< Joel 3 >

1 "For, look, in those days, and in that time, when I restore the fortunes of Judah and Jerusalem,
“Katika siku hizo na wakati huo, nitakaporejesha neema ya Yuda na Yerusalemu,
2 I will gather all nations, and will bring them down into the Valley of Jehoshaphat; and I will execute judgment on them there for my people, and for my heritage, Israel, whom they have scattered among the nations. They have divided my land,
nitayakusanya mataifa yote na kuyaleta katika Bonde la Yehoshafati Hapo nitaingia kwenye hukumu dhidi yao kuhusu urithi wangu, watu wangu Israeli, kwa kuwa waliwatawanya watu wangu miongoni mwa mataifa na kuigawa nchi yangu.
3 and have cast lots for my people, and have given a boy for a prostitute, and sold a girl for wine, that they may drink.
Wanawapigia kura watu wangu na kuwauza wavulana ili kupata makahaba; waliwauza wasichana ili wapate kunywa mvinyo.
4 "Yes, and what are you to me, Tyre, and Sidon, and all the regions of Philistia? Will you repay me? And if you repay me, I will swiftly and speedily return your repayment on your own head.
“Sasa una nini dhidi yangu, ee Tiro na Sidoni, nanyi nchi zote za Ufilisti? Je, mnanilipiza kwa yale niliyoyafanya? Kama mnalipa, mimi nitalipiza juu ya vichwa vyenu kwa kasi na kwa haraka yale mliyoyatenda.
5 Because you have taken my silver and my gold, and have carried my finest treasures into your temples,
Kwa kuwa mlichukua fedha na dhahabu yangu pia mkabeba hazina zangu nzuri sana mkapeleka kwenye mahekalu yenu.
6 and have sold the people of Judah and the people of Jerusalem to the people of the Greeks, that you may remove them far from their border.
Mliwauza watu wa Yuda na Yerusalemu kwa Wayunani, ili kwamba mpate kuwapeleka mbali na nchi yao.
7 Look, I will stir them up out of the place where you have sold them, and will return your repayment on your own head;
“Tazama nitawaamsha kutoka zile sehemu mlizowauza, nami nitawalipiza juu ya vichwa vyenu kile mlichofanya.
8 and I will sell your sons and your daughters into the hands of the people of Judah, and they will sell them to the men of Sheba, to a faraway nation, for YHWH has spoken it."
Nitawauza wana wenu na binti zenu kwa watu wa Yuda, nao watawauza kwa Waseba, taifa lililo mbali.” Bwana amesema.
9 Proclaim this among the nations: "Prepare for war. Stir up the mighty men. Let all the warriors draw near. Let them come up.
Tangazeni hili miongoni mwa mataifa: Jiandaeni kwa vita! Amsha askari! Wanaume wote wapiganaji wasogee karibu na kushambulia.
10 Beat your plowshares into swords, and your pruning hooks into spears. Let the weak say, 'I am strong.'
Majembe yenu yafueni yawe panga na miundu yenu ya kukatia iwe mikuki. Aliye dhaifu na aseme, “Mimi nina nguvu!”
11 Hurry and come, all you surrounding nations, and gather yourselves together." Cause your mighty ones to come down there, YHWH.
Njooni haraka, ninyi mataifa yote kutoka pande zote, kusanyikeni huko. Shusha wapiganaji wako, Ee Bwana!
12 "Let the nations arouse themselves, and come up to the Valley of Jehoshaphat; for there will I sit to judge all the surrounding nations.
“Mataifa na yaamshwe; na yasonge mbele kuelekea Bonde la Yehoshafati, kwa kuwa nitaketi mahali pale kuhukumu mataifa yote yaliyoko kila upande.
13 Put in the sickle; for the harvest is ripe. Come, tread, for the winepress is full, the vats overflow, for their wickedness is great."
Tia mundu, kwa kuwa mavuno yamekomaa. Njooni, mkanyage zabibu, kwa kuwa shinikizo la kukamua zabibu limejaa na mapipa yanafurika: kwa kuwa uovu wao ni mkubwa!”
14 Multitudes, multitudes in the valley of decision. For the day of YHWH is near, in the valley of decision.
Umati mkubwa, umati mkubwa katika bonde la uamuzi! Kwa kuwa siku ya Bwana ni karibu katika bonde la uamuzi.
15 The sun and the moon are darkened, and the stars withdraw their shining.
Jua na mwezi vitatiwa giza, na nyota hazitatoa mwanga wake tena.
16 YHWH will roar from Zion, and thunder from Jerusalem; and the heavens and the earth will shake; but YHWH will be a refuge to his people, and a stronghold to the children of Israel.
Bwana atanguruma kutoka Sayuni na mshindo wa ngurumo kutoka Yerusalemu; dunia na mbingu vitatikisika. Lakini Bwana atakuwa kimbilio la watu wake, ngome imara kwa ajili ya watu wa Israeli.
17 "So you will know that I am YHWH your God, who dwells in Zion, my holy mountain. Then Jerusalem will be holy, and no strangers will pass through her any more.
“Ndipo mtakapojua kwamba Mimi, Bwana Mungu wenu, nakaa Sayuni, mlima wangu mtakatifu. Yerusalemu utakuwa mtakatifu; kamwe wageni hawatavamia tena.
18 It will happen in that day, that the mountains will drop down sweet wine, the hills will flow with milk, all the brooks of Judah will flow with waters, and a fountain will come forth from the house of YHWH, and will water the Valley of Shittim.
“Katika siku hiyo milima itadondosha divai mpya, na vilima vitatiririka maziwa; mabonde yote ya Yuda yatatiririka maji. Chemchemi itatiririka kutoka kwenye nyumba ya Bwana na kunywesha Bonde la Shitimu.
19 Egypt will be a desolation, and Edom will be a desolate wilderness, for the violence done to the people of Judah, because they have shed innocent blood in their land.
Lakini Misri itakuwa ukiwa, Edomu itakuwa jangwa tupu, kwa sababu ya jeuri waliofanya kwa watu wa Yuda, ambao katika nchi yao walimwaga damu isiyo na hatia.
20 But Judah will be inhabited forever, and Jerusalem from generation to generation.
Yuda itakaliwa na watu milele na Yerusalemu itadumu vizazi vyote.
21 And I will pardon their bloodguilt, which I have not pardoned, for YHWH dwells in Zion."
Hatia yao ya damu, ambayo sijasamehe, nitasamehe.”

< Joel 3 >