< Psalms 142 >

1 [A contemplation by David, when he was in the cave. A Prayer.] I cry with my voice to YHWH. With my voice, I ask YHWH for mercy.
Kwa sauti yangu namlilia Yahwe anisaidie; kwa sauti yangu naomba kwa ajili ya neema ya Yahwe.
2 I pour out my complaint before him. I tell him my troubles.
Namwaga malalamiko yangu mbele zake; ninamwambia shida zangu.
3 When my spirit was overwhelmed within me, you knew my path. In the way in which I walk, they have hidden a snare for me.
Roho yangu inapokuwa dhaifu ndani yangu, wewe unajua mapito yangu. Kwenye njia niipitayo wamenifichia mtego.
4 Look on my right, and see; for there is no one who is concerned for me. Refuge has fled from me. No one cares for my soul.
Natazama kulia kwangu na sioni yeyote anayenijali. Sina pa kukimbilia; hakuna anayejali kuhusu uhai wangu.
5 I cried to you, YHWH. I said, "You are my refuge, my portion in the land of the living."
Nilikuita wewe, Yahwe; nikasema, “Wewe ni kimbilio langu, fungu langu katika nchi ya walio hai.
6 Listen to my cry, for I am in desperate need. Deliver me from my persecutors, for they are stronger than me.
Sikia kuita kwangu, maana nimeshushwa chini sana; uniokoe dhidi ya watesi wangu, maana wana nguvu kuliko mimi.
7 Bring my soul out of prison, that I may give thanks to your name. The righteous will surround me, for you will be good to me.
Uitoe nafsi yangu kifungoni ili niweze kulishukuru jina lako. Wenye haki watakusanyika karibu nami kwa sababu umekuwa mwema kwangu.”

< Psalms 142 >