< Mark 5 >

1 And they came to the other side of the lake, into the territory of the Gerasenes.
Basi, wakafika katika nchi ya Wagerase, ng'ambo ya ziwa.
2 And when he had come out of the boat, immediately a man with an unclean spirit met him out of the tombs.
Mara tu Yesu aliposhuka mashuani, mtu mmoja aliyepagawa na pepo mchafu alitoka makaburini, akakutana naye.
3 He lived in the tombs, and no one could bind him any more, not even with a chain.
Mtu huyo alikuwa akiishi makaburini wala hakuna mtu aliyeweza tena kumfunga kwa minyororo.
4 For he had been often bound with fetters and chains, and the chains had been torn apart by him, and the fetters broken in pieces. No one had the strength to tame him.
Mara nyingi walimfunga kwa pingu na minyororo lakini kila mara aliweza kuikata hiyo minyororo na kuzivunja hizo pingu, wala hakuna mtu aliyeweza kumzuia.
5 And always, night and day, in the tombs and in the mountains, he was crying out, and cutting himself with stones.
Mchana na usiku alikaa makaburini na milimani akipaaza sauti na kujikatakata kwa mawe.
6 And when he saw Yeshua from afar, he ran and bowed down to him,
Alipomwona Yesu kwa mbali, alimkimbilia, akamwinamia
7 and crying out with a loud voice, he said, "What have I to do with you, Yeshua, you Son of the Most High God? I adjure you by God, do not torment me."
akisema kwa sauti kubwa, “Una shauri gani nami, wewe Yesu Mwana wa Mungu aliye juu? Kwa jina la Mungu, nakusihi usinitese!”
8 For he had been saying to him, "Come out of the man, you unclean spirit."
(Alisema hivyo kwa kuwa Yesu alikuwa amemwambia, “Pepo mchafu, mtoke mtu huyu.”)
9 And then he asked him, "What is your name?" And he replied, "My name is Legion, for we are many."
Basi, Yesu akamwuliza, “Jina lako nani?” Naye akajibu, “Jina langu ni Jeshi, maana sisi tu wengi.”
10 And he pleaded with Yeshua repeatedly not to send them away out of the region.
Kisha akamsihi Yesu asiwafukuze hao pepo katika nchi ile.
11 Now on the mountainside there was a great herd of pigs feeding.
Kulikuwa na kundi kubwa la nguruwe malishoni kwenye mteremko wa mlima.
12 And they begged him, saying, "Send us into the pigs, that we may enter into them."
Basi, hao pepo wakamsihi, “Utupeleke kwa hao nguruwe, tuwaingie.”
13 And he gave them permission. The unclean spirits came out and entered into the pigs; and the herd of about two thousand rushed down the steep bank into the lake, and they were drowned in the lake.
Naye akawaruhusu. Basi, hao pepo wachafu wakatoka, wakawaingia wale nguruwe. Kundi lote la nguruwe wapatao elfu mbili likaporomoka kwenye ule mteremko mkali mpaka ziwani, likatumbukia majini.
14 And those who fed them fled, and told it in the city and in the country. And the people went to see what it was that had happened.
Wachungaji wa hao nguruwe walikimbia, wakatangaza jambo hilo mjini na mashambani. Watu wakafika kuona yaliyotukia.
15 And they came to Yeshua, and saw him who had been possessed by demons sitting, clothed and in his right mind, even him who had the legion; and they were afraid.
Wakamwendea Yesu, wakamwona na mtu yuleyule aliyekuwa amepagawa na jeshi la pepo ameketi chini, amevaa nguo na ana akili yake sawa, wakaogopa.
16 And those who saw it declared to them how it happened to him who was possessed by demons, and about the pigs.
Watu walishuhudia tukio hilo wakaeleza wengine mambo yaliyompata huyo mtu aliyekuwa amepagawa na pepo na juu ya wale nguruwe.
17 And then they began to plead with Yeshua to leave their region.
Basi, wakaanza kumwomba aondoke katika nchi yao.
18 As he was entering into the boat, he who had been possessed by demons pleaded with him that he might be with him.
Yesu alipokuwa anapanda mashuani, yule mtu aliyekuwa amepagawa na pepo akamwomba amruhusu kwenda naye.
19 However, Yeshua did not allow him, but said to him, "Go to your house, to your own, and tell them what great things the Lord has done for you, and how he had mercy on you."
Lakini Yesu akamkatalia. Badala yake akamwambia, “Nenda nyumbani kwa jamaa yako, ukawaambie mambo yote Bwana aliyokutendea na jinsi alivyokuonea huruma.”
20 So he went his way, and began to proclaim in Decapolis how Yeshua had done great things for him, and everyone was amazed.
Basi, huyo mtu akaenda, akaanza kutangaza huko Dekapoli mambo yote Yesu aliyomtendea; watu wote wakashangaa.
21 And when Yeshua had crossed back over in the boat to the other side, a large crowd was gathered to him; and he was by the lake.
Yesu alivukia tena upande wa pili wa ziwa kwa mashua. Umati mkubwa wa watu ukakusanyika mbele yake, naye akawa amesimama kando ya ziwa.
