< Luke 1 >

1 Since many have undertaken to set in order a narrative concerning those matters which have been fulfilled among us,
Wengi wamejitahidi kuweka katika mpangilio simulizi kuhusu masuala ambayo yametimizwa kati yetu,
2 even as those who from the beginning were eyewitnesses and servants of the word delivered them to us,
kama walivyotupatia sisi, ambao tangu mwanzo ni mashahidi wa macho na watumishi wa ujumbe.
3 it seemed good to me also, having traced the course of all things accurately from the first, to write to you in order, most excellent Theophilus;
Hivyo nami pia, baada ya kuchuguza kwa uangalifu chanzo cha mambo haya yote tokea mwanzo - nimeona ni vema kwangu pia kukuandikia katika mpangilio wake - mheshimiwa sana Theofilo.
4 that you might know the certainty concerning the things in which you were instructed.
Ili kwamba uweze kujua ukweli wa mambo uliyofundishwa.
5 There was in the days of Herod, the king of Judea, a certain priest named Zechariah, of the division of Abijah. He had a wife of the daughters of Aaron, and her name was Elizabeth.
Katika siku za Herode, mfalme wa Yudea, palikuwa na kuhani fulani aliyeitwa Zekaria, wa ukoo wa Abiya. Mke wake alitoka kwa binti za Haruni, na jina lake aliitwa Elizabeti.
6 They were both righteous before God, walking blamelessly in all the commandments and ordinances of the Lord.
Wote walikuwa wenye haki mbele za Mungu; walitembea bila lawama katika amri zote na maagizo ya Bwana.
7 But they had no child, because Elizabeth was barren, and they both were well advanced in years.
Lakini hawakuwa na mtoto, kwasababu Elizabethi alikuwa tasa, na kwa wakati huu wote wawili walikuwa wazee sana.
8 Now it happened, while he was performing the priest's office before God in the order of his division,
Sasa ilitokea kwamba Zakaria alikuwa katika uwepo wa Mungu, akiendelea na wajibu wa kikuhani katika utaratibu wa zamu yake.
9 according to the custom of the priest's office, his lot was to enter into the temple of the Lord and burn incense.
Kulingana na desturi ya kuchagua ni kuhani yupi atakayehudumu, alikuwa amechaguliwa kwa kura kuingia katika hekalu la Bwana na hivyo angefukiza uvumba.
10 And the whole crowd of people were praying outside at the hour of incense.
Kundi lote la watu lilikuwa likiomba nje wakati wa kufukizwa kwa ufumba.
11 An angel of the Lord appeared to him, standing on the right side of the altar of incense.
Sasa malaika wa Bwana alimtokea na kasimama upande wa kulia wa madhabahu ya kufukizia.
12 Zechariah was troubled when he saw him, and fear fell upon him.
Zakaria alitishika alipomuona; hofu ikamwangukia.
13 But the angel said to him, "Do not be afraid, Zechariah, because your request has been heard, and your wife, Elizabeth, will bear you a son, and you are to name him John.
Lakini malaika akamwambia, “Usiogope Zakaria, kwasababu maombi yako yamesikika. Mke wako Elizabeth atakuzalia mwana. Jina lake utamwita Yohana.
14 You will have joy and gladness; and many will rejoice at his birth.
Utakuwa na furaha na uchangamfu, na wengi watakufurahia kuzaliwa kwake.
15 For he will be great in the sight of the Lord, and he must never drink wine or strong drink, and he will be filled with the Holy Spirit, even from his mother's womb.
Kwa kuwa atakuwa mkuu mbele ya macho ya Bwana. Hatakunywa divai au kinywaji kikali, na atakuwa amejazwa na Roho Mtakatifu tangu tumboni mwa mama yake.
16 He will turn many of the children of Israel to the Lord, their God.
Na watu wengi wa Israel watageuzwa kwa Bwana Mungu wao.
17 He will go before him in the spirit and power of Elijah, 'to turn the hearts of the fathers to the children,' and the disobedient to the wisdom of the just; to make ready a people prepared for the Lord."
Atakwenda mbele za uso wa Bwana katika roho na nguvu ya Eliya. Atafanya hivi ili kurejesha mioyo ya baba kwa watoto, ili kwamba wasiotii wataenenda katika hekima ya wenye haki. Atafanya hivi kuweka tayari kwa Bwana watu ambao wameandaliwa kwa ajili yake.”
18 Zechariah said to the angel, "How can I be sure of this? For I am an old man, and my wife is well advanced in years."
Zakaria akamwambia malaika, “Nitawezaje kujua hili? Kwasababu mimi ni mzee na mke wangu miaka yake imekuwa mingi sana.”
