< Psalms 64 >

1 [For the Chief Musician. A Psalm by David.] Hear my voice, God, in my complaint. Preserve my life from fear of the enemy.
Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi. Ee Mungu, unisikie ninapoeleza lalamiko langu, uyahifadhi maisha yangu kutokana na vitisho vya adui.
2 Hide me from the conspiracy of the wicked, from the noisy crowd of the ones doing evil;
Unifiche kutokana na shauri la siri la waovu, kutokana na zile kelele za kundi la watenda mabaya.
3 who sharpen their tongue like a sword, and aim their arrows, deadly words,
Wananoa ndimi zao kama panga na kuelekeza maneno yao kama mishale ya kufisha.
4 to shoot innocent men from ambushes. They shoot at him suddenly and fearlessly.
Hurusha mishale kutoka kwenye mavizio kwa mtu asiye na hatia, humrushia ghafula bila woga.
5 They encourage themselves in evil plans. They talk about laying snares secretly. They say, "Who will see them?"
Kila mmoja humtia moyo mwenzake katika mipango mibaya; huzungumza juu ya kuficha mitego yao, nao husema, “Ni nani ataiona?”
6 They plot injustice; they hide a well-conceived plan. Surely man's mind and heart are cunning.
Hufanya shauri baya la dhuluma na kusema, “Tumebuni mpango mkamilifu!” Hakika nia na moyo wa mwanadamu vina hila.
7 But God will shoot at them. They will be suddenly struck down with an arrow.
Bali Mungu atawapiga kwa mishale, nao ghafula wataangushwa.
8 Their own tongues shall ruin them. All who see them will shake their heads.
Atageuza ndimi zao wenyewe dhidi yao na kuwaleta kwenye maangamizi; wote wawaonao watatikisa vichwa vyao kwa dharau.
9 All humankind shall be afraid. They shall declare the work of God, and shall wisely ponder what he has done.
Wanadamu wote wataogopa, watatangaza kazi za Mungu na kutafakari yale aliyoyatenda.
10 The righteous shall be glad in YHWH, and shall take refuge in him. All the upright in heart shall praise him.
Wenye haki na wafurahi katika Bwana, na wakimbilie kwake; wanyofu wote wa moyo na wamsifu yeye!

< Psalms 64 >