< Mark 15 >
1 Immediately in the morning the chief cohanim, with the elders and scribes, and the whole council, held a consultation, and bound Yeshua, and carried him away, and delivered him to Pilate.
Kulipopambazuka, makuhani wakuu walifanya shauri pamoja na wazee, walimu wa Sheria na Baraza lote, wakamfunga Yesu pingu, wakampeleka na kumkabidhi kwa Pilato.
2 Pilate asked him, "Are you the King of the Jews?" He answered, "You say so."
Pilato akamwuliza Yesu, “Je, wewe ni mfalme wa Wayahudi?” Yesu akajibu, “Wewe umesema.”
3 The chief cohanim accused him of many things.
Makuhani wakuu wakamshtaki Yesu mambo mengi.
4 Pilate again asked him, "Have you no answer? See how many things they testify against you."
Pilato akamwuliza tena Yesu, “Je, hujibu neno? Tazama wanavyotoa mashtaka mengi juu yako.”
5 But Yeshua made no further answer, and Pilate was amazed.
Lakini Yesu hakujibu neno, hata pilato akashangaa.
6 Now at the feast he used to release to them one prisoner, whom they requested.
Kila wakati wa sikukuu ya Pasaka, Pilato alikuwa na desturi ya kuwafungulia mfungwa mmoja waliyemtaka.
7 There was one called Barabbas, bound with those who had made insurrection, who in the insurrection had committed murder.
Basi, kulikuwa na mtu mmoja aitwaye Baraba, ambaye alikuwa amefungwa pamoja na waasi wengine kwa kusababisha uasi na mauaji.
8 And the crowd went up and began to ask him to do for them according to his custom.
Watu wengi wakamwendea Pilato wakamwomba awafanyie kama kawaida yake.
9 Pilate answered them, saying, "Do you want me to release to you the King of the Jews?"
Pilato akawauliza, “Je, mwataka niwafungulieni Mfalme wa Wayahudi?”
10 For he perceived that for envy the chief cohanim had delivered him up.
Alisema hivyo kwa sababu alijua wazi kwamba makuhani wakuu walimkabidhi Yesu kwake kwa sababu ya wivu.
11 But the chief cohanim stirred up the crowd, that he should release Barabbas to them instead.
Lakini makuhani wakuu wakawachochea watu wamwombe Pilato awafungulie Baraba.
12 Pilate again asked them, "What then should I do to him whom you call the King of the Jews?"
Pilato akawauliza tena, “Basi, sasa mwataka nifanye nini na mtu huyu mnayemwita Mfalme wa Wayahudi?”
13 They shouted again, "Crucify him."
Watu wote wakapaaza sauti tena: “Msulubishe!”
14 Pilate said to them, "Why, what evil has he done?" But they shouted all the louder, "Crucify him."
Lakini Pilato akawauliza, “Kwa nini! Amefanya kosa gani?” Lakini wao wakazidi kupaaza sauti, “Msulubishe!”
15 Pilate, wishing to please the crowd, released Barabbas to them, and handed over Yeshua, when he had flogged him, to be crucified.
Pilato alitaka kuuridhisha huo umati wa watu; basi, akamwachilia Baraba kutoka gerezani. Akaamuru Yesu apigwe viboko, kisha akamtoa asulubiwe.
16 The soldiers led him away within the court, which is the Praetorium; and they called together the whole cohort.
Kisha askari walimpeleka Yesu ndani ukumbini, katika ikulu, wakakusanya kikosi kizima cha askari.
17 They clothed him with purple, and weaving a crown of thorns, they put it on him.
Wakamvika vazi la rangi ya zambarau, wakasokota taji ya miiba, wakamwekea kichwani.
18 They began to salute him, "Greetings, King of the Jews."
Wakaanza kumsalimu, “Shikamoo Mfalme wa Wayahudi!”
19 They struck his head with a reed, and spat on him, and bowing their knees, did homage to him.
Wakampiga kichwani kwa mwanzi, wakamtemea mate; wakampigia magoti na kumsujudia.
20 When they had mocked him, they took the purple off of him, and put his own garments on him. They led him out to crucify him.
Baada ya kumdhihaki, walimvua lile joho, wakamvika nguo zake, kisha wakampeleka kumsulubisha.
21 And they forced one passing by, Shim'on of Cyrene, coming from the country, the father of Alexander and Rufus, to go with them, that he might carry his cross.
Walipokuwa njiani, walikutana na mtu mmoja aitwaye Simoni, mwenyeji wa Kurene. Yeye alikuwa baba wa Aleksanda na Rufo, na wakati huo alikuwa akitoka shambani. Basi, wakamlazimisha auchukue msalaba wa Yesu.
22 And they brought him to the place called Golgotha, which is translated, "The place of a skull."
Kisha wakampeleka Yesu mpaka mahali palipoitwa Golgotha, maana yake, “Mahali pa Fuvu la Kichwa.”
23 They offered him wine mixed with myrrh to drink, but he did not take it.
Wakampa divai iliyochanganywa na manemane, lakini yeye akaikataa.
24 Crucifying him, they parted his garments among them, casting lots on them, what each should take.
Basi, wakamsulubisha, wakagawana mavazi yake kwa kuyapigia kura waamue nani angepata nini.
25 It was nine in the morning, and they crucified him.
Ilikuwa saa tatu asubuhi walipomsulubisha.
26 The superscription of his accusation was written over him, "THE KING OF THE JEWS."
Na mshtaka wake ulikuwa umeandikwa: “Mfalme wa Wayahudi.”
