< Matthew 13 >

1 On that day Jesus went out of the house, and sat by the seaside.
Siku hiyohiyo, Yesu alitoka katika ile nyumba, akaenda na kuketi kando ya ziwa.
2 And large crowds gathered to him, so that he entered into a boat, and sat, and all the crowd stood on the beach.
Makundi makubwa ya watu yalimzunguka hata Yesu akapanda mashua, akaketi. Hao watu walisimama kwenye ukingo wa ziwa,
3 And he spoke to them many things in parables, saying, "Look, a farmer went out to sow.
naye Yesu akawaambia mambo mengi kwa mifano. “Sikilizeni! Mpanzi alikwenda kupanda mbegu.
4 And as he sowed, some seeds fell by the roadside, and the birds came and devoured them.
Alipokuwa akipanda, nyingine zilianguka njiani, ndege wakaja wakazila.
5 And others fell on rocky ground, where they did not have much soil, and immediately they sprang up, because they had no depth of earth.
Nyingine zilianguka penye mawe pasipokuwa na udongo mwingi. Zikaota mara kwa kuwa udongo haukuwa na kina.
6 But when the sun had risen, they were scorched. Because they had no root, they withered away.
Jua lilipochomoza, zilichomeka; na kwa kuwa mizizi yake haikuwa na nguvu, zikanyauka.
7 Others fell among thorns, and the thorns grew up and choked them.
Nyingine zilianguka kwenye miti ya miiba, nayo ikakua na kuzisonga.
8 Still others fell on good soil, and yielded fruit: some one hundred times as much, some sixty, and some thirty.
Lakini nyingine zilianguka penye udongo mzuri, zikaota, zikazaa: nyingine punje mia moja, nyingine sitini na nyingine thelathini.
9 He who has ears, let him hear."
Mwenye masikio na asikie!”
10 Then the disciples came, and said to him, "Why do you speak to them in parables?"
Wanafunzi wake wakamwendea, wakamwuliza, “Kwa nini unasema na watu kwa mifano?”
11 And answering, he said to them, "To you it is given to know the mysteries of the kingdom of heaven, but it is not given to them.
Yesu akawajibu, “Ninyi mmejaliwa kuzijua siri za Ufalme wa mbinguni, lakini wao hawakujaliwa.
12 For whoever has, to him will be given, and he will have abundance, but whoever does not have, from him will be taken away even that which he has.
Maana, aliye na kitu atapewa na kuzidishiwa; lakini yule asiye na kitu, hata kile alicho nacho kitachukuliwa.
13 Therefore I speak to them in parables, because seeing they do not see, and hearing, they do not hear, neither do they understand.
Ndiyo maana ninasema nao kwa mifano, kwa sababu wanatazama lakini hawaoni, wanasikiliza lakini hawasikii, wala hawaelewi.
14 And in them the prophecy of Isaiah is fulfilled, which says, 'In hearing you will hear, but will not understand, and seeing you will see, but not perceive.
Kwao yametimia yale aliyosema nabii Isaya: Kusikia mtasikia, lakini hamtaelewa; Kutazama mtatazama, lakini hamtaona.
15 For the heart of this people has grown dull, and their ears are sluggish in hearing, and they have closed their eyes, otherwise they might see with their eyes, and hear with their ears, and understand with their heart, and turn back, and I would heal them.'
Maana akili za watu hawa zimepumbaa, wameyaziba masikio yao, wameyafumba macho yao. La sivyo, wangeona kwa macho yao. wangesikia kwa masikio yao, wangeelewa kwa akili zao, na kunigeukia, asema Bwana, nami ningewaponya.
16 "But blessed are your eyes, for they see; and your ears, for they hear.
“Lakini heri yenu ninyi, maana macho yenu yanaona na masikio yenu yanasikia.
17 For truly I tell you that many prophets and righteous people desired to see the things which you see, and did not see them; and to hear the things which you hear, and did not hear them.
Kweli nawaambieni, manabii na watu wengi wema walitamani kuyaona yale mnayoyaona, wasiyaone, na kuyasikia yale mnayoyasikia, wasiyasikie.
18 "Hear, then, the parable of the farmer.
“Basi, ninyi sikilizeni maana ya mfano huo wa mpanzi.
19 When anyone hears the word of the Kingdom, and does not understand it, the evil one comes, and snatches away that which has been sown in his heart. This is what was sown by the roadside.
Yeyote asikiaye ujumbe wa ufalme bila kuuelewa, ni kama zile mbegu zilizoanguka njiani; yule Mwovu huja na kunyakua kile kilichopandwa moyoni mwake.
20 And what was sown on the rocky places, this is he who hears the word, and immediately with joy receives it;
Ile mbegu iliyopandwa penye mawe ni mfano wa mtu asikiaye ujumbe huo na mara akaupokea kwa furaha.
21 yet he has no root in himself, but endures for a while. When oppression or persecution arises because of the word, immediately he stumbles.
