< Romans 3 >

1 Then what advantage does the Jew have? Or what is the profit of circumcision?
Kisha ni faida gani aliyo nayo Myahudi? Na faida ya tohara ni nini?
2 Much in every way. Because first of all, they were entrusted with the oracles of God.
Ni vyema sana kwa kila njia. Awali ya yote, Wayahudi walikabidhiwa ufunuo kutoka kwa Mungu.
3 For what if some were without faith? Will their lack of faith nullify the faithfulness of God?
Lakini, itakuwaje iwapo baadhi ya Wayahudi hawakuwa na imani? Je, kutokuamini kwao kutafanya uaminifu wa Mungu kuwa batili?
4 Absolutely not. Let God be found true, but every human being a liar. As it is written, "That you may be justified in your words, and prevail when you judge."
La hasha. Badala yake, acha Mungu aonekane kuwa kweli, hata kama kila mtu ni mwongo. Kama ilivyokuwa imeandikwa, “Ya kwamba uweze kuonekana kuwa mwenye haki katika maneno yako, na uweze kushinda uingiapo katika hukumu.”
5 But if our unrighteousness commends the righteousness of God, what will we say? Is God unrighteous who inflicts wrath? (I am speaking in human terms).
Lakini ikiwa uovu wetu unaonesha haki ya Mungu, tuseme nini? Mungu si dhalimu atoapo ghadhabu yake, je yupo hivyo? Naongea kutokana na mantiki ya kibinadamu.
6 Absolutely not. For then how will God judge the world?
La hasha! Ni jinsi gani basi Mungu atauhukumu ulimwengu?
7 For if the truth of God through my lie abounded to his glory, why am I also still judged as a sinner?
Lakini ikiwa kweli ya Mungu kupitia uongo wangu hutoa sifa tele kwa ajili yake, kwa nini ningali bado nahukumiwa kama mwenye dhambi?
8 And Why not (as we are slanderously reported, and as some affirm that we say), "Let us do evil, that good may come?" Their condemnation is just.
Kwa nini tusiseme, kama tulivyosingiziwa na kama wengine wanavyothibitisha kwamba tunasema, “Tufanye uovu, ili mema yaje”? Hukumu juu yao ni ya haki.
9 What then? Are we better than they? No, in no way. For we previously warned both Jews and Greeks, that they are all under sin.
Ni nini basi? Tunajitetea wenyewe? Hapana kabisa. Kwa kuwa sisi tayari tumewatuhumu Wayahudi na Wayunani wote pamoja, ya kuwa wapo chini ya dhambi.
10 As it is written, "There is no one righteous; no, not one."
Hii ni kama ilivyoandikwa: “Hakuna mwenye haki, hata mmoja.
11 "There is no one who understands. There is no one who seeks after God.
Hakuna mtu ambaye anaelewa. Hakuna mtu ambaye anamtafuta Mungu.
12 They have all turned aside. They have together become unprofitable. There is no one who does good, there is not even one."
Wote wamegeuka. Wao kwa pamoja wamekuwa hawana maana. Hakuna atendaye mema, la, hata mmoja.
13 "Their throat is an open tomb. With their tongues they have used deceit." "Viper's poison is under their lips;"
Makoo yao ni kaburi lililo wazi. Ndimi zao zimedanganya. Sumu ya nyoka ipo chini ya midomo yao.
14 "Whose mouth is full of cursing and bitterness."
Vinywa vyao vimejaa laana na uchungu.
15 "Their feet are swift to shed blood.
Miguu yao ina mbio kumwaga damu.
16 Destruction and calamity are in their paths.
Uharibifu na mateso yapo katika njia zao.
17 The way of peace, they have not known."
Watu hawa hawajajua njia ya amani.
18 "There is no fear of God before their eyes."
Hakuna hofu ya Mungu mbele ya macho yao.”
19 Now we know that whatever things the law says, it speaks to those who are under the law, that every mouth may be closed, and all the world may be brought under the judgment of God.
Sasa tunajua kwamba chochote sheria isemacho, husema na wale walio chini ya sheria. Hii ni ili kwamba kila kinywa kifungwe, na hivyo kwamba ulimwengu wote uweze kuwajibika kwa Mungu.
20 Because by the works of the law, no flesh will be justified in his sight. For through the law comes the knowledge of sin.
Hii ni kwa sababu hakuna mwili utakaohesabiwa haki kwa matendo ya sheria mbele za macho yake. Kwa kuwa kupitia Sheria huja ufahamu wa dhambi.
21 But now apart from the law, a righteousness of God has been revealed, being testified by the Law and the Prophets;
Lakini sasa pasipo sheria, haki ya Mungu imejulikana. Ilishuhudiwa kwa sheria na Manabii,
22 even the righteousness of God through faith in Jesus Christ to all who believe. For there is no distinction,
hiyo ni, haki ya Mungu kupitia imani katika Yesu Kristo kwa wale wote wanaoamini. Maana hakuna tofauti.
23 for all have sinned, and fall short of the glory of God;
Kwa kuwa wote wamefanya dhambi, na kupungukiwa na utukufu wa Mungu.
24 being justified freely by his grace through the redemption that is in Christ Jesus;
Wamehesabiwa haki bure kwa neema yake kwa njia ya ukombozi ulio katika Kristo Yesu.
25 whom God set forth whom God displayed publicly as a mercy seat, through faith in his blood, for a demonstration of his righteousness, because in God's forbearance he had passed over the sins previously committed;
Kwa maana Mungu alimtoa Kristo Yesu awe upatanisho kwa njia ya imani katika damu yake. Alimtoa Kristo kama ushahidi wa haki yake, kwa sababu ya kuziachilia dhambi zilizopita
26 to demonstrate his righteousness at this present time, so that he would be just, and the justifier of him who has faith in Jesus.
katika uvumilivu wake. Haya yote yalitokea ili kuonesha haki yake wakati huu wa sasa. Hii ilikuwa ili aweze kujithibitisha mwenyewe kuwa haki, na kuonesha kwamba humhesabia haki mtu yeyote kwa sababu ya imani katika Yesu.
27 Where then is the boasting? It is excluded. By what manner of law? Of works? No, but by a law of faith.
Kuwapi basi kujisifu? Kumetengwa. Kwa misingi ipi? Misingi ya matendo? Hapana, lakini kwa misingi ya imani.
28 For we maintain that one is justified by faith apart from the works of the law.
Hivyo tunahitimisha kwamba mtu huhesabiwa haki kwa imani pasipo matendo ya sheria.
29 Or is God for Jews only? Is he not the God of the non-Jews also? Yes, of the non-Jews also,
Au Mungu ni Mungu wa Wayahudi tu? Je yeye si Mungu wa watu wa Mataifa pia? Ndiyo, wa mataifa pia.
30 since indeed there is one God who will justify the circumcised by faith, and the uncircumcised through faith.
Ikiwa kwa kweli Mungu ni mmoja, atawahesabia haki walio wa tohara kwa imani, na wasiotahiriwa kwa njia ya imani.
31 Do we then nullify the law through faith? Absolutely not. No, we establish the law.
Je sisi twaibatilisha sheria kwa imani? La hasha! Kinyume cha hayo, sisi twaithibitisha sheria.

< Romans 3 >