< Daniel 8 >

1 In the third year of the reign of king Belshazzar a vision appeared to me, Daniel, after that which appeared to me previously.
Katika mwaka wa tatu wa utawala wa Mfalme Belshaza, mimi Danieli, nilipata maono, baada ya maono ambayo yalikuwa yamenitokea mbeleni.
2 And I saw in the vision, and when I looked, I was in the citadel of Shushan, which is in the province of Elam. And I saw in the vision, and I was by the river Ulai.
Katika maono yangu, nilijiona nikiwa ndani ya ngome ya Shushani katika jimbo la Elamu. Katika maono nilikuwa kando ya Mto Ulai.
3 Then I lifted up my eyes, and saw, and look, there stood before the river a ram which had two horns. And the two horns were long, but one was longer than the other, and the longer one came up last.
Nikatazama juu, na hapo mbele yangu kulikuwa na kondoo dume mwenye pembe mbili, akiwa amesimama kando ya mto, nazo pembe zake zilikuwa ndefu. Pembe moja ilikuwa ndefu kuliko hiyo nyingine, lakini iliendelea kukua baadaye.
4 I saw the ram pushing westward, and northward, and southward; and no animals could stand before him, neither was there any who could deliver out of his hand. But he did according to his will, and became great.
Nikamtazama yule kondoo dume alivyokuwa akishambulia kuelekea magharibi, kaskazini na kusini. Hakuna mnyama yeyote aliyeweza kusimama dhidi yake, wala hakuna aliyeweza kuokoa kutoka nguvu zake. Alifanya kama atakavyo, naye akawa mkuu.
5 As I was considering, look, a male goat came from the west over the surface of the whole earth, and did not touch the ground. And the goat had a prominent horn between his eyes.
Nilipokuwa ninatafakari hili, ghafula beberu mwenye pembe moja kubwa sana katikati ya macho yake alikuja kutoka magharibi, akiruka kasi juu ya dunia yote bila kugusa ardhi.
6 He came to the ram that had the two horns, which I saw standing before the river, and rushed at him in the fury of his power.
Alikuja akimwelekea yule kondoo dume mwenye pembe mbili niliyemwona akisimama kando ya mto, akamshambulia kwa hasira nyingi.
7 I saw him come close to the ram, and he was moved with anger against him, and struck the ram, and broke his two horns. And there was no power in the ram to stand before him, but he threw him down to the ground and trampled on him, and there was no one who could deliver the ram from his power.
Nikamwona akimshambulia yule kondoo dume kwa hasira nyingi, akimpiga yule kondoo dume na kuvunja pembe zake mbili. Yule kondoo dume hakuwa na nguvu za kumzuia yule beberu, hivyo akamwangusha yule kondoo dume chini na kumkanyaga, wala hakuna aliyeweza kumwokoa yule kondoo dume kutoka nguvu za huyo beberu.
8 The male goat became very strong. But when he was strong, the large horn was broken; and instead of it there came up four prominent horns toward the four winds of heaven.
Yule beberu akawa mkubwa sana, lakini katika kilele cha nguvu zake ile pembe yake ndefu ilivunjika, na mahali pake pakaota pembe nne kubwa kuelekea pande nne za dunia.
9 Out of one of them came forth a little horn, which grew exceeding great, toward the south, and toward the east, and toward the beautiful land.
Kutoka mojawapo ya zile pembe nne palitokea pembe ndogo ukaongezeka nguvu kuelekea kusini, na kuelekea mashariki, na kuelekea Nchi ya Kupendeza.
10 It grew so great that it reached to the host of heaven, and some of the host and of the stars it cast down to the ground, and trampled on them.
Pembe hiyo ikaendelea kukua hadi kufikia jeshi la mbinguni, nayo ikalitupa baadhi ya jeshi la vitu vya angani hapa chini duniani, na kulikanyaga.
11 And it magnified itself, even against the Prince of the host; and it took away from him the daily sacrifice, and the place of his sanctuary was thrown down.
Pembe hiyo ikajikweza ili iwe kama Mkuu wa hilo jeshi; ikamwondolea dhabihu ya kila siku, napo mahali pake patakatifu pakashushwa chini.
12 The host was given over to it together with the daily sacrifice because of transgression. And it cast down truth to the ground, and kept prospering.
Kwa sababu ya uasi, jeshi la watakatifu na dhabihu za kila siku vikatiwa mikononi mwake. Ikafanikiwa katika kila kitu ilichofanya, nayo kweli ikatupwa chini.
13 Then I heard a holy one speaking; and another holy one said to that certain one who spoke, "How long shall be the vision concerning the daily sacrifice, and the transgression that makes desolate, to give both the sanctuary and the host to be trampled?"