Lakini haumwingii na kuwa na mizizi ndani yake; huendelea kuuzingatia ujumbe huo kwa kitambo tu, na wakati taabu au udhalimu vinapotokea kwa sababu ya ujumbe huo, anakata tamaa mara.
22 And what was sown among the thorns, this is he who hears the word, but the cares of the world and the deceitfulness of riches choke the word, and he becomes unfruitful. (aiōn g165)
Ile mbegu iliyoanguka kati ya miti ya miiba, ni mfano wa mtu asikiaye huo ujumbe, lakini wasiwasi wa ulimwengu huu na anasa za mali huusonga ujumbe huo, naye hazai matunda. (aiōn g165)
23 And what was sown on the good ground, this is he who hears the word, and understands it, who truly bears fruit, and brings forth, some one hundred times as much, some sixty, and some thirty."
Ile mbegu iliyopandwa katika udongo mzuri ni mfano wa mtu ausikiaye ujumbe huo na kuuelewa, naye huzaa matunda; mmoja mia, mwingine sitini na mwingine thelathini.”
24 He set another parable before them, saying, "The kingdom of heaven is like a person who sowed good seed in his field,
Yesu akawaambia watu mfano mwingine: “Ufalme wa mbinguni unafanana na mtu aliyepanda mbegu nzuri katika shamba lake.
25 but while everyone slept, his enemy came and sowed tares also among the wheat, and went away.
Lakini watu wakiwa wamelala, adui yake akaja akapanda magugu kati ya ngano, akaenda zake.
26 But when the blade sprang up and brought forth fruit, then the tares appeared also.
Basi, mimea ilipoota na kuanza kuchanua, magugu pia yakaanza kuonekana.
27 So the servants of the householder came and said to him, 'Sir, did you not sow good seed in your field? Where did these tares come from?'
Watumishi wa yule mwenye shamba wakamwendea, wakamwambia, Mheshimiwa, bila shaka ulipanda mbegu nzuri katika shamba lako. Sasa magugu yametoka wapi?
28 "And he said to them, 'An enemy has done this.' "And the servants asked him, 'Then do you want us to go and gather them up?'
Yeye akawajibu, Adui ndiye aliyefanya hivyo. Basi, watumishi wake wakamwuliza, Je, unataka twende tukayang'oe
29 "But he said, 'No, lest perhaps while you gather up the tares, you root up the wheat with them.
Naye akawajibu, La, msije labda mnapokusanya magugu, mkang'oa na ngano pia.
30 Let both grow together until the harvest, and in the harvest time I will tell the reapers, "First, gather up the tares, and bind them in bundles to burn them; but gather the wheat into my barn."'"
Acheni vikue pamoja mpaka wakati wa mavuno. Wakati huo nitawaambia wavunaji: kusanyeni kwanza magugu mkayafunge mafungumafungu ya kuchomwa. Lakini ngano ikusanyeni mkaiweke ghalani mwangu.”
31 He set another parable before them, saying, "The kingdom of heaven is like a mustard seed which a man took and sowed in his field;
Yesu akawaambia watu mfano mwingine: “Ufalme wa mbinguni unafanana na mbegu ya haradali aliyotwaa mtu mmoja, akaipanda katika shamba lake.
32 which indeed is least of all the seeds. But when it has grown it is larger than the garden plants and becomes a tree, so that the birds of the air come and nest in its branches."
Yenyewe ni ndogo kuliko mbegu zote, lakini ikishaota huwa kubwa kuliko mimea yote. Hukua ikawa mti, na ndege wa angani huja na kujenga viota katika matawi yake.”
33 He spoke another parable to them. "The kingdom of heaven is like yeast, which a woman took, and hid in three measures of meal, until it was all leavened."
Yesu akawaambia mfano mwingine: “Ufalme wa mbinguni umefanana na chachu aliyotwaa mama mmoja, akaichanganya na unga pishi tatu, hata unga wote ukaumuka.”
34 Jesus spoke all these things in parables to the crowds; and without a parable, he did not speak to them,
Yesu aliwaambia watu hayo yote kwa mifano. Hakuwaambia chochote bila kutumia mifano,
35 that it might be fulfilled which was spoken through the prophet, saying, "I will open my mouth in parables; I will utter things hidden since the beginning of the world."
ili jambo lililonenwa na nabii litimie: “Nitasema kwa mifano; nitawaambia mambo yaliyofichika tangu kuumbwa ulimwengu.”
36 Then Jesus sent the crowds away, and went into the house. His disciples came to him, saying, "Explain to us the parable of the tares in the field."
Kisha Yesu aliwaaga wale watu, akaingia nyumbani. Wanafunzi wake wakamwendea, wakamwambia, “Tufafanulie ule mfano wa magugu shambani.”
37 And he answered them, "The one who sows the good seed is the Son of Man,
Yesu akawaambia, “Mpanzi wa zile mbegu nzuri ni Mwana wa Mtu.
38 and the field is the world; and the good seed, these are the children of the Kingdom; and the tares are the children of the evil one,
Lile shamba ni ulimwengu. Zile mbegu nzuri ni watu wale ambao Ufalme ni wao. Lakini yale magugu ni wale watu wa yule Mwovu.
