< Mark 6 >
1 And he went out from there and came into his own country, and his disciples followed him.
Na akaondoka hapo na kwenda mjini kwao, na wanafunzi wake wakamfuata.
2 And when the Sabbath had come, he began to teach in the synagogue, and many hearing him were astonished, saying, "Where did this man get these things?" and, "What is the wisdom that is given to this man, that such mighty works come about by his hands?
Sabato ilipofika, alianza kufundisha katika Sinagogi. Watu wengi walimsikia na wakashangazwa. Wakasema, “Amepata wapi mafundisho haya?” “Ni hekima gani hii aliyopewa?” “Anatendaje miujiza hii kwa mikono yake?”
3 Is not this the carpenter, the son of Mary, and brother of James, Josi, Judas, and Simon? Are not his sisters here with us?" They were offended at him.
“Je huyu si yule seremala, mwana wa Mariamu na ndugu yao kina Yakobo, Yose, Yuda na Simioni? Je dada zake si wanaishi papa hapa pamoja nasi?” Na hawakufurahishwa na Yesu.
4 Jesus said to them, "A prophet is not without honor, except in his own country, and among his own relatives, and in his own house."
Yesu akawaambia, “Nabii hakosi heshima, isipokuwa katika mji wake na miongoni mwa ndugu zake na nyumbani mwake.”
5 And he could do no mighty work there, except that he laid his hands on a few sick people, and healed them.
Hakuweza kutenda miujiza hapo, ila aliwawekea mikono wagonjwa wachache akawaponya.
6 And he was amazed because of their unbelief. And he went around the villages teaching.
Alishangazwa sana kwa sababu ya kutokuamini kwao. Kisha alivitembelea vijiji vya jirani akifundisha.
7 And he called to himself the twelve, and began to send them out two by two; and he gave them authority over the unclean spirits.
Aliwaita wale wanafunzi kumi na wawili akaanza kuwatuma wawili wawili. Aliwapa mamlaka juu ya pepo wachafu,
8 And he commanded them that they should take nothing for their journey, except a staff only: no bread, no pack, no money in their belts,
na kuwaamuru wasichukue chochote wanapokwenda isipokuwa fimbo tu. Wasichukue mkate, wala mkoba, wala fedha kibindoni;
9 but to wear sandals, and not to put on two tunics.
lakini wavae viatu, na siyo kanzu mbili.
10 And he said to them, "Wherever you enter into a house, stay there until you depart from there.
Na akawaambia, “Nyumba yoyote mtakayoingia, kaeni hapo mpaka mtakapoondoka.
11 And if any place will not receive you or listen to you, as you depart from there, shake off the dust that is under your feet for a testimony against them."
Na mji wowote usipowapokea wala kuwasikiliza, ondokeni kwao, kung'uteni mavumbi ya miguu yenu, iwe ushuhuda kwao.”
12 So they went out and proclaimed that all should repent.
Nao wakaenda wakitangaza watu watubu na kuacha dhambi zao.
13 They cast out many demons, and anointed many with oil who were sick, and healed them.
Waliwafukuza pepo wengi, na waliwapaka mafuta wagonjwa na wakaponywa.
14 King Herod heard this, for his name had become known, and he said, "John the Baptist has risen from the dead, and therefore these powers are at work in him."
Mfalme Herode aliposikia hayo, kwa kuwa jina la Yesu lilikuwa limejulikana sana. Baadhi walisema, “Yohana mbatizaji amefufuka na kwa sababu hiyo, hii nguvu ya miujiza inafanya kazi ndani yake.”
15 But others said, "He is Elijah." Others said, "He is a prophet, like one of the prophets."
Baadhi yao wakasema, “Huyu ni Eliya,” Bado wengine wakasema, “Huyu ni nabii, kama mmoja wa wale manabii wa zamani.”
16 But Herod, when he heard this, said, "This is John, whom I beheaded. He has risen."
Lakini Herode aliposikia haya akasema, “Yohana, niliyemkata kichwa amefufuliwa.”
17 For Herod himself had sent out and arrested John, and bound him in prison for the sake of Herodias, his brother Philip's wife, for he had married her.
Maana Herode mwenyewe aliagiza Yohana akamatwe na alimfunga gerezani kwa sababu ya Herodia (mke wa kaka yake Filipo) kwa sababu yeye alikuwa amemuoa.
18 For John said to Herod, "It is not lawful for you to have your brother's wife."
Kwa maana Yohana alimwambia Herode, “Si halali kumuoa mke wa kaka yako.”
