< Psalms 29 >

1 [A Psalm by David.] Ascribe to YHWH, you sons of the mighty, ascribe to YHWH glory and strength.
Mpeni sifa Yahwe, enyi wana wa Mungu! Mpeni sifa Yahwe kwa ajili ya utukufu wake na nguvu.
2 Ascribe to YHWH the glory due to his name. Worship YHWH in holy array.
Mpeni Yahwe utukufu ambao jina lake linastahili. Mpigieni magoti Yahwe katika mapambo ya utakatifu.
3 The voice of YHWH is on the waters. The God of glory thunders, even YHWH on many waters.
Sauti ya Yahwe imesikika zaidi ya maji; Mungu wa radi ya utukufu, radi yaYahwe i juu ya maji mengi.
4 The voice of YHWH is powerful. The voice of YHWH is full of majesty.
Sauti ya Yahwe ina nguvu; sauti ya Yahwe ni kuu.
5 The voice of YHWH breaks the cedars. Yes, YHWH breaks in pieces the cedars of Lebanon.
Sauti ya Yahwe huivunja mierezi; Yahwe huivunja vipande vipande mierezi ya Lebanon.
6 He makes them also to skip like a calf; Lebanon and Sirion like a young, wild ox.
Yeye huifanya Lebanoni kuruka kama ndama wa ng'ombe na Sirioni kama mwana wa nyati.
7 The voice of YHWH strikes with flashes of lightning.
Sauti ya Yahwe hutoa miale ya moto.
8 The voice of YHWH shakes the wilderness. YHWH shakes the wilderness of Kadesh.
Sauti ya Yahwe hutetemesha Jangwa; Yahwe hutetemesha jangwa la Kadeshi.
9 The voice of YHWH makes the large trees tremble, and strips the forests bare. In his temple everything says, "Glory."
Sauti ya Yahwe huufanya miti mikubwa kutikisika na huipukutisha misitu. Kila mmoja katika hekalu lake husema, “Utukufu!”
10 YHWH sat enthroned at the Flood. Yes, YHWH sits as King forever.
Yahwe hukaa kama mfalme juu ya mafuriko; Yahwe hukaa kama mfalme milele.
11 YHWH will give strength to his people. YHWH will bless his people with peace.
Yahwe huwatia nguvu watu wake; Yahwe huwa bariki watu wake na amani.

< Psalms 29 >