< John 16 >
1 "I have said all these things to you so that you may be kept from stumbling.
Nimewaambia mambo haya ili msiweze kukwazwa.
2 They will put you out of the synagogues, but an hour is coming when whoever kills you will think that he is offering a service to God.
Watawatoa nje ya masinagogi; hakika saa inakuja ambayo kila atakayewaua atafikiri kuwa anafanya kazi njema kwa ajili ya Mungu.
3 They will do these things because they have not known the Father or me.
Watawatendea mambo haya kwa sababu hawamfahamu Baba wala hawanifahamu mimi.
4 But I have told you these things, so that when their hour comes, you may remember that I told you about them. I did not tell you these things from the beginning, because I was with you.
Nimewaambia mambo haya ili kwamba wakati ukifika wa haya kutokea, mnaweza kuyakumbuka na jinsi nilivyowaambia muweze wao. Sikuwaambia kuhusu mambo haya tangu mwanzo kwa sababu nilikuwa pamoja nanyi.
5 But now I am going to him who sent me, and none of you asks me, 'Where are you going?'
Japokuwa, sasa naenda kwa yule aliyenituma; lakini hakuna kati yenu anayeniuliza, “Unaenda wapi?”
6 But because I have told you these things, sorrow has filled your heart.
Kwa sababu nimesema maneno haya kwenu, huzuni imejaa mioyoni mwenu.
7 Nevertheless I tell you the truth: It is to your advantage that I go away, for if I do not go away, the Helper won't come to you. But if I go, I will send him to you.
Hata hivyo, nawaambia ukweli: ni vyema kwenu nikiondoka; kwa maana nisipoondoka, mfariji hatakuja kwen; lakini nikienda ntamtuma kwenu.
8 When he has come, he will convict the world about sin, and about righteousness, and about judgment;
Akija, huyo mfariji ataubitisha ulimwengu kuhusiana na dhambi, kuhusiana na haki na kuhusiana na hukumu.
9 about sin, because they do not believe in me;
Kuhusiana na dhambi, kwa sababu hawakuniamini mimi,
10 about righteousness, because I am going to the Father, and you won't see me any more;
kuhusiana na haki, kwa sababu naenda kwa baba, na hamtaniona tena;
11 about judgment, because the prince of this world has been judged.
na kuhusiana na hukumu kwa sababu mkuu wa ulimwengu huu amehukumiwa.
12 "I have yet many things to tell you, but you cannot bear them now.
Ninayo mengi ya kuwaambia, lakini hamtayaelewa sasa.
13 However when he, the Spirit of truth, has come, he will guide you into all truth, for he will not speak on his own; but whatever he hears he will speak, and he will declare to you things that are coming.
Lakini, yeye, Roho wa kweli, akija, atawaongoza katika kweli yote; kwa kuwa hataongea kwa ajili yake mwenyewe; lakini yoyote atakayoyasikia, atayasema mambo hayo; na atayadhihirisha kwenu mambo yatakayokuja.
14 He will glorify me, for he will take from what is mine, and will declare it to you.
Yeye atanitukuza mimi, kwa sababu atayachukua mambo yangu na atayatangaza kwenu.
15 All things that the Father has are mine; that is why I said that he takes of mine, and will declare it to you.
Vitu vyote alivyonavyo Baba ni vyangu; kwa hiyo, nimesema kwamba Roho atachukua mambo yangu na atayadhihirisha kwenu.
16 A little while, and you will no longer see me. Again a little while, and you will see me."
Bado muda mfupi, hamtaniona tena; na baada ya muda mfupi tena, mtaniona.”
17 Some of his disciples therefore said to one another, "What is this that he says to us, 'A little while, and you won't see me, and again a little while, and you will see me;' and, 'Because I go to the Father?'"
Baadhi ya wanafunzi wake wakaambizana, “Ni nini anachotuambia, “muda mfupi, na hamtaniona tena,' na, kisha, mda mfupi mtaniona,' na, 'kwa sababu naenda kwa Baba?”
18 So they kept asking, "What is this that he says, 'A little while?' We do not know what he is saying."
Kwa hiyo wakasema, “Ni kitu gani anachosema, 'Bado mda mfupi'? Hatujui asemavyo.”
