< Hebrews 3 >
1 Therefore, holy brothers, partakers of a heavenly calling, consider the Apostle and High Priest of our confession, Jesus;
Kwa hiyo ndugu watakatifu, mnaoshiriki mwito wa mbinguni, mtafakarini Yesu, mtume na Kuhani Mkuu wa ukiri wetu.
2 who was faithful to him who appointed him, as also was Moses in his house.
Alikuwa mwaminifu kwa yeye aliyemweka, kama vile Mose alivyokuwa mwaminifu katika nyumba yote ya Mungu.
3 For he has been counted worthy of more glory than Moses, just as he who built the house has more honor than the house.
Yesu ameonekana anastahili heshima kubwa kuliko Mose, kama vile mjenzi wa nyumba alivyo wa heshima kubwa kuliko nyumba yenyewe.
4 For every house is built by someone; but he who built all things is God.
Kwa kuwa kila nyumba hujengwa na mtu fulani, lakini Mungu ni mjenzi wa kila kitu.
5 Moses indeed was faithful in all his house as a servant, for a testimony of those things which were afterward to be spoken,
Basi Mose kama mtumishi alikuwa mwaminifu katika nyumba yote ya Mungu, akishuhudia kwa yale ambayo yangetamkwa baadaye.
6 but Christ is faithful as a Son over his house; whose house we are, if we hold fast our confidence and the boast of our hope.
Lakini Kristo ni mwaminifu kama Mwana katika nyumba ya Mungu. Sisi ndio nyumba yake, kama tutashikilia sana ujasiri wetu na tumaini tunalojivunia.
7 Therefore, even as the Holy Spirit says, "Today if you will hear his voice,
Kwa hiyo, kama Roho Mtakatifu asemavyo: “Leo, kama mkiisikia sauti yake,
8 do not harden your hearts, as in the provocation, like as in the day of the trial in the wilderness,
msiifanye mioyo yenu migumu, kama mlivyofanya katika uasi, wakati ule wa kujaribiwa jangwani,
9 where your fathers tested me and challenged me, and saw my works for forty years.
ambapo baba zenu walinijaribu na kunipima ingawa kwa miaka arobaini walikuwa wameyaona matendo yangu.
10 Therefore I was displeased with this generation, and said, 'They always err in their heart, but they did not know my ways;'
Hiyo ndiyo sababu nilikasirikia kizazi kile, nami nikasema, ‘Siku zote mioyo yao imepotoka, nao hawajazijua njia zangu.’
11 as I swore in my wrath, 'They will not enter into my rest.'"
Hivyo nikatangaza kwa kiapo katika hasira yangu, ‘Kamwe hawataingia rahani mwangu.’”
12 Beware, brothers, lest perhaps there be in any one of you an evil heart of unbelief, in falling away from the living God;
Ndugu zangu, angalieni, asiwepo miongoni mwenu mtu mwenye moyo mwovu usioamini, unaojitenga na Mungu aliye hai.
13 but exhort one another day by day, so long as it is called "today;" lest any one of you be hardened by the deceitfulness of sin.
Lakini mtiane moyo mtu na mwenzake kila siku, maadamu iitwapo Leo, ili asiwepo hata mmoja wenu mwenye kufanywa mgumu kwa udanganyifu wa dhambi.
14 For we have become partakers of Christ, if we hold fast the beginning of our confidence firm to the end:
Kwa kuwa tumekuwa washiriki wa Kristo, kama tukishikamana tu kwa uthabiti na tumaini letu la kwanza hadi mwisho.
15 while it is said, "Today if you will hear his voice, do not harden your hearts, as in the rebellion."
Kama ilivyonenwa: “Leo, kama mkiisikia sauti yake, msiifanye mioyo yenu migumu kama mlivyofanya wakati wa kuasi.”
16 For who, when they heard, rebelled? No, did not all those who came out of Egypt by Moses?
Basi ni nani waliosikia lakini bado wakaasi? Je, si wale wote waliotoka Misri wakiongozwa na Mose?
17 With whom was he displeased forty years? Was not it with those who sinned, whose bodies fell in the wilderness?
Lakini ni nani aliowakasirikia miaka arobaini? Je, si wale waliofanya dhambi ambao miili yao ilianguka jangwani?
18 To whom did he swear that they would not enter into his rest, but to those who were disobedient?
Ni nani hao ambao Mungu aliapa kuwa kamwe hawataingia rahani mwake isipokuwa ni wale waliokataa kutii?
19 We see that they were not able to enter in because of unbelief.
Hivyo tunaona kwamba hawakuweza kuingia kwa sababu ya kutokuamini kwao.