< Matthew 23 >
1 Then Jesus spoke to the crowds and to his disciples,
Kisha Yesu akauambia umati wa watu pamoja na wanafunzi wake:
2 saying, "Upon the seat of Moses the Pharisees and scribes sit.
“Walimu wa sheria na Mafarisayo wameketi katika kiti cha Mose,
3 All which they will say unto you, observe and do; but their works do not do, because they say, and do not do.
hivyo inawapasa kuwatii na kufanya kila kitu wanachowaambia. Lakini msifuate yale wanayotenda, kwa sababu hawatendi yale wanayohubiri.
4 For they bind heavy and hard to bear burdens, and lay them on men's shoulders; but they themselves will not lift a finger to help them.
Wao hufunga mizigo mikubwa na kuiweka mabegani mwa watu, lakini wao wenyewe hawako radhi hata kuinua kidole ili kuisogeza.
5 But all their works they do to be seen by others. They make their tefillin broad and enlarge the fringe of their garments,
“Wao hutenda mambo yao yote ili waonekane na watu. Hupanua vikasha vyao vyenye maandiko ya sheria na kurefusha matamvua ya mavazi yao.
6 and love the place of honor at feasts, the best seats in the synagogues,
Wanapenda kukalia viti vya heshima katika karamu, na vile viti maalum sana katika masinagogi.
7 the grteetings in the marketplaces, and to be called 'Rabbi' by people.
Hupenda kusalimiwa masokoni na kutaka watu wawaite ‘Rabi.’
8 But you are not to be called 'Rabbi,' for one is your Teacher, and all of you are brothers.
“Lakini ninyi msiitwe ‘Rabi,’ kwa sababu mnaye Bwana mmoja na ninyi nyote ni ndugu.
9 Call no man on the earth your father, for one is your Father, he who is in heaven.
Nanyi msimwite mtu yeyote ‘Baba,’ hapa duniani, kwa maana mnaye Baba mmoja, naye yuko mbinguni.
10 Neither be called masters, for one is your master, the Messiah.
Wala msiitwe ‘Mwalimu,’ kwa maana mnaye mwalimu mmoja tu, ndiye Kristo.
11 But he who is greatest among you will be your servant.
Yeye aliye mkuu kuliko ninyi nyote miongoni mwenu atakuwa mtumishi wenu.
12 Whoever exalts himself will be humbled, and whoever humbles himself will be exalted.
Kwa kuwa yeyote anayejikweza atashushwa, na yeyote anayejinyenyekeza atakwezwa.
13 "But woe to you, scribes and Pharisees, hypocrites. For you devour the houses of widows, and for show make long prayers. Therefore you will receive greater condemnation.
“Lakini ole wenu, walimu wa sheria na Mafarisayo, enyi wanafiki! Kwa maana mnawafungia watu milango ya Ufalme wa Mbinguni. Ninyi wenyewe hamuingii humo, nao wale wanaotaka kuingia mnawazuia. [
14 "Woe to you, scribes and Pharisees, hypocrites. For you shut up the kingdom of heaven in front of people; for you do not enter in yourselves, neither do you allow those who are entering in to enter.
Ole wenu walimu wa sheria na Mafarisayo, enyi wanafiki! Mnakula katika nyumba za wajane, nanyi kwa kujifanya kuwa wema, mnasali sala ndefu. Kwa hiyo hukumu yenu itakuwa kuu zaidi.]
15 "Woe to you, scribes and Pharisees, hypocrites. For you travel around by sea and land to make one proselyte; and when he becomes one, you make him twice as much of a son of hell as yourselves. (Geenna )
“Ole wenu walimu wa sheria na Mafarisayo, enyi wanafiki! Ninyi mnasafiri baharini na nchi kavu ili kumfanya mtu mmoja mwongofu, lakini baada ya kumpata, mnamfanya mwana wa jehanamu mara mbili kuliko ninyi! (Geenna )
16 "Woe to you, you blind guides, who say, 'Whoever swears by the temple, it is nothing; but whoever swears by the gold of the temple, he is obligated.'
“Ole wenu, viongozi vipofu! Ninyi mwasema, ‘Mtu akiapa kwa Hekalu, kiapo hicho si kitu; lakini mtu akiapa kwa dhahabu ya Hekalu, amefungwa kwa kiapo chake.’
17 You blind fools. For which is greater, the gold, or the temple that sanctified the gold?
Ninyi vipofu wapumbavu! Ni kipi kilicho kikuu zaidi: ni ile dhahabu, au ni lile Hekalu linaloifanya hiyo dhahabu kuwa takatifu?
18 'Whoever swears by the altar, it is nothing; but whoever swears by the gift that is on it, he is obligated?'
Pia mnasema, ‘Mtu akiapa kwa madhabahu, si kitu; lakini mtu akiapa kwa sadaka iliyo juu ya madhabahu, amefungwa kwa kiapo chake’
19 You blind people. For which is greater, the gift, or the altar that sanctifies the gift?
Ninyi vipofu! Ni kipi kikuu zaidi: ni sadaka, au ni madhabahu yanayoifanya hiyo sadaka kuwa takatifu?
20 He therefore who swears by the altar, swears by it, and by everything on it.
Kwa hiyo, mtu aapaye kwa madhabahu, huapa kwa hayo madhabahu na vitu vyote vilivyo juu yake.