Kisha nikamsikia mtakatifu mmoja akizungumza na mtakatifu mwingine, akamwambia, “Je, itachukua muda gani maono haya yatimie: maono kuhusu dhabihu ya kila siku, uasi unaosababisha ukiwa, kutwaliwa kwa mahali patakatifu, na jeshi litakalokanyagwa chini ya nyayo?”
14 He said to me, "To two thousand and three hundred evenings and mornings; then shall the sanctuary be restored to its rightful state."
Akaniambia, “Itachukua siku 2,300. Ndipo mahali patakatifu patawekwa wakfu tena.”
15 It came about when I, Daniel, had seen the vision, that I sought to understand it. And look, there stood before me someone who appeared to be a man.
Mimi Danieli nilipokuwa ninaangalia maono na kujaribu kuelewa, mbele yangu alisimama mmoja aliyefanana na mwanadamu.
16 I heard a man's voice between the banks of the Ulai, and called out and said, "Gabriel, make this man understand the vision."
Kisha nikasikia sauti ya mwanadamu kutoka Mto Ulai ikiita, “Gabrieli, mwambie mtu huyu maana ya maono haya.”
17 So he came near where I stood, and when he came I was frightened, and fell prostrate. But he said to me, "Understand, son of man, that the vision belongs to the time of the end."
Alipokuwa akikaribia pale nilipokuwa nimesimama, niliogopa, nikaanguka kifudifudi. Akaniambia, “Mwana wa mwanadamu, fahamu kuwa maono haya yanahusu siku za mwisho.”
18 Now as he was speaking with me, I fell into a deep sleep with my face toward the ground; but he touched me, and stood me upright.
Alipokuwa akinena nami, nilikuwa katika usingizi mzito, huku nimelala kifudifudi. Ndipo aliponigusa na kunisimamisha wima.
19 He said, "Look, I will make you know what shall be in the latter time of wrath, for it belongs to the appointed time of the end.
Akaniambia, “Nitakuambia yale yatakayotokea baadaye wakati wa ghadhabu, kwa sababu maono haya yanahusu wakati wa mwisho ulioamriwa.
20 The ram which you saw, that had the two horns, they are the kings of Media and Persia.
Kondoo dume mwenye pembe mbili ambaye ulimwona anawakilisha wafalme wa Umedi na Uajemi.
21 The male goat is the king of Greece, and the large horn that is between his eyes is the first king.
Yule beberu mwenye nywele nyingi ni mfalme wa Uyunani, nayo ile pembe ndefu katikati ya macho yake ni mfalme wa kwanza.
22 As for that which was broken, in the place where four stood up, four kingdoms shall arise out of his nation, but not with his power.
Zile pembe nne zilizoota badala ya ile pembe iliyovunjika zinawakilisha falme nne ambazo zitatokea kutoka taifa lake, lakini hakuna hata mmoja utakaokuwa na nguvu kama ule uliovunjika.
23 In the latter time of their kingdom, when the transgressions have reached their full measure, a rash and deceitful king shall arise.
“Katika sehemu ya mwisho ya utawala wao, wakati waasi watakapokuwa waovu kabisa, atainuka mfalme mwenye uso mkali, aliye stadi wa hila.
24 His power shall be great, but not by his own strength; and he shall cause terrible destruction, and shall succeed in whatever he does. And he shall destroy the mighty and the holy people.
Atakuwa na nguvu nyingi, lakini si kwa uwezo wake mwenyewe. Atasababisha uharibifu wa kutisha, na atafanikiwa kwa chochote anachofanya. Atawaangamiza watu maarufu na watu watakatifu.
25 Through his cunning he shall cause deceit to prosper by his influence, and he shall be great in his own mind, and without warning he shall destroy many. He shall also stand up against the Prince of princes; but he shall be shattered, but not by human hands.
Atasababisha udanganyifu ustawi, naye atajihesabu mwenyewe kuwa bora. Wakati wajisikiapo kuwa wako salama, atawaangamiza wengi, na kushindana na Mkuu wa wakuu. Lakini ataangamizwa, isipokuwa si kwa uwezo wa mwanadamu.
26 The vision of the evenings and mornings which has been told is true; but seal up the vision because it refers to many days from now."
“Maono kuhusu jioni na asubuhi ambayo umepewa ni kweli, lakini yatie muhuri maono haya, kwa maana yanahusu wakati mrefu ujao.”
27 I, Daniel, was overcome, and was ill for days. Then I rose up, and carried out the king's business. And I was astonished by the vision, but there was no one to explain it.
Mimi Danieli nilikuwa nimechoka sana, na nikalala nikiwa mgonjwa kwa siku kadhaa. Ndipo nikaamka, nikaenda kwenye shughuli za mfalme. Nilifadhaishwa na maono hayo, nami sikuweza kuyaelewa.

< Daniel 8 >