27 With him they crucified two robbers; one on his right hand, and one on his left.
Pamoja naye waliwasulubisha wanyang'anyi wawili, mmoja upande wake wa kulia na mwingine upande wake wa kushoto.
28 And the Scripture was fulfilled which says, "And he was numbered with transgressors."
Hapo yakatimia Maandiko Matakatifu yanayosema, “Aliwekwa kundi moja na waovu.”
29 Those who passed by blasphemed him, wagging their heads, and saying, "Ha. You who destroy the temple, and build it in three days,
Watu waliokuwa wanapita mahali hapo walimtukana, wakitikisa vichwa vyao na kusema, “Aha! Wewe mwenye kuvunja Hekalu na kulijenga kwa siku tatu!
30 save yourself and come down from the cross."
Sasa, shuka msalabani ujiokoe mwenyewe!”
31 Likewise, also the chief cohanim mocking among themselves with the scribes said, "He saved others. He cannot save himself.
Nao makuhani wakuu pamoja na walimu wa Sheria walimdhihaki wakisema, “Aliwaokoa wengine, lakini kujiokoa mwenyewe hawezi!
32 Let the Messiah, the King of Israel, now come down from the cross, that we may see and believe him." Those who were crucified with him insulted him.
Eti yeye ni Kristo, Mfalme wa Israeli! Basi, na ashuke msalabani ili tuone na kuamini.” Hata watu wale waliosulubiwa pamoja naye walimtukana.
33 Now when it was noon, there was darkness over the whole land until three in the afternoon.
Tangu saa sita mchana mpaka saa tisa kulikuwa giza nchini kote.
34 Then at three in the afternoon Yeshua called out with a loud voice, saying, "Elohi, Elohi, lema shabachthani?" which is translated, "My God, my God, why have you forsaken me?"
Saa tisa alasiri Yesu akalia kwa sauti kubwa, “Eloi, Eloi, lema sabakthani?” Maana yake, “Mungu wangu, Mungu wangu, mbona umeniacha?”
35 Some of those who stood by, when they heard it, said, "Look, he is calling for Elijah."
Baadhi ya watu waliosimama pale waliposikia hivyo, walisema, “Sikiliza! Anamwita Eliya!”
36 One ran, and filling a sponge full of vinegar, put it on a reed, and gave it to him to drink, saying, "Let him be. Let us see whether Elijah comes to take him down."
Mtu mmoja akakimbia, akachovya sifongo katika siki, akaiweka juu ya mwanzi, akampa anywe akisema, “Hebu tuone kama Eliya atakuja kumteremsha msalabani!”
37 Yeshua gave a loud cry, and gave up the spirit.
Yesu akapaaza sauti kubwa, akakata roho.
38 The veil of the temple was torn in two from the top to the bottom.
Basi, pazia la Hekalu likapasuka vipande viwili toka juu mpaka chini.
39 And when the centurion, who stood by opposite him, saw that he cried out like this and breathed his last, he said, "Truly this man was the Son of God."
Jemadari mmoja aliyekuwa amesimama mbele yake aliona jinsi Yesu alivyolia kwa sauti na kukata roho, akasema, “Kweli mtu huyu alikuwa Mwana wa Mungu!”
40 There were also women watching from afar, among whom were both Miriam from Magdala, and Miriam the mother of Jacob the younger and of Josi, and Salome;
Walikuwako pia wanawake waliotazama kwa mbali, miongoni mwao akiwa Maria toka mji wa Magdala, Salome, na Maria mama wa kina Yakobo mdogo na Yose.
41 who, when he was in Galil, followed him, and served him; and many other women who came up with him to Jerusalem.
Hawa walimfuata Yesu alipokuwa Galilaya na kumtumikia. Kulikuwa na wanawake wengine wengi waliokuja Yerusalemu pamoja naye.
42 When evening had now come, because it was the Preparation Day, that is, the day before the Sabbath,
Wakati wa jioni ulikuwa umekwisha fika. Hiyo ilikuwa siku ya Maandalio, yaani siku inayotangulia Sabato.
43 Joseph of Arimateh, a prominent council member who also himself was looking for the Kingdom of God, came. He boldly went in to Pilate, and asked for the body of Yeshua.
Hapo akaja Yosefu mwenyeji wa Armathaya, mjumbe wa Baraza Kuu, aliyeheshimika sana. Yeye pia alikuwa anatazamia kuja kwa Ufalme wa Mungu. Basi, alimwendea Pilato bila uoga, akaomba apewe mwili wa Yesu.
44 Pilate was surprised that he was already dead; and summoning the centurion, he asked him whether he had been dead long.
Pilato alishangaa kusikia kwamba Yesu alikuwa amekwisha kufa. Basi, akamwita jemadari, akamwuliza kama Yesu alikuwa amekufa kitambo.
45 When he found out from the centurion, he granted the body to Joseph.
Pilato alipoarifiwa na huyo jemadari kwamba Yesu alikuwa amekwisha kufa, akamruhusu Yosefu auchukue mwili wake.
46 He bought a linen cloth, and taking him down, wound him in the linen cloth, and placed him in a tomb which had been cut out of a rock. He rolled a stone against the door of the tomb.
Hapo Yosefu akanunua sanda ya kitani, akauteremsha chini huo mwili, akauzungushia sanda. Akauweka katika kaburi lililokuwa limechongwa mwambani, kisha akavingirisha jiwe kubwa mbele ya mlango.
47 Miriam from Magdala and Miriam, the mother of Josi, saw where he was placed.
Nao Maria Magdalene na Maria mama yake Yose walipaona hapo alipolazwa.