21 He who swears by the temple, swears by it, and by him who dwells in it.
Naye mtu aapaye kwa Hekalu, huapa kwa hilo Hekalu na kwa huyo akaaye ndani yake.
22 He who swears by heaven, swears by the throne of God, and by him who sits on it.
Naye aapaye kwa mbingu, huapa kwa kiti cha enzi cha Mungu na kwa yeye aketiye juu ya kiti hicho.
23 "Woe to you, scribes and Pharisees, hypocrites. For you tithe mint, dill, and cumin, and have left undone the weightier matters of the Law: justice, mercy, and faith. But you ought to have done these, and not to have left the other undone.
“Ole wenu walimu wa sheria na Mafarisayo, ninyi wanafiki! Kwa maana mnatoa zaka ya mnanaa, bizari na jira, lakini mmeacha mambo makuu zaidi ya sheria, yaani haki, huruma na uaminifu. Iliwapasa kufanya haya makuu ya sheria bila kupuuza hayo matoleo.
24 You blind guides, who strain out a gnat, and swallow a camel.
Ninyi viongozi vipofu, mnachuja kiroboto lakini mnameza ngamia!
25 "Woe to you, scribes and Pharisees, hypocrites. For you clean the outside of the cup and the plate, but within they are full of extortion and self-indulgence.
“Ole wenu, walimu wa sheria na Mafarisayo, ninyi wanafiki! Kwa maana mnasafisha kikombe na sahani kwa nje, lakini ndani mmejaa unyangʼanyi na kutokuwa na kiasi.
26 You blind Pharisee, first clean the inside of the cup and the plate, so that the outside may become clean also.
Ewe Farisayo kipofu! Safisha ndani ya kikombe na sahani kwanza, ndipo nje itakuwa safi pia.
27 "Woe to you, scribes and Pharisees, hypocrites. For you are like whitened tombs, which outwardly appear beautiful, but inwardly are full of dead people's bones, and of all uncleanness.
“Ole wenu, walimu wa sheria na Mafarisayo, ninyi wanafiki! Mnafanana na makaburi yaliyopakwa chokaa, ambayo yanapendeza kwa nje, lakini ndani yamejaa mifupa ya wafu na kila aina ya uchafu.
28 Even so you also outwardly appear righteous to people, but inwardly you are full of hypocrisy and iniquity.
Vivyo hivyo, kwa nje ninyi mnaonekana kwa watu kuwa wenye haki, lakini kwa ndani mmejaa unafiki na uovu.
29 "Woe to you, scribes and Pharisees, hypocrites. For you build the tombs of the prophets, and decorate the tombs of the righteous,
“Ole wenu, walimu wa sheria na Mafarisayo, ninyi wanafiki! Mnajenga makaburi ya manabii na kuyapamba makaburi ya wenye haki.
30 and say, 'If we had lived in the days of our fathers, we would not have been partakers with them in the blood of the prophets.'
Nanyi mwasema, ‘Kama tungaliishi wakati wa baba zetu, tusingalikuwa tumeshiriki katika kumwaga damu ya manabii!’
31 Therefore you testify to yourselves that you are children of those who killed the prophets.
Hivyo mnajishuhudia wenyewe kwamba ninyi ni wana wa wale waliowaua manabii.
32 Fill up, then, the measure of your fathers.
Haya basi, kijazeni kipimo cha dhambi ya baba zenu!
33 You serpents, you offspring of vipers, how will you escape the judgment of hell? (Geenna )
“Ninyi nyoka, ninyi uzao wa nyoka wenye sumu! Mtaiepukaje hukumu ya jehanamu? (Geenna )
34 Therefore, look, I send to you prophets, wise people, and scribes. Some of them you will kill and crucify; and some of them you will scourge in your synagogues, and persecute from city to city;
Kwa sababu hii, tazameni, natuma kwenu manabii na wenye hekima na walimu. Baadhi yao mtawaua na kuwasulubisha, na wengine wao mtawapiga mijeledi katika masinagogi yenu na kuwafuatia kutoka mji mmoja hadi mji mwingine.
35 that on you may come all the righteous blood shed on the earth, from the blood of righteous Abel to the blood of Zechariah son of Berechiah, whom you killed between the sanctuary and the altar.
Hivyo ile damu ya wenye haki wote iliyomwagwa hapa duniani, tangu damu ya Abeli, ambaye alikuwa hana hatia, hadi damu ya Zekaria mwana wa Barakia, mliyemuua kati ya patakatifu na madhabahu, itawajia juu yenu.
36 Truly I tell you, all these things will come upon this generation.
Amin, nawaambia, haya yote yatakuja juu ya kizazi hiki.
37 "Jerusalem, Jerusalem, who kills the prophets, and stones those who are sent to her. How often I would have gathered your children together, even as a hen gathers her chicks under her wings, and you would not.
“Ee Yerusalemu, Yerusalemu, uwauaye manabii na kuwapiga mawe wale waliotumwa kwako! Mara ngapi nimetamani kuwakusanya watoto wako pamoja, kama vile kuku akusanyavyo vifaranga wake chini ya mabawa yake, lakini hukutaka!
38 Look, your house is abandoned to you.
Tazama nyumba yenu imeachwa ukiwa.
39 For I tell you, you will not see me from now on, until you say, 'Blessed is he who comes in the name of the Lord.'"
Kwa maana nawaambia, hamtaniona tena tangu sasa mpaka mtakaposema, ‘Amebarikiwa yeye ajaye kwa Jina la Bwana.’”