< Psalms 44 >

1 [For the Chief Musician. By the sons of Korah. A contemplative psalm.] We have heard with our ears, God; our fathers have told us, what work you did in their days, in the days of old.
Mungu, tumesikia kwa masikio yetu, baba zetu wametuambia kazi uliyofanya katika siku zao, siku za kale.
2 You drove out the nations with your hand, but you planted them. You afflicted the peoples, but you spread them abroad.
Uliwafukuza mataifa kwa mkono wako, lakini ukawafanya watu wetu kuishi humo; wewe uliwataabisha mataifa, lakini ukawaeneza watu wetu katika nchi.
3 For they did not get the land in possession by their own sword, neither did their own arm save them; but your right hand, and your arm, and the light of your face, because you were favorable to them.
Kwa maana hawakupata umiliki wa nchi kwa upanga wao, wala mkono wao wenyewe haukuwaokoa; bali mkono wako wakuume, mkono wako, na nuru ya uso wako, na kwa sababu uliwaridhia.
4 You are my King, my God, who commands victories for Jacob.
Mungu, wewe ni Mfalme wangu, amuru ushindi kwa ajili ya Yakobo.
5 Through you we will push back our adversaries. Through your name we will trample down those who rise up against us.
Kwa uweza wako tutawaangusha chini maadui zetu; kwa jina lako tutatembea juu yao, wale wanao inuka dhidi yetu.
6 For I will not trust in my bow, neither shall my sword save me.
Kwa maana sitauamini upinde wangu, wala upanga wangu hautaniokoa.
7 But you have saved us from our adversaries, and have shamed those who hate us.
Bali wewe ndeye uliyetuokoa na adui zetu, na umewaaibisha wale watuchukiao.
8 In God we have made our boast all day long, we will give thanks to your name forever. (Selah)
Katika Mungu tumefanywa kujivuna siku zote, nasi tutalishukuru jina lako milele. (Selah)
9 But now you rejected us, and brought us to dishonor, and do not go out with our armies.
Lakini sasa umetutupa na kutufedhehesha, na hauendi na majeshi yetu.
10 You make us turn back from the adversary. Those who hate us take spoil for themselves.
Umetufanya kuwakimbia maadui zetu; na wale watuchukiao huchukua vitu vyetu vya thamani kwa ajili yao wenyewe.
11 You have made us like sheep for food, and have scattered us among the nations.
Umetufanya kama kondoo aliyeandaliwa kwa ajili ya chakula na umetutawanya kati ya mataifa.
12 You sell your people for nothing, and have gained nothing from their sale.
Wewe unawauza watu wako bure; kwa kufanya hivyo haukupata faida.
13 You make us the taunt of our neighbors, a scoffing and a derision to those who are around us.
Wewe umetufanya kukemewa na majirani zetu, kuchekwa, na kudhihakiwa na wale wanao tuzunguka.
14 You make us a byword among the nations, a shaking of the head among the peoples.
Umetufaya kituko kati ya mataifa, .......................................................
15 All day long my dishonor is before me, and shame covers my face,
Siku zote fedheha yangu iko mbele yangu, na aibu ya uso wangu imenifunika
16 At the taunt of one who reproaches and verbally abuses, because of the enemy and the avenger.
kwa sababu ya sauti yake iliyo kemea na kutukana, kwa sababu ya adui na kisasi.
17 All this has come on us, yet have we not forgotten you, Neither have we been false to your covenant.
Yote haya yametupata sisi; bado hatukukusahau wewe wala kulikosea agano lako.
18 Our heart has not turned back, neither have our steps strayed from your path,
Mioyo yetu haikukengeuka; hatua zetu hazikuiacha njia yako.
19 Though you have crushed us in the haunt of jackals, and covered us with the shadow of death.
Bali wewe umetuadhibu vikali katika mahali pa mbweha na kutufunika na uvuli wa mauti.
20 If we have forgotten the name of our God, or spread forth our hands to a strange god;
Ikiwa tumelisahau jina la Mungu wetu au kueneza mikono yetu kwa Mungu mgeni,
21 won't God search this out? For he knows the secrets of the heart.
Mungu asingeligundua hili? Kwa maana yeye anazijua siri za moyo.
22 For your sake we are killed all day long. We are regarded as sheep to be slaughtered.
Hakika, kwa ajili ya jina lako tutauawa siku zote; tunahesabiwa kuwa kondoo kwa ajili ya kuchinjwa.
23 Wake up. Why do you sleep, LORD? Arise. Do not reject us forever.
Bwana, amka, kwa nini unalala? Inuka, usitutupe moja kwa moja.
24 Why do you hide your face, and forget our affliction and our oppression?
Kwa nini unaficha uso wako na kusahau mateso yetu na kukandamizwa kwetu?
25 For our soul is bowed down to the dust. Our body cleaves to the earth.
Kwa maana tumeyeyushwa kwenye mavumbi; miili yetu imeshikamana na ardhi.
26 Rise up to help us. Redeem us for your loving kindness' sake.
Inuka utusaidie na utuokoe kwa ajili ya uaminifu wa agano lako.

< Psalms 44 >