19 So Herodias set herself against him, and desired to kill him, but she could not,
Lakini Herodia alianza kumchukia na alikuwa akitaka kumuua, lakini hakuweza,
20 for Herod feared John, knowing that he was a righteous and holy man, and kept him safe. And when he heard him, he was very perplexed, but he heard him gladly.
maana Herode alimwogopa Yohana; alijua kwamba ni mwenye haki mtu mtakatifu, na alimwacha salama. Na alipoendelea kumsikiliza alihuzunika sana, lakini alifurahi kumsikiliza.
21 And then a convenient day came, that Herod on his birthday gave a supper for his nobles, the high officers, and the leaders of Galilee.
Hata ilipofika wakati mwafaka ikiwa imekaribia siku ya kuzaliwa Herode akawaandalia moafisa wake karamu, na makamanda, na viongozi wa Galilaya.
22 And when the daughter of Herodias herself came in and danced, she pleased Herod and those sitting with him. The king said to the young woman, "Ask me whatever you want, and I will give it to you."
Ndipo binti wa Herodia akaingia na kucheza mbele yao, akamfurahisha Herode na wageni walioketi wakati wa chakula cha jioni. Ndipo mfalme akamwambia binti, “Niombe chochote unachotaka nami nitakupa.”
23 And he swore to her, "Whatever you ask me, I will give you, up to half of my kingdom."
Akamwapia na kusema, chochote utakachoniomba, nitakupa, hata nusu ya ufalme wangu.”
24 So she went out, and said to her mother, "What should I ask?" And she said, "The head of John the baptizer."
Akatoka nje akamuuliza mama yake, “Niombe nini?” Akasema, “Kichwa cha Yohana Mbatizaji.”
25 And she came in immediately with haste to the king, and asked, "I want you to give me right now the head of John the Baptist on a platter."
Na mara moja akaingia kwa mfalme akaanza kusema, “Nataka unipatie ndani ya sahani, kichwa cha Yohana Mbatizaji.”
26 And the king was exceedingly sorry, but for the sake of his oaths, and those reclining, he did not wish to refuse her.
Mfalme alisikitishwa sana, lakini kwa sababu ya kiapo chake na kwa ajili ya wageni, hakuweza kumkatalia ombi lake.
27 So immediately the king sent out a soldier of his guard, and commanded to bring John's head, and he went and beheaded him in the prison,
Hivyo, mfalme akatuma askari kati ya walinzi wake na kuwaagiza kwenda kumletea kichwa cha Yohana. Mlinzi alikwenda kumkata kichwa akiwa kifungoni.
28 and brought his head on a platter, and gave it to the young woman; and the young woman gave it to her mother.
Akakileta kichwa chake kwenye sahani na kumpatia binti, na binti akampa mama yake.
29 And when his disciples heard this, they came and took up his corpse, and placed it in a tomb.
Na wanafunzi wake waliposikia hayo, walikwenda kuuchukua mwili wake wakaenda kuuzika kaburini.
30 Then the apostles gathered themselves together to Jesus, and they told him all things, whatever they had done, and whatever they had taught.
Na mitume, walikusanyika pamoja mbele ya Yesu, wakamweleza yote waliyofanya na waliyoyafundisha.
31 And he said to them, "Come away by yourselves to an isolated place, and rest awhile." For there were many coming and going, and they had no leisure so much as to eat.
Naye akawaambia, “Njooni wenyewe mahali pa faragha na tupumzike kwa muda.” Watu wengi walikuwa wanakuja na kuondoka, hata hawakupata nafasi ya kula.
32 So they went away in the boat to an isolated place by themselves.
Hivyo wakapanda mashua wakaenda mahali pa faragha peke yao.
33 But they saw them going, and many recognized him and ran there on foot from all the cities and they arrived before them.
Lakini waliwaona wakiondoka na wengi wakawatambua, kwa pamoja walikimbia kwa miguu kutoka miji yote, nao wakafika kabla yao.
34 And he came out, saw a large crowd, and he had compassion on them, because they were like sheep without a shepherd, and he began to teach them many things.
Walipofika pwani, aliona umati mkubwa na akawahurumia, kwa sababu walikuwa kama kondoo wasiokuwa na mchungaji. Na akaanza kuwafundisha mambo mengi.
35 And when it was late in the day, his disciples came to him, and said, "This place is desolate, and it is late in the day.
Muda ulipoendelea sana, wanafunzi wakamjia wakamwambia,”Hapa ni mahali pa faragha na muda umeendelea.
