< Proverbs 13 >

1 A wise son listens to his father's instruction, but a scoffer doesn't listen to rebuke.
Mwana mwenye hekima husikia mafundisho ya baba yake, bali mwenye dhihaka hatasikiliza karipio.
2 By the fruit of his lips, a man enjoys good things; but the unfaithful crave violence.
Mtu hufurahia vitu vizuri kutokana na matunda ya kinywa chake, bali hamu ya wadanganyifu ni jeuri.
3 He who guards his mouth guards his soul. One who opens wide his lips comes to ruin.
Yeye anayelinda kinywa chake huyalinda maisha, bali anayefumbua sana midomo yake atajiangamiza mwenyewe.
4 The soul of the sluggard desires, and has nothing, but the desire of the diligent shall be fully satisfied.
Hamu ya watu wavivu ni uchu lakini hawapati kitu, bali hamu ya watu wenye bidii hutoshelezwa sana.
5 A righteous man hates lies, but a wicked man brings shame and disgrace.
Atendaye haki huchukia uongo, bali mtu mwovu hukinzana mwenyewe, na kufanya ya kuaibisha.
6 Righteousness guards the way of integrity, but wickedness overthrows the sinner.
Wenye haki huwalinda wale ambao ni wakamilifu katika mapito yao, bali uovu huwaangusha wale watendao dhambi.
7 There are some who pretend to be rich, yet have nothing. There are some who pretend to be poor, yet have great wealth.
Kuna mtu ambaye hujitajirisha mwenyewe, lakini hana chochote na kuna mtu ambaye hutoa kila kitu, bado ni tajiri kweli.
8 The ransom of a man's life is his riches, but the poor hear no threats.
Mtu tajiri anaweza kufidia maisha yake kwa mali zake, bali mtu masikini hatapokea kitisho cha aina hiyo.
9 The light of the righteous shines brightly, but the lamp of the wicked is snuffed out.
Mwanga wa mtu atendaye haki hufurahia, bali taa ya waovu itazimika.
10 Pride only breeds quarrels, but with ones who take advice is wisdom.
Kiburi huzaa mafarakano, bali kwa wale wasikiao shauri jema kuna hekima.
11 Wealth gained dishonestly dwindles away, but he who gathers by hand makes it grow.
Penye majivuno mengi utajiri hufifia, bali yeye apataye pesa kwa kufanya kazi kwa mkono wake pesa zake zitaongezeka.
12 Hope deferred makes the heart sick, but when longing is fulfilled, it is a tree of life.
Tumaini linapoachwa, huvunja moyo, bali kukamilishwa kwa shauku ni mti wa uzima.
13 Whoever despises instruction will pay for it, but he who respects a command will be rewarded.
Yule ambaye anadharau fundisho bado atakuwa chini ya utawala wake, bali yeye ambaye anaheshimu amri atapewa thawabu.
14 The teaching of the wise is a spring of life, to turn from the snares of death.
Mafundisho ya mtu mwenye hekima ni chemchemi ya uzima, yanakuondoa kutoka kwenye mitego ya mauti.
15 Good understanding brings favor; but the way of the unfaithful leads to calamity.
Busara njema huleta fadhila, bali njia ya wadanganyifu haina mwisho.
16 Every prudent man acts from knowledge, but a fool exposes folly.
Watu wenye busara hutenda kwa maarifa kwa kila uamuzi, bali mpumbavu huonyesha upuuzi wake.
17 A wicked messenger falls into trouble, but a trustworthy envoy gains healing.
Mjumbe mbaya huangukia kwenye shida, bali balozi mwaminifu huleta upatanisho.
18 Poverty and shame come to him who refuses discipline, but he who heeds correction shall be honored.
Yeye ambaye hupuuza kurudiwa atapata umasikini na aibu, bali heshima itamjia yeye ambaye hujifunza kutokana na masahihisho.
19 Longing fulfilled is sweet to the soul, but fools detest turning from evil.
Shauku iliyotambuliwa ni tamu kwa hamu, bali wapumbavu huchukia kuacha uovu.
20 One who walks with wise men grows wise, but a companion of fools suffers harm.
Tembea pamoja na watu wenye hekima nawe utakuwa na hekima, bali rafiki wa wapumbavu atateseka.
21 Misfortune pursues sinners, but prosperity rewards the righteous.
Maafa huwakimbilia wenye dhambi, bali wale watendao haki hupewa thawabu kwa mema.
22 A good man leaves an inheritance to his children's children, but the wealth of the sinner is stored for the righteous.
Mtu mwema huacha urithi kwa wajukuu wake, bali mali ya mwenye dhambi huwekwa akiba kwa yule atendaye haki.
23 An abundance of food is in poor people's fields, but injustice sweeps it away.
Shamba la masikini lisilolimwa linaweza huzalisha chakula kingi, bali huchukuliwa kwa udhalimu.
24 One who spares the rod hates his son, but one who loves him is careful to discipline him.
Yeye ambaye hamrudi mwanawe humchukia, bali yule anayempenda mwanawe humjali kwa kumwadibisha.
25 The righteous one eats to the satisfying of his soul, but the belly of the wicked goes hungry.
Yeye atendaye haki hula hadi kutosheleza hamu yake bali tumbo la mwovu linanjaa daima.

< Proverbs 13 >