19 The angel answered him, "I am Gabriel, who stands in the presence of God. I was sent to speak to you, and to bring you this good news.
Malaika akajibu na kumwambia, “Mimi ni Gabrieli, ambaye husimama mbele za Mungu. Nilitumwa kukwambia, kukuletea habari hii njema.
20 And look, you will be silent and not able to speak, until the day that these things will happen, because you did not believe my words, which will be fulfilled in their proper time."
Na tazama, hutaongea, utakuwa kimya, hutaweza kuongea mpaka siku ile mambo haya yatakapotokea. Hii ni kwasababu ulishindwa kuamini maneno yangu ambayo yatatimizwa kwa wakati mwafaka.”
21 The people were waiting for Zechariah, and they were wondering why he was delayed in the temple.
Sasa watu walikuwa wakimsubiri Zakaria. Walishangazwa kwamba alikuwa anatumia muda mwingi hekaluni.
22 When he came out, he could not speak to them, and they perceived that he had seen a vision in the temple. He continued making signs to them, and remained mute.
Lakini alipotoka nje, hakuweza kuongea nao. Wakatambua kwamba alikuwa amepata maono alipokuwa hekaluni. Aliendelea kuonesha ishara na alibaki kimya.
23 It happened, when the days of his service were fulfilled, he departed to his house.
Ikatokea kwamba siku za huduma yake zilipokwisha aliondoka kurudi nyumbani kwake.
24 After these days Elizabeth, his wife, conceived, and she hid herself five months, saying,
Baada ya Zakaria kurudi nyumbani kutoka kwenye huduma yake hekaluni, mke wake akawa mjamzito. Naye hakutoka nyumbani mwake kwa muda wa miezi mitano. Akasema,
25 "Thus has the Lord done to me in the days in which he looked at me, to take away my disgrace among people."
“Hili ndilo amabalo Bwana amefanya kwangu aliponitazama kwa upendeleo ili kuiondoa aibu yangu mbele za watu.”
26 Now in the sixth month, the angel Gabriel was sent from God to a city of Galilee, named Nazareth,
Sasa, katika mwezi wa sita wa mimba ya Elizabeti, Mungu alimwambia malaika Gabrieli kwenda kwenye mji wa Galilaya uitwao Nazareti,
27 to a virgin pledged to be married to a man whose name was Joseph, of the house of David. The virgin's name was Mary.
kwa bikra aliyekuwa ameposwa na mwanaume ambaye jina lake lilikuwa Yusufu. Yeye alikuwa wa ukoo wa Daudi, na jina la bikra huyo lilikuwa Mariamu.
28 Having come in, the angel said to her, "Greetings, favored one. The Lord is with you."
Akaja kwake na akasema, “Salaam, wewe uliyepokea neema kuu! Bwana amependezwa nawe.”
29 But when she saw him, she was greatly troubled at the saying, and considered what kind of greeting this might be.
Lakini maneno ya malaika yalimchanganya na hakuelewa kwa nini malaika alisema salaam hii ya ajabu kwake.
30 The angel said to her, "Do not be afraid, Mary, for you have found favor with God.
Malaika akamwambia, “Usiogope, Mariamu, maana umepata neema kutoka kwa Mungu.
31 And look, you will conceive in your womb, and bring forth a son, and will call his name 'Jesus.'
Na tazama, utabeba mimba katika tumbo lako na utazaa mwana. Nawe utamwita jina lake 'Yesu.'
32 He will be great, and will be called the Son of the Most High. The Lord God will give him the throne of his father, David,
Atakuwa mkuu na ataitwa Mwana wa Aliye Juu Sana. Bwana Mungu atampa kiti cha enzi cha Daudi baba yake.
33 and he will reign over the house of Jacob forever. There will be no end to his Kingdom." (aiōn g165)
Atatawala juu ya ukoo wa Yakobo milele na ufalme wake hautakuwa na mwisho. (aiōn g165)
34 Mary said to the angel, "How can this be, seeing I am a virgin?"
Mariamu akamwambia malaika, hili litatokea kwa namna gani, maana sijawahi kulala na mwanaume yeyote?
35 The angel answered her, "The Holy Spirit will come on you, and the power of the Most High will overshadow you. Therefore also the holy one who is born will be called the Son of God.
Malaika akajibu na akamwambia, “Roho Mtakatifu atakujia juu yako, na nguvu ya Aliye Juu Sana itakuja juu yako. Kwa hiyo, mtakatifu atakayezaliwa ataitwa Mwana wa Mungu.
36 And look, Elizabeth, your relative, also has conceived a son in her old age; and this is the sixth month with her who was called barren.