39 and the enemy who sowed them is the devil, and the harvest is the end of the age, and the reapers are angels. (aiōn g165)
Adui aliyepanda yale magugu ni Ibilisi. Mavuno ni mwisho wa nyakati na wavunaji ni malaika. (aiōn g165)
40 As therefore the tares are gathered up and burned with fire; so will it be at the end of the age. (aiōn g165)
Kama vile magugu yanavyokusanywa kuchomwa moto, ndivyo itakavyokuwa mwishoni mwa nyakati; (aiōn g165)
41 The Son of Man will send out his angels, and they will gather out of his Kingdom all things that cause stumbling, and those who do iniquity,
Mwana wa Mtu atawatuma malaika wake wawakusanye kutoka katika Ufalme wake wale wote wenye kusababisha dhambi, na wote wenye kutenda maovu,
42 and will cast them into the furnace of fire. There will be weeping and the grinding of teeth.
na kuwatupa katika tanuru ya moto, na huko watalia na kusaga meno.
43 Then the righteous will shine forth like the sun in the Kingdom of their Father. He who has ears, let him hear.
Kisha, wale wema watang'ara kama jua katika Ufalme wa Baba yao. Sikieni basi, kama mna masikio!
44 "The kingdom of heaven is like a treasure hidden in the field, which a man found, and hid. In his joy, he goes and sells all that he has, and buys that field.
“Ufalme wa mbinguni umefanana na hazina iliyofichika shambani. Mtu mmoja aliigundua, akaificha tena. Alifurahi sana hata akaenda kuuza yote aliyokuwa nayo, akalinunua shamba lile.
45 "Again, the kingdom of heaven is like a man who is a merchant seeking fine pearls,
“Tena, Ufalme wa mbinguni umefanana na mfanyabiashara mmoja mwenye kutafuta lulu nzuri.
46 and having found one pearl of great price, he went and sold all that he had, and bought it.
Alipopata lulu moja ya thamani kubwa, alienda akauza yote aliyokuwa nayo, akainunua lulu ile.
47 "Again, the kingdom of heaven is like a dragnet, that was cast into the sea, and gathered some fish of every kind,
“Tena, Ufalme wa mbinguni unafanana na wavu uliotupwa baharini, ukanasa samaki wa kila aina.
48 which, when it was filled, they drew up on the beach. They sat down, and gathered the good into containers, but the bad they threw away.
Ulipojaa, watu waliuvuta pwani, wakaketi, wakachagua samaki wazuri wakawaweka ndani ya vikapu vyao, na wabaya wakawatupa.
49 So will it be in the end of the world. The angels will come forth, and separate the wicked from among the righteous, (aiōn g165)
Ndivyo itakavyokuwa mwishoni mwa nyakati: malaika watatokea, watawatenganisha watu wabaya na watu wema, (aiōn g165)
50 and will cast them into the furnace of fire. There will be the weeping and the grinding of teeth."
na kuwatupa hao wabaya katika tanuru ya moto. Huko watalia na kusaga meno.”
51 "Have you understood all these things?" They answered him, "Yes."
Yesu akawauliza, “Je, mmeelewa mambo haya yote?” Wakamjibu, “Naam.”
52 And he said to them, "Therefore, every scribe who has been made a disciple in the kingdom of heaven is like a man who is a householder, who brings out of his treasure new and old things."
Naye akawaambia, “Hivyo basi, kila mwalimu wa Sheria aliye mwanafunzi wa Ufalme wa mbinguni anafanana na mwenye nyumba atoaye katika hazina yake vitu vipya na vya kale.”
53 And it happened that when Jesus had finished these parables, he departed from there.
Yesu alipomaliza kusema mifano hiyo alitoka mahali hapo,
54 And coming into his own country, he taught them in their synagogue, so that they were astonished, and said, "Where did this man get this wisdom, and these mighty works?
akaenda kijijini kwake. Huko akawa anawafundisha watu katika sunagogi hata wakashangaa, wakasema, “Huyu amepata wapi hekima hii na maajabu?
55 Is not this the carpenter's son? Is not his mother called Mary, and his brothers, James and Joseph and Simon and Judas?
Je, huyu si yule mwana wa seremala? Je, mama yake si anaitwa Maria, na ndugu zake si kina Yakobo, Yosefu, Simoni na Yuda?
56 And are not all of his sisters with us? Where then did this man get all of these things?"
Na dada zake je, si wote wako hapa pamoja nasi? Basi amepata wapi haya yote?”
57 And they were offended by him. But Jesus said to them, "A prophet is not without honor, except in his own country, and in his own house."
Basi, wakawa na mashaka naye. Lakini Yesu akawaambia, “Nabii hakosi kuheshimiwa, isipokuwa katika nchi yake na nyumbani mwake!”
58 And he did not do many mighty works there because of their unbelief.
Kwa hiyo, hakutenda miujiza mingi pale kwa sababu ya kutoamini kwao.

< Matthew 13 >