22 One of the rulers of the synagogue, Jairus by name, came; and seeing him, he fell at his feet,
Hapo akaja mmojawapo wa maofisa wa sunagogi, jina lake Yairo. Alipomwona Yesu, akajitupa mbele ya miguu yake,
23 and pleaded with him repeatedly, saying, "My little daughter is at the point of death. Please come and lay your hands on her, that she may be made healthy, and live."
akamsihi akisema, “Binti yangu mdogo ni mgonjwa karibu kufa. Twende tafadhali, ukamwekee mikono yako, apate kupona na kuishi.”
24 And he went with him, and a large crowd followed him, and they pressed upon him on all sides.
Basi, Yesu akaondoka pamoja naye. Watu wengi sana wakamfuata, wakawa wanamsonga kila upande.
25 Now a woman, who had an issue of blood for twelve years,
Mmojawapo alikuwa mwanamke mwenye ugonjwa wa kutokwa damu kwa muda wa miaka kumi na miwili.
26 and had suffered many things by many physicians, and had spent all that she had, and was no better, but rather grew worse,
Mwanamke huyo alikuwa amekwisha sumbuka sana kuwaendea waganga wengi. Na ingawa alikuwa amekwisha tumia mali yake yote, hakupata nafuu bali hali yake ilizidi kuwa mbaya.
27 having heard the things concerning Yeshua, came up behind him in the crowd, and touched his clothes.
Alikuwa amesikia habari za Yesu, na hivyo akaupenya msongamano wa watu kutoka nyuma, akagusa vazi lake.
28 For she said, "If I just touch his clothes, I will be made well."
Alifanya hivyo, maana alijisemea, “Nikigusa tu vazi lake, nitapona.”
29 And immediately the flow of her blood was dried up, and she felt in her body that she was healed of her affliction.
Mara chemchemi ya damu yake ikakauka, akajisikia mwilini mwake kwamba ameponywa ugonjwa wake.
30 And immediately Yeshua, perceiving in himself that the power had gone out from him, turned around in the crowd, and asked, "Who touched my clothes?"
Yesu alitambua mara kwamba nguvu imemtoka. Basi akaugeukia ule umati wa watu, akauliza, “Nani aliyegusa mavazi yangu?”
31 And his disciples said to him, "You see the crowd pressing against you, and you say, 'Who touched me?'"
Wanafunzi wake wakamjibu, “Unaona jinsi watu wanavyokusonga; mbona wauliza nani aliyekugusa?”
32 He looked around to see her who had done this thing.
Lakini Yesu akaendelea kutazama amwone huyo aliyefanya hivyo.
33 But the woman, fearing and trembling, knowing what had been done to her, came and fell down before him, and told him the whole truth.
Hapo huyo mwanamke, akifahamu yaliyompata, akajitokeza akitetemeka kwa hofu, akajitupa chini mbele ya Yesu na kusema ukweli wote.
34 And he said to her, "Daughter, your faith has made you well. Go in peace, and be cured of your disease."
Yesu akamwambia, “Binti, imani yako imekuponya. Nenda kwa amani, upone kabisa ugonjwa wako.”
35 While he was still speaking, people came from the synagogue ruler's house saying, "Your daughter is dead. Why bother the Teacher any more?"
Yesu alipokuwa bado anaongea, watu walifika kutoka nyumbani kwa yule ofisa wa sunagogi, wakamwambia, “Binti yako amekwisha kufa. Ya nini kuendelea kumsumbua Mwalimu?”
36 But Yeshua, overhearing the message spoken, said to the ruler of the synagogue, "Do not be afraid, only believe."
Lakini, bila kujali walichosema, Yesu akamwambia mkuu wa sunagogi, “Usiogope, amini tu.”
37 And he allowed no one to follow him, except Peter, Jacob, and John the brother of Jacob.
Wala hakumruhusu mtu yeyote kufuatana naye ila Petro, Yakobo na Yohane nduguye Yakobo.
38 And they came to the synagogue ruler's house, and he saw an uproar, weeping, and great wailing.
Wakafika nyumbani kwa ofisa wa sunagogi naye Yesu akasikia makelele, kilio na maombolezo mengi.
39 And when he had entered in, he said to them, "Why do you make an uproar and weep? The child is not dead, but is asleep."
Akaingia ndani, akawaambia, “Mbona mnapiga kelele na kulia? Msichana hakufa, amelala tu.”
40 And they ridiculed him. But he, having put them all out, took the father of the child, her mother, and those who were with him, and went in where the child was.
Lakini wao wakamcheka. Basi, akawaondoa wote nje, akawachukua baba na mama ya huyo msichana na wale wanafunzi wake, wakaingia chumbani alimokuwa huyo msichana.
41 And taking the child by the hand, he said to her, "Talitha koum," which translated means, "Little girl, I tell you, get up."
Kisha akamshika mkono, akamwambia, “Talitha, kumi,” maana yake, “Msichana, nakwambia, amka!”
42 And immediately the girl rose up and walked, for she was twelve years old. And immediately they were overcome with amazement.
Mara msichana akasimama, akaanza kutembea. (Alikuwa na umri wa miaka kumi na miwili.) Hapo watu wakashangaa kupita kiasi.
43 And he strictly ordered them that no one should know this, and commanded that something should be given to her to eat.
Yesu akawakataza sana wasimjulishe mtu jambo hilo. Kisha akawaambia wampe huyo msichana chakula.

< Mark 5 >