19 Jesus knew that they wanted to ask him, so he said to them, "Do you inquire among yourselves concerning this, that I said, 'A little while, and you won't see me, and again a little while, and you will see me?'
Yesu aliona kuwa walitamani kumuuliza, naye akawaambia, “Mnajiuliza wenyewe kuhusu hili, nilivyosema, 'Bado muda mfupi, hamtaniona tena; na baada ya muda mfupi mtaniona'?
20 Truly, truly, I tell you, that you will weep and lament, but the world will rejoice. You will be sorrowful, but your sorrow will be turned into joy.
Amin, amin, nawaambia, mtalia na kuomboleza, lakini ulimwengu utashangilia, mtakuwa na huzuni lakini huzuni yenu itageuka kuwa furaha.
21 A woman, when she gives birth, has pain, because her time has come. But when she has delivered the child, she does not remember the anguish any more, for the joy that a human being is born into the world.
Mwanamke anakuwa na huzuni wakati anapokuwa na uchungu kwa sababu wakati wa kujifungua umefika; lakini anapojifungua mtoto, hakumbuki tena maumivu kwa sababu ya furaha yake kwamba mtoto amezaliwa duniani.
22 Therefore you have sorrow now, but I will see you again, and your heart will rejoice, and no one will take your joy away from you.
Ninyi pia mna huzuni sasa, lakini nitawaona tena; na mioyo yenu itafurahi na hakuna atakayeweza kuiondoa furaha yenu.
23 "And in that day you will ask nothing of me. Truly, truly I tell you, whatever you may ask of the Father in my name, he will give it to you.
Siku hiyo hamtaniuliza maswali. Amin, Amin, nawaambia, Mkiomba lolote kwa Baba, atawapa kwa jina langu.
24 Until now, you have asked nothing in my name. Ask, and you will receive, that your joy may be made full.
Mpaka sasa hamjaomba lolote kwa jina langu; ombeni, nanyi mtapokea ili kwamba furaha yenu ikamilike.
25 I have spoken these things to you in figures of speech. The hour is coming when I will no more speak to you in figures of speech, but will tell you plainly about the Father.
Nimezungumza na ninyi kwa lugha isiyoeleweka, lakini saa inakuja ambapo sitazungumza kwa lugha isiyoeleweka lakini badala yake nitawaambia waziwazi kuhusu Baba.
26 In that day you will ask in my name, and I am not saying to you that I will ask the Father on your behalf,
Siku hiyo mtaomba kwa jina langu, na siwaambii kwamba nitaomba kwa Baba kwa ajili yenu;
27 for the Father himself loves you, because you have loved me, and have believed that I came forth from God.
Kwa kuwa Baba mwenyewe anawapenda kwa sababu mmenipenda mimi na kwa sababu mmeniamini kuwa nimetoka kwa Baba.
28 I came forth from the Father and have come into the world. Again, I leave the world, and go to the Father."
Nilitoka kwa Baba na nimekuja ulimwenguni; tena, naondoka ulimwenguni na ninaenda kwa Baba”.
29 His disciples said to him, "Look, now you are speaking plainly and not in any figure of speech.
Wanafunzi wake wakamwambia, “Unaona, sasa unaongea wazi wazi na hautumii mafumbo.
30 Now we know that you know all things and do not need anyone to question you. By this we believe that you came forth from God."
Sasa, tunajua kwamba unajua mambo yote, na hauhitaji mtu yoyote akuulize maswali. Kwa sababu hii tunaamini kuwa unatoka kwa Mungu.
31 Jesus answered them, "Do you now believe?
Yesu akawajibu, “Sasa mmeamini?”
32 Look, the time is coming, and has come, that you will be scattered, everyone to his own place, and you will leave me alone. But I am not alone, because the Father is with me.
Tazama, saa inakuja, ndiyo na hakika imefika, ambapo mtatawanyika kila mmoja na kwa wa kwao mtaniacha mwenyewe. Lakini siko peke yangu kwa sababu Baba yupo nami.
33 I have told you these things, that in me you may have peace. In the world you have oppression; but cheer up. I have overcome the world."
Nawaambia mambo haya ili kwamba ndani yangu muwe na amani. Duniani mna matatizo, lakini jipeni moyo, nimeushinda ulimwengu.