< John 3 >

1 Now there was a man of the Pharisees named Nicodemus, a ruler of the Jewish people.
Basi palikuwa na mtu mmoja Farisayo, jina lake Nikodemo, mmoja wa Baraza la Wayahudi lililotawala.
2 This man came to him at night, and said to him, "Rabbi, we know that you are a teacher come from God, for no one can do these signs that you do, unless God is with him."
Huyu alimjia Yesu usiku akamwambia, “Rabi, tunajua kuwa wewe ni mwalimu uliyetumwa na Mungu, kwa maana hakuna mtu awezaye kufanya miujiza hii uifanyayo wewe, kama Mungu hayuko pamoja naye.”
3 Jesus answered him, "Truly, truly, I tell you, unless one is born again he cannot see the Kingdom of God."
Yesu akamjibu, “Amin, amin nakuambia, hakuna mtu anayeweza kuuona Ufalme wa Mungu kama hajazaliwa mara ya pili.”
4 Nicodemus said to him, "How can anyone be born when he is old? Can he enter a second time into his mother's womb, and be born?"
Nikodemo akauliza, “Awezaje mtu kuzaliwa wakati akiwa mzee? Hakika hawezi kuingia mara ya pili kwenye tumbo la mama yake ili azaliwe!”
5 Jesus answered, "Truly, truly, I tell you, unless one is born of water and Spirit he cannot enter into the Kingdom of God.
Yesu akamwambia, “Amin, amin nakuambia, hakuna mtu yeyote anayeweza kuingia Ufalme wa Mungu kama hajazaliwa kwa maji na kwa Roho.
6 That which is born of the flesh is flesh. That which is born of the Spirit is spirit.
Mwili huzaa mwili, lakini Roho huzaa roho.
7 Do not be surprised that I said to you, 'You must be born again.'
Kwa hiyo usishangae ninapokuambia huna budi ‘kuzaliwa mara ya pili.’
8 The wind blows where it wants to, and you hear its sound, but do not know where it comes from and where it is going. So is everyone who is born of the Spirit."
Upepo huvuma popote upendapo. Mvumo wake unausikia lakini huwezi ukafahamu utokako wala uendako. Ndivyo ilivyo kwa kila mtu aliyezaliwa na Roho.”
9 Nicodemus answered and said to him, "How can these things be?"
Nikodemo akamuuliza, “Mambo haya yanawezekanaje?”
10 Jesus answered him, "Are you the teacher of Israel, and do not understand these things?
Yesu akamwambia, “Wewe ni mwalimu mashuhuri wa Waisraeli, nawe huelewi mambo haya?
11 Truly, truly, I tell you, we speak that which we know, and testify of that which we have seen, but you do not accept our testimony.
Amin, amin ninakuambia, sisi tunazungumza lile tunalolijua na tunashuhudia lile tuliloliona. Lakini ninyi watu hamkubali ushuhuda wetu.
12 If I told you earthly things and you do not believe, how will you believe if I tell you heavenly things?
Nimewaambia mambo ya duniani, nanyi hamkuniamini, mtaniaminije basi nitakapowaambia mambo ya mbinguni?
13 And no one has ascended into heaven, but he who descended out of heaven, the Son of Man, who is in heaven.
Hakuna mtu yeyote aliyekwenda mbinguni isipokuwa yeye aliyeshuka kutoka mbinguni, yaani, Mwana wa Adamu.
14 And as Moses lifted up the serpent in the wilderness, even so must the Son of Man be lifted up,
Kama vile Mose alivyomwinua yule nyoka kule jangwani, vivyo hivyo Mwana wa Adamu hana budi kuinuliwa juu.
15 so that everyone who believes in him may have life without end. (aiōnios g166)
Ili kila mtu amwaminiye awe na uzima wa milele. (aiōnios g166)
16 For this is how God loved the world: he gave his only Son, so that everyone who believes in him will not perish but have life without end. (aiōnios g166)
“Kwa maana jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu hata akamtoa Mwanawe wa pekee, ili kila mtu amwaminiye asipotee, bali awe na uzima wa milele. (aiōnios g166)
17 For God did not send his Son into the world to judge the world, but that the world should be saved through him.
Kwa maana Mungu hakumtuma Mwanawe kuuhukumu ulimwengu, bali kupitia kwake ulimwengu upate kuokolewa.
18 The one who believes in him is not judged, but the one who does not believe has been judged already, because he has not believed in the name of the only Son of God.
Yeyote amwaminiye hahukumiwi, lakini asiyeamini amekwisha kuhukumiwa, kwa sababu hakuliamini jina la Mwana pekee wa Mungu.
