< Yochanan 20 >
1 Now on the first day of the week, Miriam from Magdala went early, while it was still dark, to the tomb, and saw the stone taken away from the tomb.
Alfajiri na mapema Jumapili, kukiwa bado na giza, Maria Magdalene alikwenda kaburini, akaliona lile jiwe limeondolewa mlangoni pa kaburi.
2 Therefore she ran and came to Shim'on Peter, and to the other talmid whom Yeshua loved, and said to them, "They have taken away the Lord out of the tomb, and we do not know where they have put him."
Basi, akaenda mbio hadi kwa Petro na yule mwanafunzi mwingine ambaye Yesu alimpenda, akawaambia, “Wamemwondoa Bwana kaburini, na wala hatujui walikomweka.”
3 Therefore Peter and the other talmid went out, and they went toward the tomb.
Petro pamoja na yule mwanafunzi mwingine wakaenda kaburini.
4 They both ran together. The other talmid outran Peter, and came to the tomb first.
Wote wawili walikimbia lakini yule mwanafunzi mwingine alikimbia mbio zaidi kuliko Petro, akatangulia kufika kaburini.
5 Stooping and looking in, he saw the linen cloths lying, yet he did not enter in.
Alipoinama na kuchungulia ndani, aliona sanda, lakini hakuingia ndani.
6 Then Shim'on Peter came, following him, and entered into the tomb. He saw the linen cloths lying,
Simoni Petro naye akaja akimfuata, akaingia kaburini; humo akaona sanda,
7 and the cloth that had been on his head, not lying with the linen cloths, but rolled up in a place by itself.
na kile kitambaa alichofungwa Yesu kichwani. Hicho kitambaa hakikuwekwa pamoja na hiyo sanda, bali kilikuwa kimekunjwa na kuwekwa mahali peke yake.
8 So then the other talmid who came first to the tomb also entered in, and he saw and believed.
Kisha yule mwanafunzi mwingine aliyemtangulia kufika kaburini, akaingia pia ndani, akaona, akaaamini.
9 For as yet they did not know the Scripture, that he must rise from the dead.
(Walikuwa bado hawajaelewa Maandiko Matakatifu yaliyosema kwamba ilikuwa lazima afufuke kutoka wafu).
10 So the talmidim went away again to their own homes.
Basi, hao wanafunzi wakarudi nyumbani.
11 But Miriam was standing outside at the tomb weeping. So, as she wept, she stooped and looked into the tomb,
Maria alikuwa amesimama nje ya kaburi, akilia. Huku akiwa bado analia, aliinama na kuchungulia kaburini,
12 and she saw two angels in white sitting, one at the head, and one at the feet, where the body of Yeshua had lain.
akawaona malaika wawili waliovaa mavazi meupe, wameketi pale mwili wa Yesu ulipokuwa umelazwa, mmoja kichwani na wa pili miguuni.
13 They told her, "Woman, why are you weeping?" She said to them, "Because they have taken away my Lord, and I do not know where they have put him."
Hao malaika wakamwuliza, “Mama, kwa nini unalia?” Naye akawaambia, “Wamemwondoa Bwana wangu, na wala sijui walikomweka!”
14 When she had said this, she turned around and saw Yeshua standing, and did not know that it was Yeshua.
Baada ya kusema hayo, aligeuka nyuma, akamwona Yesu amesimama hapo, lakini asitambue ya kuwa ni Yesu.
15 Yeshua said to her, "Woman, why are you weeping? Who are you looking for?" She, supposing him to be the gardener, said to him, "Sir, if you have carried him away, tell me where you have put him, and I will take him away."
Yesu akamwuliza, “Mama, kwa nini unalia? Unamtafuta nani?” Maria, akidhani kwamba huyo ni mtunza bustani, akamwambia, “Mheshimiwa, kama ni wewe umemwondoa, niambie ulikomweka, nami nitamchukua.”
16 Yeshua said to her, "Miriam." She turned and said to him in Hebrew, "Rabboni." which is to say, "Teacher."
Yesu akamwambia, “Maria!” Naye Maria akageuka, akamwambia kwa Kiebrania, “Raboni” (yaani “Mwalimu”).
17 Yeshua said to her, "Do not touch me, for I have not yet ascended to the Father; but go to my brothers, and tell them, 'I am ascending to my Father and your Father, to my God and your God.'"
