< 1 Timothy 2 >

1 I exhort then, first of all, that supplications, prayers, intercessions, and giving of thanks be made for all men;
Kwanza kabisa, basi naomba dua, sala, maombi na sala za shukrani zitolewe kwa Mungu kwa ajili ya watu wote,
2 for kings, and all that are in authority; that we may lead a quiet and tranquil life in all godliness and propriety.
kwa ajili ya wafalme na wote wenye mamlaka, ili tupate kuishi maisha ya utulivu na amani pamoja na uchaji wa Mungu na mwenendo mwema.
3 For this is good and acceptable in the sight of God our Saviour,
Jambo hili ni jema na lampendeza Mungu Mwokozi wetu,
4 whose will is that all men should be saved, and come to the knowledge of the truth.
ambaye anataka watu wote waokolewe na wapate kuujua ukweli.
5 For there is one God, and one mediator between God and men, the man Christ Jesus,
Maana yuko Mungu mmoja, na pia yuko mmoja anayewapatanisha watu na Mungu, binadamu Kristo Yesu,
6 who gave himself a ransom for all; to which the testimony was to be borne in its own due times,
ambaye alijitoa mwenyewe kuwakomboa watu wote. Huo ulikuwa uthibitisho, wakati ufaao ulipowadia.
7 whereunto I was appointed a herald and an apostle, (I speak the truth, I lie not, ) a teacher of the gentiles in faith and truth.
Kwa sababu hiyo mimi nilitumwa niwe mtume na mwalimu wa watu wa mataifa, niutangaze ujumbe wa imani na ukweli. Nasema ukweli; sisemi uongo!
8 I desire, then, that the men pray in every place, lifting up holy hands, without wrath and doubting.
Basi, popote mnapokutana kufanya ibada nataka wanaume wasali, watu waliojitolea kweli na ambao wanaweza kuinua mikono yao wakisali bila hasira wala ubishi.
9 In like manner also, that women, in seemly attire, adorn themselves with modesty and sobriety, not with braided hair, and gold, or pearls, or costly apparel;
Hali kadhalika, nawataka wanawake wawe wanyofu na wenye busara kuhusu mavazi yao; wavae sawasawa na si kwa urembo wa mitindo ya kusuka nywele, kujipamba kwa dhahabu, lulu au mavazi ya gharama kubwa,
10 but, as becometh women professing godliness, with good works.
bali kwa matendo mema kama iwapasavyo wanawake wamchao Mungu.
11 Let the woman learn in silence with all subjection.
Wanawake wanapaswa kukaa kimya na kuwa wanyenyekevu wakati wa kujifunza.
12 But I suffer not the woman to teach, nor to have authority over the man, but to be in silence.
Mimi simruhusu mwanamke amfundishe au amtawale mwanamume; anapaswa kukaa kimya.
13 For Adam was first formed, then Eve.
Maana Adamu aliumbwa kwanza, halafu Hawa.
14 And Adam was not deceived; but the woman being deceived fell into transgression.
Na wala si Adamu aliyedanganywa; bali mwanamke ndiye aliyedanganywa, akaivunja sheria ya Mungu.
15 But she will be saved through child-bearing, if they continue in faith, and love, and holiness, with sobriety.
Hata hivyo, mwanamke ataokolewa kwa kupata watoto, kama akidumu katika imani, upendo, utakatifu na unyofu.

< 1 Timothy 2 >