< 2 Samuel 8 >

1 After this it happened that David struck the Philistines, and subdued them, and David took the bridle of Ammah out of the hand of the Philistines.
ikawa baada ya haya Daudi aliwashambulia Wafilisti na kuwashinda. Hivyo Daudi akaichukua Gathi na vijiji vyake kutoka katika mamlaka ya wafilisti.
2 He struck Moab, and measured them with the line, making them to lie down on the ground; and he measured two lines to put to death, and one full line to keep alive. The Moabites became servants to David, and brought tribute.
Kisha akaishinda Moabu na akawapima watu wake kwa mstari kwa kuwafanya walale chini juu ya ardhi. Alipima mistari miwili ya kuua, na mstari mmoja kamili kuwahifadhi hai. Hivyo Wamoabu wakawa watumishi wa Daudi na wakaanza kumlipa kodi.
3 David struck also Hadadezer the son of Rehob, king of Zobah, as he went to recover his dominion at the River.
Kisha Daudi akamshinda Hadadezeri mwana wa Rehobu, mfalme wa Soba, Hadadezeri aliposafiri kuurudisha ufalme wake katika mto Frati.
4 And David took from him a thousand of his chariots, and seven thousand horsemen, and twenty thousand footmen: and David hamstrung all the chariot horses, but reserved of them for one hundred chariots.
Daudi aliteka magari 1, 700 ya farasi na askari ishirini elfu waendao kwa miguu. Daudi akawakata miguu farasi wa magari, lakini akahifadhi wakutosha magari mia moja.
5 When the Arameans of Damascus came to help Hadadezer king of Zobah, David struck of the Arameans two and twenty thousand men.
Wakati Washami wa Dameski walipokuja kumsaidia Hadadeziri mfalme wa Soba, Daudi akaua katika Washami watu ishirini na mbili elfu.
6 Then David put garrisons in Aram of Damascus; and the Arameans became servants to David, and brought tribute. YHWH gave victory to David wherever he went.
Daudi akaweka ngome huko Shamu ya Dameski, na Washami wakawa watumishi wake na wakaleta kodi. Yahwe akampa Daudi ushindi kila alikokwenda.
7 And David took the shields of gold that were on the servants of Hadadezer, and brought them to Jerusalem, which, later on, were also taken by Shishak king of Egypt in the days of Rehoboam son of Solomon when he went up to Jerusalem.
Daudi akachukua ngao za dhahabu walizokuwa nazo watumishi wa Hadadezeri naye akazileta Yerusalemu.
8 From Tebah and from Berothai, cities of Hadadezer, king David took a very great amount of bronze.
Mfalme Daudi akachukua shaba nyingi kutoka Beta na Berosai, miji ya Hadadezeri.
9 When Toi king of Hamath heard that David had struck all the army of Hadadezer,
Wakati Tou, mfalme wa Hamathi, aliposikia kwamba Daudi amelishinda jeshi lote la Hadadezeri,
10 then Toi sent Hadoram his son to king David, to greet him, and to bless him, because he had fought against Hadadezer and struck him: for Hadadezer had wars with Toi. And he brought with him vessels of silver, and vessels of gold, and vessels of bronze.
Tou akamtuma Hadoramu mwanawe kwa mfalme Daudi kumpa salamu na kumbariki, kwa kuwa Daudi alikuwa amepigana na Hadadezeri na kumshinda, maana Hadadezeri alikuwa amepiga vita dhidi ya Tou. Hadoramu akaja pamoja na vitu vya fedha, dhahabu, na shaba.
11 The King also dedicated these to YHWH, with the silver and gold that he dedicated of all the nations which he subdued;
Mfalme Daudi akaviweka wakfu vitu hivi kwa ajili ya Yahwe, pamoja na fedha na dhahabu kutoka katika mataifa yote aliyokuwa ameyashinda-
12 of Edom, and of Moab, and of the people of Ammon, and of the Philistines, and of Amalek, and of the spoil of Hadadezer, son of Rehob, king of Zobah.
kutoka Shamu, Moabu, Waamoni, Wafilist, Waamaleki, pamoja na nyara zote alizoziteka kutoka kwa Hadadezeri mwana wa Rehobu, mfalme wa Soba.
13 And David made a name for himself when he returned from defeating the Arameans. And Abishai son of Zeruiah defeated the Edomites in the Valley of Salt--eighteen thousand.
Jina la Daudi likajulikana sana alipowashinda washami katika bonde la Chumvi, pamoja na watu wao wapatao elfu kumi na nane.
14 And he put a garrison in Edom, and all the Edomites became servants to David. YHWH gave victory to David wherever he went.
Akaweka ngome katika Edomu yote, na Waedomu wote wakawa watumishi wake. Yahwe akampa Daudi ushindi kila alipokwenda.
15 And David reigned over Israel, exercising justice and righteousness for all his people.
Daudi akatawala juu ya Israeli yote, naye akatenda kwa haki na usawa kwa watu wote.
16 And Joab the son of Zeruiah was in charge of the army; and Jehoshaphat the son of Ahilud was recorder;
Yoabu mwana wa Seruya alikuwa mkuu wa jeshi, na Yehoshafati mwana wa Ahiludi alikuwa mwenye kuandika taarifa.
17 and Zadok the son of Ahitub, and Abiathar the son of Ahimelech, were priests; and Shisha was scribe;
Sadoki mwana wa Ahitubu na Ahimeleki mwana wa Abiathari walikuwa makuhani, na Seraya alikuwa mwandishi.
18 and Benaiah the son of Jehoiada supervised the Cherethites and the Pelethites; and David's sons were chief ministers.
Benaya mwana wa Yehoyada alikuwa juu ya Wakerethi na Wapelethi, na wana wa Daudi walikuwa washauri wa mfalme.

< 2 Samuel 8 >