< 2 Corinthians 5 >

1 For we know that, if our earthly tent-habitation be destroyed, we have a building provided by God, a house not made with hands, everlasting, in the heavens. (aiōnios g166)
Kwa maana twajua kama hema yetu ya dunia tunayoishi ikiharibiwa, tunalo jengo kutoka kwa Mungu, nyumba iliyo ya milele kule mbinguni, isiyojengwa kwa mikono ya wanadamu. (aiōnios g166)
2 For while in this we groan, longing to be clothed upon with our habitation which is from heaven;
Katika hema hii twalia kwa uchungu, tukitamani kuvikwa makao yetu ya mbinguni,
3 since, indeed, when we have put off our present garment, we shall not be found naked.
kwa kuwa tukiisha kuvikwa hatutaonekana tena kuwa uchi.
4 For we who are in this tent groan, being burdened; inasmuch as we do not desire to be unclothed, but to be clothed upon, that mortality may be swallowed up by life.
Kwa kuwa tukiwa bado katika hema hii twalia kwa uchungu na kulemewa, kwa sababu hatutaki kuvuliwa bali kuvikwa makao yetu ya mbinguni ili kwamba kile kipatikanacho na mauti kimezwe na uzima.
5 Now he that hath prepared us for this very thing is God; who also gave to us the Spirit as the pledge.
Basi Mungu ndiye alitufanya kwa ajili ya jambo lilo hilo naye ametupa Roho Mtakatifu kuwa amana, akituhakikishia ahadi ya kile kijacho.
6 We have courage, therefore, always, and know that while we are at home in the body, we are absent from the Lord;
Kwa hiyo siku zote tunalo tumaini, hata ingawa tunajua kwamba wakati tukiwa katika mwili huu, tuko mbali na Bwana,
7 for we walk by faith, not by sight; but we have courage,
kwa maana twaenenda kwa imani wala si kwa kuona.
8 and are well pleased rather to be absent from the body, and to be at home with the Lord.
Naam, tunalo tumaini na ingekuwa bora zaidi kuuacha mwili huu na kwenda kukaa na Bwana.
9 Wherefore we also strive that, whether at home or absent, we may be approved by him.
Kwa hiyo, kama tuko katika mwili huu au tuko mbali nao, lengo letu ni kumpendeza Bwana.
10 For we must all be made manifest before the judgment-seat of Christ, that each one may receive the things done in his body, according to what he did, whether good or bad.
Kwa kuwa sisi sote tutasimama mbele ya kiti cha hukumu cha Kristo, ili kila mmoja apate kulipwa kwa ajili ya yale ambayo yametendwa katika mwili wake, yakiwa mema au mabaya.
11 Knowing therefore the fear of the Lord, we persuade men; but to God we have been made manifest, and I hope have been made manifest in your consciences also.
Basi, kwa kuwa tunajua kumcha Bwana, tunajitahidi kuwavuta wengine. Lakini Mungu anatufahamu dhahiri, nami natumaini kwamba tu dhahiri katika dhamiri zenu pia.
12 For we are not again commending ourselves to you, but giving you occasion to glory on our behalf; that ye may have somewhat to answer those who glory in outward appearance, and not in heart.
Sio kwamba tunajaribu kujistahilisha kwenu tena, lakini tunataka kuwapa nafasi ili mwone fahari juu yetu mweze kuwajibu hao wanaoona fahari juu ya mambo yanayoonekana badala ya mambo yaliyo moyoni.
13 For whether we were beside ourselves, it was for God; or whether we are in our sound mind, it is for you.
Kama tumerukwa na akili, ni kwa ajili ya Mungu; kama tuna akili timamu, ni kwa ajili yenu.
14 For the love of Christ constraineth us, because we thus judged, that if one died for all, then all died;
Kwa kuwa upendo wa Kristo unatutia nguvu, kwa sababu tunasadiki kuwa mmoja alikufa kwa ajili ya wote, kwa hiyo wote walikufa.
15 and he died for all, that they who live should no longer live to themselves, but to him who died for their sakes, and rose again.
Naye alikufa kwa ajili ya watu wote, ili kwamba wote wanaoishi wasiishi tena kwa ajili ya nafsi zao wenyewe, bali kwa ajili yake yeye aliyekufa na kufufuliwa tena kwa ajili yao.
16 So that we henceforth know no one according to the flesh; and if we have even known Christ according to the flesh, yet now we no longer know him.
Hivyo tangu sasa hatumwangalii mtu yeyote kwa mtazamo wa kibinadamu. Ingawa wakati fulani tulimwangalia Kristo kwa namna ya kibinadamu, hatumwangalii tena hivyo.
17 Therefore, if any one is in Christ, he is a new creation; the old things have passed away; behold, all things have become new.
Kwa hiyo kama mtu akiwa ndani ya Kristo, amekuwa kiumbe kipya; ya kale yamepita, tazama, yamekuwa mapya.
18 And all things are from God, who reconciled us to himself by Christ, and gave to us the ministry of reconciliation;
Haya yote yanatokana na Mungu, ambaye ametupatanisha sisi na nafsi yake kwa njia ya Yesu Kristo na kutupata sisi huduma ya upatanisho:
19 seeing that in Christ God was reconciling the world to himself, not reckoning to them their trespasses, and having committed to us the word of reconciliation.
Kwamba Mungu alikuwa ndani ya Kristo akiupatanisha ulimwengu na nafsi yake mwenyewe, akiwa hawahesabii watu dhambi zao. Naye ametukabidhi sisi ujumbe huu wa upatanisho.
20 We then are ambassadors for Christ; as though God were exhorting you by us, in behalf of Christ we entreat you, Be reconciled to God.
Kwa hiyo sisi ni mabalozi wa Kristo, kana kwamba Mungu anawasihi kupitia kwa vinywa vyetu. Nasi twawaomba sana ninyi kwa niaba ya Kristo, mpatanishwe na Mungu.
21 Him, who knew not sin, he made sin for us, that we might become God's righteousness in him.
Kwa maana Mungu alimfanya yeye asiyekuwa na dhambi kuwa dhambi kwa ajili yetu, ili sisi tupate kufanywa haki ya Mungu kwake yeye.

< 2 Corinthians 5 >