< Zechariah 7 >

1 It happened in the fourth year of king Daryavesh that the word of the LORD came to Zechariah in the fourth day of the ninth month, the month of Chislev.
Katika mwaka wa nne wa utawala wa Mfalme Dario, neno la Bwana lilimjia Zekaria siku ya nne ya mwezi wa tisa, mwezi wa Kisleu.
2 The people of Bethel sent Sharezer and Regem Melech, and their men, to entreat the LORD's favor,
Watu wa Betheli walikuwa wamemtuma Shareza na Regem-Meleki pamoja na watu wao, kumsihi Bwana
3 and to speak to the cohanim of the house of the LORD of hosts, and to the prophets, saying, "Should I weep in the fifth month, separating myself, as I have done these so many years?"
kwa kuwauliza makuhani wa nyumba ya Bwana Mwenye Nguvu Zote na manabii, “Je, imempasa kuomboleza na kufunga katika mwezi wa tano, kama ambavyo nimekuwa nikifanya kwa miaka mingi?”
4 Then the word of the LORD of hosts came to me, saying,
Kisha neno la Bwana Mwenye Nguvu Zote likanijia kusema:
5 "Speak to all the people of the land, and to the cohanim, saying, 'When you fasted and mourned in the fifth and in the seventh month for these seventy years, did you at all fast to me, really to me?
“Waulize watu wote wa nchi na makuhani, ‘Je, mlipofunga na kuomboleza katika mwezi wa tano na wa saba kwa miaka sabini iliyopita, mlifunga kweli kwa ajili yangu?
6 When you eat, and when you drink, do you not eat for yourselves, and drink for yourselves?
Na mlipokuwa mkila na kunywa, je, hamkuwa mnasherehekea kwa ajili ya nafsi zenu?
7 Aren't these the words which the LORD proclaimed by the former prophets, when Jerusalem was inhabited and in prosperity, and its cities around her, and the Negev and the lowland were inhabited?'"
Je, haya sio maneno ya Bwana aliyosema kupitia manabii waliotangulia, wakati Yerusalemu pamoja na miji inayoizunguka ilipokuwa katika hali ya utulivu na ya mafanikio, wakati Negebu na Shefala zikiwa zimekaliwa na watu?’”
8 The word of the LORD came to Zechariah, saying,
Neno la Bwana likamjia tena Zekaria:
9 "Thus has the LORD of hosts spoken, saying, 'Execute true judgment, and show kindness and compassion every man to his brother.
“Hivi ndivyo asemavyo Bwana Mwenye Nguvu Zote: ‘Fanyeni hukumu za haki, onyesheni rehema na huruma ninyi kwa ninyi.
10 Do not oppress the widow, nor the fatherless, the foreigner, nor the poor; and let none of you devise evil against his brother in your heart.'
Msimwonee mjane wala yatima, mgeni wala maskini. Msiwaziane mabaya mioyoni mwenu ninyi kwa ninyi.’
11 But they refused to listen, and turned their backs, and stopped their ears, that they might not hear.
“Lakini wakakataa kusikiliza, wakanipa kisogo kwa ukaidi na kuziba masikio yao.
12 Yes, they made their hearts as hard as flint, lest they might hear the law, and the words which the LORD of hosts had sent by his Ruach by the former prophets. Therefore great wrath came from the LORD of hosts.
Wakaifanya mioyo yao migumu kama jiwe gumu na hawakuisikiliza sheria au maneno ambayo Bwana Mwenye Nguvu Zote aliyatuma kwa njia ya Roho wake kupitia manabii waliotangulia. Kwa hiyo Bwana Mwenye Nguvu Zote alikasirika sana.
13 It has come to pass that, as he called, and they refused to listen, so they will call, and I will not listen," said the LORD of hosts;
“‘Wakati nilipoita, hawakusikiliza, kwa hiyo walipoita, sikusikiliza,’ asema Bwana Mwenye Nguvu Zote.
14 "but I will scatter them with a whirlwind among all the nations which they have not known. Thus the land was desolate after them, so that no man passed through nor returned: for they made the pleasant land desolate."
‘Niliwatawanya kwa upepo wa kisulisuli miongoni mwa mataifa yote, mahali ambapo walikuwa wageni. Nchi ikaachwa ukiwa nyuma yao kiasi kwamba hakuna aliyeweza kuingia au kutoka. Hivi ndivyo walivyoifanya ile nchi iliyokuwa imependeza kuwa ukiwa.’”

< Zechariah 7 >