< Psalms 1 >

1 Blessed is the one who doesn't follow the advice of the wicked, or take the path of sinners, or join in with scoffers.
Amebarikiwa mtu yule asiye enenda katika ushauri wa waovu, au kusimama katika njia ya wenye dhambi, au kukaa katika kusanyiko la wenye mizaha.
2 But his delight is in the law of YHWH, and on his law he meditates day and night.
Bali yeye huifurahia sheria ya Yahwe, na huitafakari sheria yake mchana na usiku.
3 He will be like a tree planted by the streams of water, that brings forth its fruit in its season, whose leaf also does not wither, and whatever he does shall prosper.
Atakuwa kama mti uliopandwa karibu na mkondo wa maji ambao huzaa matunda yake kwa majira yake, ambao majani yake hayakauki; lolote afanyalo litafanikiwa.
4 Not so with the wicked; instead, they are like the chaff which the wind drives away.
Waovu hawako hivyo, wao badala yake ni kama makapi yapeperushwayo na upepo.
5 Therefore the wicked shall not stand in the judgment, nor sinners in the congregation of the righteous.
Kwa hivyo waovu hawatasimama katika hukumu, wala wenye dhambi katika kusanyiko la wenye haki.
6 For YHWH knows the way of the righteous, but the way of the wicked shall perish.
Kwa kuwa Yahweh huikubali njia ya wenye haki, njia ya waovu itaangamizwa.

< Psalms 1 >