36 Send them away, that they may go into the surrounding country and villages, and buy themselves something to eat."
Uwaage waende miji ya jirani na vijiji ili wakajinunulie chakula.”
37 But he answered them, "You give them something to eat." And they said to him, "Are we to go and buy two hundred denarii worth of bread, and give them something to eat?"
Lakini akawajibu akisema, “Wapeni ninyi chakula.” Wakamwambia, “Tunaweza kwenda na kununua mikate yenye thamani ya dinari mia mbili na kuwapa wale?”
38 He said to them, "How many loaves do you have? Go see." When they knew, they said, "Five, and two fish."
Akawambia,” Mna mikate mingapi? Nendeni mkaangalie.” walipopata wakamwambia, “Mikate mitano na samaki wawili.”
39 He commanded them that everyone should sit down in groups on the green grass.
Akawaamuru watu waketi katika makundi juu ya majani mabichi.
40 They sat down in ranks, by hundreds and by fifties.
Wakawaketisha katika makundi; makundi ya mamia kwa hamsini.
41 He took the five loaves and the two fish, and looking up to heaven, he blessed and broke the loaves, and he gave to his disciples to set before them, and he divided the two fish among them all.
Kisha akachukua mikate mitano na samaki wawili, na kutazama mbinguni, akaibariki kisha akawapa wanafunzi waweke mbele ya umati. Na kisha aligawa samaki wawili kwa watu wote.
42 They all ate, and were filled.
Walikula wote hadi wakatosheka.
43 They took up twelve baskets full of broken pieces and also of the fish.
Walikusanya vipande vya mikate iliyobaki, Vikajaa vikapu kumi na viwili, na pia vipande vya samaki.
44 Those who ate the loaves were five thousand men.
Na walikuwa wanaume elfu tano waliokula mikate.
45 And immediately he made his disciples get into the boat, and to go ahead to the other side, to Bethsaida, while he himself was sending the crowd away.
Mara akawaambia wapande kwenye mashua waende sehemu nyingine, hadi Bethsaida, wakati Yeye akiwaaga makutano.
46 After he had taken leave of them, he went up the mountain to pray.
Walipokuwa wamekwisha kuondoka, akaenda mlimani kuomba.
47 When evening had come, the boat was in the midst of the sea, and he was alone on the land.
Kulipokuwa jioni, na mashua yao wakati huo ikiwa katikati ya bahari, naye alikuwa peke yake nchi kavu.
48 He saw them distressed in rowing, for the wind was against them. In the watch between three and six in the morning he came to them, walking on the sea, and he would have passed by them,
Na aliwaona wakitaabika kupiga makasia kwa sababu upepo uliwazuia. Ilipokaribia asubuhi akawaendea, akitembea juu ya maji, na alitaka kuwapita.
49 but they, when they saw him walking on the sea, supposed that it was a ghost, and began to scream;
Lakini walipomwona anatembea juu ya maji, wakaingiwa na wasiwasi wakidhani ni mzimu hata wakapiga kelele.
50 for they all saw him, and were troubled. But he immediately spoke with them, and said to them, "Cheer up. It is I. Do not be afraid."
kwa sababu walimwona wakajawa na hofu. Mara akasema nao akawaambia, “Muwe wajasiri! ni mimi! Msiwe na hofu.”
51 And he got into the boat with them, and the wind ceased. And they were completely profusely astonished among themselves;
Akaingia ndani ya mashua, na upepo ukaacha kuvuma, nao wakamshangaa kabisa.
52 for they had not understood about the loaves, but their hearts were hardened.
Hivyo hawakuwa wameelewa maana ya ile mikate. Maana akili zao zilikuwa na uelewa mdogo.
53 When they had crossed over, they came to land at Gennesaret, and moored to the shore.
Nao walipovuka ng'ambo, walifika nchi ya Genesareti mashua ikatia nanga.
54 When they had come out of the boat, immediately the people recognized him,
Walipotoka nje ya mashua, mara wakamtambua.
55 and ran around that whole region, and began to bring those who were sick, on their mats, to where they heard he was.
Wakakimbia kutangaza katika mkoa mzima na wakaanza kuwaleta wagonjwa kwa machela, kila waliposikia anakuja.
56 Wherever he entered, into villages, or into cities, or into the country, they placed the sick in the marketplaces, and begged him that they might touch just the fringe of his garment; and everyone who touched him were made well.
Popote alipoingia katika vijiji, au mjini, au katika nchi, waliwaweka wagonjwa mahali pa soko, na wakamsihi awaruhusu kugusa pindo la vazi lake. Na wote waliomgusa waliponywa.