< Psalms 141 >

1 [A Psalm by David.] YHWH, I have called on you. Come to me quickly. Listen to my voice when I call to you.
Ee Yahwe, ninakulilia wewe; uje upesi kwangu. Unisikilize nikuitapo.
2 Let my prayer be set before you like incense; the lifting up of my hands like the evening sacrifice.
Maombi yangu na yawe kama uvumba mbele zako; mikono yangu iliyoinuliwa na iwe kama dhabihu ya jioni.
3 Set a watch, YHWH, before my mouth. Keep the door of my lips.
Ee Yahwe, uweke mlinzi kinywani mwangu; mngojezi malangoni pa midomo yangu.
4 Do not incline my heart to any evil thing, to practice deeds of wickedness with men who work iniquity. Do not let me eat of their delicacies.
Usiruhusu tamaa ya moyo wangu kutamani uovu wowote wala kushiriki katika matendo ya dhambi na watu waishio maovuni. Nisile vyakula vyao vya anasa.
5 Let the righteous strike me, it is kindness; let him reprove me, it is like oil on the head; do not let my head refuse it; Yet my prayer is always against evil deeds.
Mwenye haki na anipige; nao utakuwa ni wema kwangu. Anirudi; itakuwa kama mafuta kichwani pangu; kichwa changu na kisikatae kupokea. Lakini maombi yangu siku zote yatakuwa dhidi ya matendo yao mauvu.
6 Their judges are thrown down by the sides of the rock. They will hear my words, for they are well spoken.
Viongozi wao watatupwa chini toka juu mlimani; watayasikia maneno yangu kuwa ni matamu.
7 "As when one plows and breaks up the earth, our bones are scattered at the mouth of Sheol." (Sheol h7585)
Watalazimika kusema, “Kama vile jembe moja livunjapo ardhi, hivyo mifupa yetu imesambaratishwa kinywani pa kuzimu.” (Sheol h7585)
8 For my eyes are on you, YHWH. In you, I take refuge. Do not leave my soul destitute.
Hakika macho yangu yanakutazama wewe, Yahwe, Bwana; katika wewe napata kimbilio; usiiache nafsi yangu.
9 Keep me from the snare which they have laid for me, from the traps of evildoers.
Unilinde dhidi ya mitego waliyoiweka kwa ajili yangu, na matanzi yao watendao maovu.
10 Let the wicked fall together into their own nets, while I pass by.
Waovu na waangukie kwenye nyavu zao wenywe pindi mimi nitorokapo.

< Psalms 141 >