< Titus 2 >

1 But say the things which fit sound doctrine,
Lakini wewe unapaswa kuhubiri mafundisho safi.
2 that older men should be sober-minded, worthy of respect, self-controlled, sound in faith, in love, and in patience:
Waambie wazee kwamba wanapaswa kuwa na kiasi, wawe na busara na wataratibu; wanapaswa kuwa timamu katika imani yao, upendo na uvumilivu.
3 and that older women likewise be reverent in behavior, not slanderers nor enslaved to much wine, teachers of that which is good;
Hali kadhalika waambie wanawake wazee wawe na mwenendo wa uchaji wa Mungu; wasiwe wachongezi, au watumwa wa pombe. Wanapaswa kufundisha mambo mema,
4 that they may train the young women to love their husbands, to love their children,
ili wawazoeze kina mama vijana kuwapenda waume zao na watoto,
5 to be self-controlled, pure, working at home, kind, and being subject to their own husbands, so that God's word may not be discredited.
wawe na kiasi na safi, waangalie vizuri mambo ya nyumbani, na wawatii waume zao, ili ujumbe wa Mungu usije ukadharauliwa.
6 Likewise, exhort the younger men to be self-controlled;
Kadhalika, wahimize vijana wawe na kiasi.
7 in all things showing yourself an example of good works. In your teaching show integrity, seriousness,
Katika mambo yote wewe mwenyewe unapaswa kuwa mfano wa matendo mema. Uwe mnyofu na uwe na uzito katika mafundisho yako.
8 and a sound message that cannot be condemned; that he who opposes you may be ashamed, having no evil thing to say about us.
Maneno yako yasiwe na hitilafu yoyote ili adui zako waaibike wasipopata chochote kibaya cha kusema juu yetu.
9 Exhort servants to be in subjection to their own masters, and to be well-pleasing in all things; not contradicting;
Watumwa wanapaswa kuwatii wakuu wao na kuwapendeza katika mambo yote. Wasibishane nao,
10 not stealing, but showing all good fidelity; that they may adorn the doctrine of God, our Savior, in all things.
au kuiba vitu vyao. Badala yake wanapaswa kuonyesha kwamba wao ni wema na waaminifu daima, ili, kwa matendo yao yote, wayapatie sifa njema mafundisho juu ya Mungu, Mwokozi wetu.
11 For the grace of God has appeared, bringing salvation to all people,
Maana neema ya Mungu imedhihirishwa kwa ajili ya wokovu wa watu wote.
12 instructing us to say "No" to ungodliness and worldly desires, and to live soberly, righteously, and godly in this present age; (aiōn g165)
Neema hiyo yatufunza kuachana na uovu wote na tamaa za kidunia; tuwe na kiasi, tuishi maisha adili na ya kumcha Mungu katika ulimwengu huu wa sasa, (aiōn g165)
13 looking for the blessed hope and appearing of the glory of our great God and Savior, Jesus Christ;
tukiwa tunangojea siku ile ya heri tunayoitumainia, wakati utakapotokea utukufu wa Mungu Mkuu na Mwokozi wetu Yesu Kristo.
14 who gave himself for us, that he might redeem us from all iniquity, and purify for himself a people for his own possession, zealous for good works.
Yeye alijitoa mwenyewe kwa ajili yetu ili atukomboe kutoka katika uovu wote na kutufanya watu safi walio wake yeye mwenyewe, watu walio na hamu ya kutenda mema.
15 Say these things and exhort and reprove with all authority. Let no one despise you.
Basi, fundisha mambo hayo na tumia mamlaka yako yote ukiwahimiza na kuwaonya wasikilizaji wako. Mtu yeyote na asikudharau.

< Titus 2 >