< Psalms 46 >

1 [For the Chief Musician. By the sons of Korah. According to Alamoth.] God is our refuge and strength, a very present help in trouble.
Mungu kwetu ni kimbilio la usalama na nguvu, upatikanao tele wakati wa mateso.
2 Therefore we won't be afraid, though the earth changes, though the mountains are shaken into the heart of the seas;
Hivyo hatutaogopa, hata kama dunia italazimika kubadilika, hata kama milima italazimika kutetemeka na kuangukia kwenye mtima wa bahari, hata kama maji yatavuma kwa kishindo kikuu,
3 though its waters roar and are troubled, though the mountains tremble with their swelling. (Selah)
hata kama milima itatetemeka kwa vurugu ya maji. (Selah)
4 There is a river, the streams of which make the city of God glad, the holy place of the tents of the Most High.
Kuna mto, mikondo yake huufanya mji wa Mungu kufurahi, mahali patakatifu pa hema ya Aliye Juu.
5 God is in her midst. She shall not be moved. God will help her at dawn.
Mungu yuko katikati yake; naye hatasogezwa; Mungu atamsaidia, naye atafanya hivyo asubuhi na mapema.
6 The nations raged. The kingdoms were moved. He lifted his voice, and the earth melted.
Mataifa yalikasirika na falme zikataharuki; yeye alipaza sauti yake, na nchi ikayeyuka.
7 YHWH of hosts is with us. The God of Jacob is our refuge. (Selah)
Yahwe wa majeshi yuko pamoja nasi; Mungu wa Yakobo ni kimbilio letu la usalama. (Selah)
8 Come, see YHWH's works, what desolations he has made in the earth.
Njoni, mtazame matendo ya Yahwe, uharibifu alioufanya juu ya nchi.
9 He makes wars cease throughout the earth. He breaks the bow, and shatters the spear. He burns the chariots in the fire.
Anaisitisha vita kwenye nchi; yeye anauvunja upinde na kuikata vipande vipande mishale; anazichoma ngao.
10 "Be still, and know that I am God. I will be exalted among the nations. I will be exalted in the earth."
Mkae kimya na mjue kuwa mimi ni Mungu; nitainuliwa juu ya nchi.
11 YHWH of hosts is with us. The God of Jacob is our refuge. (Selah)
Mungu wa majeshi yuko pamoja nasi; Mungu wa Yakobo ni kimbilio letu la usalama. Serah

< Psalms 46 >