19 This is the judgment, that the light has come into the world, and people loved the darkness rather than the light, because their works were evil.
Hii ndiyo hukumu kwamba: Nuru imekuja ulimwenguni, nao watu wakapenda giza kuliko nuru kwa sababu matendo yao ni maovu.
20 For everyone who does evil hates the light, and does not come to the light, so that his works will not be exposed.
Kwa kuwa kila atendaye maovu huchukia nuru, wala haji kwenye nuru ili matendo yake maovu yasifichuliwe.
21 But the one who does the truth comes to the light, that his works may be revealed, that they have been done in God."
Lakini yule aishiye kwa ukweli huja kwenye nuru, ili ionekane wazi kwamba matendo yake yametendeka katika Mungu.”
22 After these things, Jesus came with his disciples into the land of Judea. He stayed there with them, and was baptizing.
Baada ya haya, Yesu na wanafunzi wake walikwenda katika nchi ya Uyahudi, nao wakakaa huko kwa muda na kubatiza.
23 Now John also was baptizing in Aenon near Salim, because there was much water there. They came, and were baptized.
Yohana naye alikuwa akibatiza huko Ainoni karibu na Salimu kwa sababu huko kulikuwa na maji tele. Watu wazima wakamjia huko ili kubatizwa.
24 For John was not yet thrown into prison.
(Hii ilikuwa kabla Yohana hajatiwa gerezani).
25 Now a dispute arose between John's disciples with a Jew about purification.
Mashindano yakazuka kati ya baadhi ya wanafunzi wa Yohana na Myahudi mmoja kuhusu suala la desturi ya kunawa kwa utakaso.
26 And they came to John, and said to him, "Rabbi, he who was with you beyond the Jordan, to whom you have testified, look, he is baptizing, and everyone is coming to him."
Wakamwendea Yohana wakamwambia, “Rabi, yule mtu aliyekuwa pamoja nawe ngʼambo ya Mto Yordani, yule uliyeshuhudia habari zake, sasa anabatiza na kila mtu anamwendea!”
27 John answered, "No one can receive anything, unless it has been given to him from heaven.
Yohana akawajibu, “Hakuna mtu yeyote awezaye kupata kitu chochote isipokuwa kile tu alichopewa kutoka mbinguni.
28 You yourselves bear me witness that I said, 'I am not the Christ,' but, 'I have been sent before him.'
Ninyi wenyewe ni mashahidi wangu kwamba nilisema, ‘Mimi si Kristo, ila nimetumwa nimtangulie.’
29 He who has the bride is the bridegroom; but the friend of the bridegroom, who stands and hears him, rejoices greatly because of the bridegroom's voice. So this joy of mine is now complete.
Bibi arusi ni wa bwana arusi. Lakini rafiki yake bwana arusi anayesimama karibu naye na kusikiliza kutoka kwake, hufurahi sana aisikiapo sauti ya bwana arusi. Kwa sababu hii furaha yangu imekamilika.
30 He must increase, but I must decrease.
Yeye hana budi kuwa mkuu zaidi na mimi nizidi kuwa mdogo.”
31 He who comes from above is above all. He who is from the earth belongs to the earth, and speaks of the earth. He who comes from heaven is above all.
“Yeye ajaye kutoka juu yu juu ya yote, yeye aliye wa duniani ni wa dunia, naye huzungumza mambo ya duniani. Yeye aliyekuja kutoka mbinguni, yu juu ya yote.
32 What he has seen and heard, of that he testifies; and no one receives his witness.
Yeye hushuhudia yale aliyoyaona na kuyasikia, lakini hakuna yeyote anayekubali ushuhuda wake.
33 He who has received his witness has set his seal to this, that God is true.
Lakini yeyote anayekubali huo ushuhuda anathibitisha kwamba, Mungu ni kweli.
34 For he whom God has sent speaks the words of God; for he does not give the Spirit by measure.
Yeye aliyetumwa na Mungu husema maneno ya Mungu, kwa kuwa Mungu humtoa Roho pasipo kipimo.
35 The Father loves the Son, and has given all things into his hand.
Baba anampenda Mwana, naye ametia vitu vyote mikononi mwake.
36 Whoever believes in the Son has everlasting life, but whoever refuses to believe in the Son won't see life, but the wrath of God remains on him." (aiōnios g166)
Yeyote anayemwamini Mwana ana uzima wa milele, lakini yeye asiyemwamini Mwana hatauona uzima, bali ghadhabu ya Mungu itakuwa juu yake.” (aiōnios g166)

< John 3 >