Na tazama, ndugu yako Elizabeti anaujauzito wa mwana kwenye umri wake wa uzee. Huu ni mwezi wa sita kwake, ambaye alikuwa anaitwa mgumba.
37 For with God nothing will be impossible."
Maana hakuna lisilowezekana kwa Mungu.”
38 And Mary said, "See, the handmaid of the Lord; be it to me according to your word." The angel departed from her.
Mariamu akasema, “Tazama, mimi ni mtumishi wa kike wa Bwana. Acha iwe hivyo kwangu sawa sawa na ujumbe wako.” Kisha malaika akamwacha.
39 Mary arose in those days and went into the hill country with haste, into a city of Judah,
Ndipo katika siku hizo Mariamu aliondoka na kwa haraka alikwenda katika nchi ya vilima, kwenye mji katika nchi ya Yudea.
40 and entered into the house of Zechariah and greeted Elizabeth.
Alikwenda nyumbani mwa Zekaria na akamsalimia Elizabeti.
41 It happened, when Elizabeth heard Mary's greeting, that the baby leaped in her womb, and Elizabeth was filled with the Holy Spirit.
Sasa, ilitokea kwamba Elizabeti aliposikia salamu ya Mariamu, mtoto tumboni mwake akaruka, na Elizabeti akajazwa na Roho Mtakatifu.
42 She called out with a loud voice, and said, "Blessed are you among women, and blessed is the fruit of your womb.
Akapaza sauti yake na kusema kwa sauti kuu, “umebarikiwa wewe zaidi miongoni mwa wanawake, na mtoto aliyemo tumboni mwako amebarikiwa.
43 Why am I so favored, that the mother of my Lord should come to me?
Na imekuwaje kwangu kwamba, mama wa Bwana wangu ilipasa aje kwangu?
44 For look, when the voice of your greeting came into my ears, the baby leaped in my womb for joy.
Kwa kuwa tazama, iliposikika masikoni mwangu sauti ya kusalimia kwako, mtoto tumboni mwangu akaruka kwa furaha.
45 Blessed is she who believed, for there will be a fulfillment of the things which have been spoken to her from the Lord."
Na amebarikiwe mwanamke yule ambaye aliamini ya kwamba ungetokea ukamilifu wa mambo yale aliyoambiwa kutoka kwa Bwana.”
46 Mary said, "My soul magnifies the Lord.
Mariamu akasema, nafsi yangu inamsifu Bwana,
47 And my spirit rejoices in God my Savior,
na roho yangu imefurahi katika Mungu Mwokozi wangu.
48 for he has looked at the humble state of his servant girl. For look, from now on all generations will call me blessed.
Kwa maana ameiangalia hali ya chini ya mtumishi wake wa kike. Tazama, tangu sasa katika vizazi vyote wataniita mbarikiwa.
49 For he who is mighty has done great things for me, and holy is his name.
Kwa maana yeye aliyemweza amefanya mambo makubwa kwangu, na jina lake ni takatifu.
50 His mercy is for generations of generations on those who fear him.
Rehema yake inadumu toka kizazi hata kizazi kwa wale wanao mheshimu yeye.
51 He has shown strength with his arm. He has scattered the proud in the imagination of their hearts.
Ameonesha nguvu kwa mkono wake; amewatawanya wale ambao walijivuna juu ya mawazo ya mioyo yao.
52 He has put down princes from their thrones. And has exalted the lowly.
Amewashusha chini wana wa wafalme toka katika viti vyao vya enzi na kuwainua juu walio na hali ya chini.
53 He has filled the hungry with good things. He has sent the rich away empty.
Aliwashibisha wenye njaa kwa vitu vizuri, bali matajiri amewafukuza mikono mitupu.
54 He has given help to Israel, his servant, that he might remember mercy,
Ametoa msaada kwa Israeli mtumishi wake, ili kukumbuka kuonesha rehema
55 As he spoke to our fathers, to Abraham and his offspring forever." (aiōn g165)
(kama alivyosema kwa baba zetu) kwa Abrahamu na uzao wake milele.” (aiōn g165)
56 Mary stayed with her about three months, and then returned to her house.
Mariamu alikaa na Elizabeti yapata miezi mitatu hivi ndipo akarudi nyumbani kwake.
57 Now the time that Elizabeth should give birth was fulfilled, and she brought forth a son.
Sasa wakati ulikuwa umewadia kwa Elizabeti kujifungua mtoto wake na akajifungua mtoto wa kiume.
58 Her neighbors and her relatives heard that the Lord had magnified his mercy towards her, and they rejoiced with her.
Jirani zake na ndugu zake walisikia jinsi Bwana alivyoikuza rehema kwake, na wakafurahi pamoja naye.
