< 2 Chronicles 10 >

1 Rehoboam went to Shechem; for all Israel had come to Shechem to make him king.
Rehoboamu akaenda Shekemu, kwa kuwa Waisraeli wote walikuwa wamekwenda huko kumfanya yeye kuwa mfalme.
2 It happened, when Jeroboam the son of Nebat heard of it, (for he was in Egypt, where he had fled from the presence of king Solomon), that Jeroboam returned out of Egypt.
Yeroboamu mwana wa Nebati aliposikia hili (alikuwa bado yuko Misri alikokuwa amekimbilia awe mbali na Mfalme Solomoni), akarudi kutoka Misri.
3 They sent and called him; and Jeroboam and all Israel came, and they spoke to Rehoboam, saying,
Kwa hiyo wakatuma watu kumwita Yeroboamu, yeye na kusanyiko lote la Israeli wakamwendea Rehoboamu na kumwambia,
4 "Your father made our yoke grievous: now therefore make you the grievous service of your father, and his heavy yoke which he put on us, lighter, and we will serve you."
“Baba yako aliweka nira nzito, lakini sasa tupunguzie kazi za kikatili na nira nzito aliyoweka juu yetu, nasi tutakutumikia.”
5 He said to them, "Come again to me after three days." The people departed.
Rehoboamu akajibu, “Nendeni kwa muda wa siku tatu na kisha mnirudie.” Basi watu wakaenda zao.
6 King Rehoboam took counsel with the old men, who had stood before Solomon his father while he yet lived, saying, "What counsel do you give me to return answer to this people?"
Kisha Mfalme Rehoboamu akataka shauri kwa wazee ambao walimtumikia Solomoni baba yake wakati wa uhai wake akawauliza, “Mnanishauri nini katika kuwajibu watu hawa?”
7 They spoke to him, saying, "If you are kind to this people, and please them, and speak good words to them, then they will be your servants forever."
Wakajibu, “Kama leo utakuwa mtumishi wa watu hawa na kuwahudumia na kuwapa jibu linaloridhisha, watakuwa watumishi wako daima.”
8 But he forsook the counsel of the old men which they had given him, and took counsel with the young men who had grown up with him, who stood before him.
Lakini Rehoboamu akakataa shauri alilopewa na wazee na akataka ushauri kwa vijana wanaume rika lake waliokuwa wakimtumikia.
9 He said to them, "What counsel do you give, that we may return answer to this people, who have spoken to me, saying, 'Make the yoke that your father put on us lighter?'"
Akawauliza, “Ninyi ushauri wenu ni nini? Tutawajibuje watu hawa wanaoniambia, ‘Ifanye nyepesi nira baba yako aliyoweka juu yetu?’”
10 The young men who had grown up with him spoke to him, saying, "Thus you shall tell the people who spoke to you, saying, 'Your father made our yoke heavy, but make it lighter on us;' thus you shall say to them, 'My little finger is thicker than my father's waist.
Wale vijana wa rika lake wakamjibu, “Waambie watu hawa waliokuambia, ‘Baba yako aliweka nira nzito juu yetu, lakini ifanye nira yetu nyepesi,’ kuwa, ‘Kidole changu kidogo ni kinene kuliko kiuno cha baba yangu.
11 Now whereas my father burdened you with a heavy yoke, I will add to your yoke. My father chastised you with whips, but I will chastise you with scorpions.'"
Baba yangu aliweka nira nzito juu yenu, mimi nitaifanya hata iwe nzito zaidi. Baba yangu aliwachapa kwa mijeledi; mimi nitawachapa kwa nge.’”
12 So Jeroboam and all the people came to Rehoboam the third day, as the king asked, saying, "Come to me again the third day."
Siku tatu baadaye, Yeroboamu na watu wote wakamrudia Rehoboamu, kama mfalme alivyokuwa amesema, “Rudini kwangu baada ya siku tatu.”
13 The king answered them roughly; and king Rehoboam forsook the counsel of the old men,
Mfalme akawajibu watu kwa ukatili. Akikataa shauri alilopewa na wazee,
14 and spoke to them after the counsel of the young men, saying, "My father made your yoke heavy, but I will add to it. My father chastised you with whips, but I will chastise you with scorpions."
akafuata shauri la vijana wa rika lake na kusema, “Baba yangu alifanya nira yenu kuwa nzito, mimi nitaifanya kuwa nzito zaidi. Baba yangu aliwachapa kwa mijeledi, mimi nitawachapa kwa nge.”
15 So the king did not listen to the people; for it was brought about of God, that YHWH might establish his word, which he spoke by Ahijah the Shilonite to Jeroboam the son of Nebat.
Kwa hiyo mfalme hakuwasikiliza watu, kwa kuwa jambo hili lilitoka kwa Mungu ili kutimiza neno ambalo Bwana alikuwa amenena kwa Yeroboamu mwana wa Nebati kupitia Ahiya Mshiloni.
16 When all Israel saw that the king did not listen to them, the people answered the king, saying, "What portion have we in David? Neither have we inheritance in the son of Jesse. Every man to your tents, Israel. Now see to your own house, David." So all Israel departed to their tents.
Israeli wote walipoona kuwa mfalme amekataa kuwasikiliza, wakamjibu mfalme: “Tuna fungu gani kwa Daudi? Sisi hatuna urithi kwa mwana wa Yese. Nendeni kwenye mahema yenu, ee Israeli, angalia nyumba yako mwenyewe, ee Daudi!” Hivyo Waisraeli wakaenda kwenye mahema yao.
17 But as for the children of Israel who lived in the cities of Judah, Rehoboam reigned over them.
Lakini kwa habari ya Waisraeli waliokuwa wakiishi katika miji ya Yuda, Rehoboamu akaendelea kuwatawala bado.
18 Then king Rehoboam sent Hadoram, who was over the men subject to forced labor; and the children of Israel stoned him to death with stones. King Rehoboam made speed to get himself up to his chariot, to flee to Jerusalem.
Mfalme Rehoboamu akamtuma Adoniramu aliyekuwa msimamizi wa wale waliofanya kazi ngumu kwa kulazimishwa, lakini Israeli wote wakampiga kwa mawe hadi akafa. Hata hivyo, Mfalme Rehoboamu, akafanikiwa kuingia kwenye gari lake na kutorokea Yerusalemu.
19 So Israel rebelled against the house of David to this day.
Hivyo Israeli wakaasi dhidi ya nyumba ya Daudi hadi leo.

< 2 Chronicles 10 >