mungu hakuwahurumia, bali aliwatupa katika moto wa Jehanamu ambako wamefungwa wakingojea Siku ile ya Hukumu. (Tartaroō )
5 and spared not the old world, but saved Noah with seven others, a preacher of righteousness, when he brought in the flood upon the world of the ungodly;
Mungu hakuihurumia dunia ya hapo kale, bali alileta gharika kuu juu ya nchi ile ya watu wasiomcha Mungu; lakini Noa ambaye alihubiri uadilifu, Mungu alimwokoa pamoja na watu wengine saba.
6 and turning into ashes the cities of Sodom and Gomorrah, condemned them to overthrow, making them an example for those who in after time should live ungodly;
Mungu aliadhibu miji ya Sodoma na Gomora, akaiteketeza kwa moto, akaifanya iwe mfano wa mambo yatakayowapata watu wasiomcha Mungu.
7 and delivered righteous Lot, distressed by the lewd conduct of the lawless men;
Alimwokoa Loti, mtu mwema, ambaye alisikitishwa sana na mwenendo mbaya wa watu hao waasi.
8 (for that righteous man dwelling among them, in seeing and hearing tormented his righteous soul from day to day with their lawless deeds; )
Loti aliishi miongoni mwa watu hao, na kwa siku nyingi moyo wake ulikuwa katika wasiwasi mkuu aliposikia matendo yao maovu.
9 the Lord knoweth how to deliver the godly out of temptation, and to reserve the unrighteous under punishment to the day of judgment;
Kwa hiyo, basi, Bwana anajua jinsi ya kuwaokoa katika majaribu watu wanaomcha Mungu, na jinsi ya kuwaweka waovu katika adhabu hadi Siku ile ya hukumu,
10 but chiefly those who walk after the flesh in the lust of uncleanness, and despise dominion. Presumptuous, self-willed, they are not afraid to rail at dignities;
hasa wale wanaofuata tamaa mbaya za mwili na kupuuza mamlaka. Watu hao ni washupavu na wenye majivuno, huvitukana na hawaviheshimu viumbe vitukufu vya juu.
11 whereas angels, who are greater in strength and power, bring not against them a railing accusation;
Lakini malaika, ambao wana uwezo na nguvu zaidi kuliko hao walimu wa uongo, hawawashtaki na kuwatukana hao mbele ya Bwana.
12 but these, as brute beasts, by nature born to be taken and destroyed, railing at things which they understand not, shall even perish in their own corruption,
Watu hao ambao hutukana chochote kile wasichoelewa, ni sawa na wanyama wasio na akili, ambao huzaliwa na baadaye hukamatwa na kuchinjwa! Wataangamizwa kutokana na uharibifu wao wenyewe,
13 receiving the wages of unrighteousness. Counting it pleasure to riot in the day-time, spots and blemishes, reveling in their deceits while they feast with you,
na watalipwa mateso kwa mateso ambayo wameyasababisha. Furaha yao ni kufanya, tena mchana kabisa, chochote kinachotosheleza anasa zao za mwili. Hao ni fedheha na aibu tupu kwa jumuiya yenu wakati wanapojiunga nanyi katika karamu zenu, bali wakifurahia njia zao za udanganyifu.
14 having eyes full of an adulteress, and that cannot cease from sin, alluring unstable souls, having a heart exercised in covetousness, children of a curse,
Macho yao yamejaa uzinzi na uwezo wao wa kutenda dhambi hauna kikomo. Huwaongoza watu walio dhaifu mpaka mitegoni. Mioyo yao imezoea kuwa na tamaa ya mali. Wapo chini ya laana ya Mungu!
15 they have forsaken the right way, and have gone astray, following the way of Balaam the son of Bosor, who loved the wages of unrighteousness,
Wameiacha njia iliyonyoka, wakapotoka na kuifuata njia aliyofuata Balaamu, mwana wa Beori, ambaye alipendelea kupata faida kwa kufanya udanganyifu,
16 but was rebuked for his iniquity; the dumb ass, speaking with man's voice, restrained the madness of the prophet.
akakaripiwa kwa ajili ya uovu wake. Punda ambaye hasemi alinena kwa sauti ya binadamu, akaukomesha wazimu wa huyo nabii.
17 These are wells without water, and mists driven by a tempest; for whom the blackness of darkness is reserved.
Watu hao ni kama chemchemi zilizokauka, kama mawingu yanayopeperushwa na tufani; makao yao waliyowekewa ni mahali pa giza kuu.
18 For speaking great swelling words of vanity, they allure in the lusts of the flesh, by dissolute ways, such as were in some measure escaping from those who live in error;
Husema maneno ya majivuno na yasiyo na maana, na kutumia tamaa zao mbaya za kimwili kuwatega wale ambao wamejitenga hivi karibuni na watu waishio katika udanganyifu.
19 promising them liberty, while they themselves are slaves of corruption; for by what a man is overcome, by the same is he also brought into bondage.
Huwaahidi watu wengine eti watakuwa huru, kumbe wao wenyewe ni watumwa wa upotovu—maana mtu ni mtumwa wa chochote kile kinachomtawala.
20 For if after they have escaped the pollutions of the world through the knowledge of the Lord and Saviour Jesus Christ, they are again entangled therein and overcome, the last state is worse with them than the first.
Watu waliokwisha ponyoka katika upotovu wa ulimwengu kwa kupata kumjua Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo, kisha wakakubali kunaswa na kutawaliwa tena na upotovu huo, hali yao itakuwa mbaya zaidi kuliko awali.
21 For it would have been better for them not to have known the way of righteousness, than, after having known it, to turn from the holy commandment delivered to them.
Ingalikuwa afadhali kwao kama wasingalijua kamwe njia hiyo ya uadilifu kuliko kujua na kisha kuiacha na kupoteza amri takatifu waliyopokea.
22 It hath happened to them according to the true proverb, The dog returned to his own vomit; and, The sow that was washed, to her wallowing in the mire.
Ipo mithali isemayo: “Mbwa huyarudia matapishi yake mwenyewe,” na nyingine isemayo: “Nguruwe aliyekwisha oshwa hugaagaa tena katika matope!” Ndivyo ilivyo kwao sasa.