59 It happened on the eighth day, that they came to circumcise the child; and they would have called him Zechariah, after the name of the father.
Sasa ilitokea siku ya nane kwamnba walikuja kumtahiri mtoto. Ingewapasa kumwita jina lake, “Zekaria,” kwa kuzingatia jina la baba yake,
60 His mother answered, "Not so; but he will be called John."
Lakini mama yake akajibu na kusema, “Hapana; ataitwa Yohana.”
61 They said to her, "There is no one among your relatives who is called by this name."
Wakamwambia, hakuna hata mmoja katika ndugu zako anayeitwa kwa jina hili.”
62 They made signs to his father, what he would have him called.
Wakamfanyia ishara baba yake kuashiria yeye alitaka jina aitwe nani.
63 And he asked for a writing tablet, and wrote, "His name is John." And they were all amazed.
Baba yake akahitaji kibao cha kuandikia, na akaandika, “Jina lake ni Yohana.” Wote wakashangazwa na hili.
64 His mouth was opened immediately, and his tongue freed, and he spoke, blessing God.
Ghafla mdomo wake ukafunguliwa na ulimi wake ukawa huru. Akaongea na kumsifu Mungu.
65 Fear came on all who lived around them, and all these sayings were talked about throughout all the hill country of Judea.
Hofu ikawajia wote walioishi karibu nao. Mambo haya yakaenea katika nchi yote ya vilima vya Yudea.
66 All who heard them laid them up in their heart, saying, "What then will this child be?" The hand of the Lord was with him.
Na wote walioyasikia wakayatunza mioyoni mwao, wakisema, “Mtoto huyu kuwa wa namna gani?” Kwasababu mkono wa Bwana ulikuwa pamoja naye.
67 His father, Zechariah, was filled with the Holy Spirit, and prophesied, saying,
Baba yake Zekaria alijazwa na Roho Mtakatifu na akatoa unabii, akisema,
68 "Blessed be the Lord, the God of Israel, for he has visited and worked redemption for his people;
“Asifiwe Bwana, Mungu wa Israeli, kwa sababu amesaidia na alishughulikia wokovu kwa watu wake.
69 and has raised up a horn of salvation for us in the house of his servant David
Ametuinulia pembe ya wokovu katika nyumba ya mtumishi wake Daudi, kutoka miongoi mwa mwa ukoo wa mtumishi wake Daudi,
70 (as he spoke by the mouth of his holy prophets who have been from of old), (aiōn g165)
kama alivyosema kwa kinywa cha manabii wake waliokuweko katika nyakati za kale. (aiōn g165)
71 salvation from our enemies, and from the hand of all who hate us;
Atatuoka kutoka kwa adui zetu na kutoka mikononi mwa wote wanaotuchukia.
72 to show mercy towards our fathers, to remember his holy covenant,
Atafanya hivi kuonesha rehema kwa baba zetu, na kukumbuka agano lake takatifu,
73 the oath which he spoke to Abraham, our father,
kiapo alichokisema kwa Abrahamu baba yetu.
74 to grant to us that we, being delivered out of the hand of our enemies, should serve him without fear,
Aliapa kuthibitha kwamba ingewezekana kumtumikia Yeye bila hofu, baada ya kuokolewa kutoka katika mikononi ya adui zetu.
75 In holiness and righteousness before him all our days.
katika utakatifu na haki mbele zake siku zetu zote.
76 And you, child, will be called a prophet of the Most High, for you will go before the Lord to make ready his ways,
Ndiyo, na wewe mtoto, utaitwa nabii wa Aliye Juu Sana, kwa kuwa utaenenda mbele za uso wa Bwana ili kumwandalia njia, kuwaandaa watu kwa ajili ya ujio wake,
77 to give knowledge of salvation to his people by the forgiveness of their sins,
kuwafahamisha watu wake kwamba, wataokolewa kwa njia ya kusamehewa dhambi zao.
78 because of the tender mercy of our God, whereby the dawn from on high will visit us,
Hili litatokea kwa sababu ya huruma ya Mungu wetu, sababu ambayo jua tokea juu litatujia,
79 to shine on those who sit in darkness and the shadow of death; to guide our feet into the way of peace."
kuangaza kwao wakaao gizani na katika uvuli wa mauti. Atafanya hivi kuiongoza miguu yetu kwenye njia ya amani.”
80 The child was growing, and becoming strong in spirit, and was in the desert until the day of his public appearance to Israel.
Sasa, yule mtoto akakua na kuwa mwenye nguvu rohoni na alikaa nyikani mpaka siku ya kujitokeza kwake kwa Israeli.

< Luke 1 >