Yesu akamwambia, “Usinishike; sijakwenda bado juu kwa Baba. Lakini nenda kwa ndugu zangu uwaambie: nakwenda juu kwa Baba yangu na Baba yenu, Mungu wangu na Mungu wenu.”
18 Miriam from Magdala came and told the talmidim, "I have seen the lord," and that he had said these things to her.
Hivyo Maria Magdalene akaenda akawapa habari wale wanafunzi kuwa amemwona Bwana, na kwamba alikuwa amemwambia hivyo.
19 When therefore it was evening, on that day, the first day of the week, and when the doors were locked where the talmidim were, for fear of the Jewish leaders, Yeshua came and stood in the midst, and said to them, "Peace be to you."
Ilikuwa jioni ya siku hiyo ya Jumapili. Wanafunzi walikuwa wamekutana pamoja ndani ya nyumba, na milango ilikuwa imefungwa kwa sababu waliwaogopa viongozi wa Wayahudi. Basi, Yesu akaja, akasimama kati yao, akawaambia, “Amani kwenu!”
20 When he had said this, he showed them his hands and his side. The talmidim therefore were glad when they saw the Lord.
Alipokwisha sema hayo, akawaonyesha mikono yake na ubavu wake. Basi, hao wanafunzi wakafurahi mno kumwona Bwana.
21 Yeshua therefore said to them again, "Peace be to you. As the Father has sent me, even so I send you."
Yesu akawaambia tena, “Amani kwenu! Kama vile Baba alivyonituma mimi, nami nawatuma ninyi.”
22 When he had said this, he breathed on them, and said to them, "Receive the Ruach ha-Kodesh.
Alipokwisha sema hayo, akawapulizia na kuwaambia, “Pokeeni Roho Mtakatifu.
23 Whoever's sins you forgive, they are forgiven them. Whoever's sins you retain, they have been retained."
Mkiwasamehe watu dhambi zao, wamesamehewa; msipowaondolea, hawasamehewi.”
24 But Thomas, one of the twelve, called Didymus, was not with them when Yeshua came.
Thoma mmoja wa wale kumi na wawili (aitwaye Pacha), hakuwa pamoja nao wakati Yesu alipokuja.
25 The other talmidim therefore said to him, "We have seen the Lord." But he said to them, "Unless I see in his hands the mark of the nails, and put my finger into the mark of the nails, and put my hand into his side, I will not believe."
Basi, wale wanafunzi wengine wakamwambia, “Tumemwona Bwana.” Thoma akawaambia, “Nisipoona mikononi mwake alama za misumari, na kutia kidole changu katika kovu hizo, na kutia mkono wangu ubavuni mwake, sitasadiki.”
26 After eight days again his talmidim were inside, and Thomas was with them. Yeshua came, the doors being locked, and stood in the midst, and said, "Peace be to you."
Basi, baada ya siku nane hao wanafunzi walikuwa tena pamoja mle ndani, na Thoma alikuwa pamoja nao. Milango ilikuwa imefungwa, lakini Yesu akaja, akasimama kati yao, akasema, “Amani kwenu!”
27 Then he said to Thomas, "Put your finger here, and observe my hands. Reach out your hand, and put it into my side; and do not be unbelieving, but believing."
Kisha akamwambia Thoma, “Lete kidole chako hapa uitazame mikono yangu; lete mkono wako ukautie ubavuni mwangu. Usiwe na mashaka, ila amini!”
28 Thomas answered and said to him, "My Lord and my God."
Thoma akamjibu, “Bwana wangu na Mungu wangu!”
29 Yeshua said to him, "Because you have seen me, you have believed. Blessed are those who have not seen, and have believed."
Yesu akamwambia, “Je, unaamini kwa kuwa umeniona? Heri yao wale ambao hawajaona, lakini wameamini.”
30 Therefore Yeshua did many other signs in the presence of his talmidim, which are not written in this book;
Yesu alifanya mbele ya wanafunzi wake ishara nyingine nyingi ambazo hazikuandikwa katika kitabu hiki.
31 but these are written, that you may believe that Yeshua is the Messiah, the Son of God, and that believing you may have life in his name.
Lakini hizi zimeandikwa ili mpate kuamini kwamba Yesu ni Kristo, Mwana wa Mungu; na kwa kuamini mpate kuwa na uzima kwa nguvu ya jina lake.