< Yochanan 19 >

1 So Pilate then took Jesus, and flogged him.
Basi Pilato alimchukua Yesu na kumchapa.
2 The soldiers twisted thorns into a crown, and put it on his head, and dressed him in a purple garment.
Wale maaskari wakasokota miiba na kutengeneza taji. Wakaiweka juu ya kichwa cha Yesu na kumvalisha vazi la rangi ya zambarau.
3 And they kept coming up to him and saying, "Greetings, King of the Jews." and they struck him with their hands.
Wakamjia na kusema, “Wewe mfalme wa Wayahudi! na kisha kumpiga kwa mikono yao.
4 Then Pilate went out again, and said to them, "Look, I am bringing him out to you, that you may know that I find no basis for a charge against him."
Kisha Pilato alitoka nje na kuwaambia watu, “Tazama nawaleteeni huyu mtu kwenu ili mjue kwamba mimi sikuona hatia yoyote ndani yake.”
5 Then Jesus came out, wearing the crown of thorns and the purple garment. And he said to them, "Look, here is the man."
Kwa hiyo Yesu akatoka nje; alikuwa amevaa taji ya miiba na vazi la zambarau. Ndipo Pilato akawaambia, “Tazameni mtu huyu hapa!”
6 When therefore the chief priests and the officers saw him, they shouted, saying, "Crucify. Crucify." Pilate said to them, "Take him yourselves, and crucify him, for I find no basis for a charge against him."
Kwa hiyo wakati kuhani mkuu na wakuu walipomwona Yesu, wakapiga kelele wakisema, “Msulubishe, msulubishe.” Pilato akawaambia, “Mchukueni ninyi wenyewe mkamsulubishe, kwa kuwa mimi sioni hatia ndani yake.”
7 The Jewish leaders answered him, "We have a law, and by that law he ought to die, because he made himself the Son of God."
Wayahudi wakamjibu Pilato, “Sisi tunayo sheria, na kwa sheria hiyo inampasa kufa kwa sababu yeye alijifanya kuwa mwana wa Mungu.”
8 When therefore Pilate heard this saying, he was more afraid.
Pilato aliposikia maneno haya alizidi kuogopa,
9 He entered into the Praetorium again, and said to Jesus, "Where are you from?" But Jesus gave him no answer.
akaingia Praitorio tena na kumwambia Yesu, “Wewe unatoka wapi? Hata hivyo, Yesu hakumjibu.
10 Pilate therefore said to him, "Are you not speaking to me? Do you not know that I have power to release you, and have power to crucify you?"
Kisha Pilato akamwambia, “Je, wewe huongei na mimi? Je, wewe hujui kuwa mimi nina mamlaka ya kukufungua na mamlakaya kukusulubisha?”
11 Jesus answered, "You would have no power at all against me, unless it were given to you from above. Therefore he who delivered me to you has greater sin."
Yesu akamjibu, “Usingekuwa na nguvu dhidi yangu kama usingepewa toka juu. Kwa hiyo, mtu aliyenitoa kwako ana dhambi kubwa.”
12 At this, Pilate was seeking to release him, but the Jewish leaders shouted, saying, "If you release this man, you are not Caesar's friend. Everyone who makes himself a king speaks against Caesar."
Kutokana na jibu hili, Pilato akataka kumwacha huru, lakini Wayahudi wakapiga kelele wakisema, “Kama utamwacha huru basi wewe si rafiki wa Kaisari: Kila ajifanyaye kuwa mfalme hunena kinyume cah kaisari.”
13 When Pilate therefore heard these words, he brought Jesus out, and sat down on the judgment seat at a place called "The Pavement," but in Hebrew, "Gabbatha."
Pilato alipoyasikia maneno haya, akamleta Yesu nje kisha akakaa kwenye kiti cha hukumu mahali pale panapojulikana kama sakafu, lakini kwa Kiebrania, Gabatha.
14 Now it was the Preparation Day of the Passover, at about noon. He said to the Jewish leaders, "Look, here is your King."
Siku ya maandalizi ya pasaka ilipofika, panapo muda wa saa ya sita. Pilato akawaambia Wayahudi, “Tazameni mfalme wenu huyu hapa!”
15 They shouted, "Away with him. Away with him. Crucify him." Pilate said to them, "Should I crucify your King?" The chief priests answered, "We have no king but Caesar."
Wakapiga kelele, “Mwondoshe, mwondoshe, msulubishe!” Pilato akawaambia, “Je, nimsulubishe mfalme wenu?” Naye Kuhani mkuu akajibu, “Sisi hatuna mfalme isipokuwa Kaisari.”
16 So then he delivered him to them to be crucified. So they took Jesus.
Ndipo Pilato alipomtoa Yesu kwao ili asulibiwe.
17 And he went out, carrying the cross himself, to the place called "The Place of a Skull," which is called in Hebrew, "Golgotha,"
Nao wakamchukua Yesu, naye akatoka, hali ameubeba msalaba wake mwenyewe mpaka kwenye eneo liitwalo fuvu la kichwa, kwa Kihebrania huitwa Golgotha.
18 where they crucified him, and with him two others, on either side one, and Jesus in the middle.
Ndipo walipomsulibisha Yesu, pamoja naye wanaume wawili, mmoja upende huu na mwingine upande huu, na Yesu katikati yao.
19 Pilate wrote a title also, and put it on the cross. There was written, "JESUS THE NAZOREAN, THE KING OF THE JEWS."
Kisha Pilato akaandika alama na kuiwekwa juu ya msalaba. Hapo paliandikwa: YESU MNAZARETH, MFALME WA WAYAHUDI.
20 Therefore many Jews read this title, for the place where Jesus was crucified was near the city; and it was written in Hebrew, in Latin, and in Greek.
Wengi wa Wayahudi waliisoma alama hiyo kwani mahali pale aliposulibishwa Yesu palikuwa karibu na mji. Alama hiyo iliadikwa kwa Kiebrania, kwa Kirumi na kwa Kiyunani.
21 The chief priests of the Jewish people therefore said to Pilate, "Do not write, 'The King of the Jews,' but, 'he said, I am King of the Jews.'"
Kisha wakuu wa makuhani wa Wayahudi wakamwambia Pilato, “Usiandike, 'Mfalme wa Wayahudi; bali yeye alisema mimi ni mfalme wa Wayahudi.”
22 Pilate answered, "What I have written, I have written."
Naye Pilato akawajibu, “Niliyoandika nimeandika.”
23 Then the soldiers, when they had crucified Jesus, took his clothes and made four parts, to every soldier a part; and also the tunic. Now the tunic was without seam, woven from the top throughout.
Baada ya askari kumsulibisha Yesu, walichukua mavazi yake na kuyagawa katika mafungu manne, kila askari fungu moja, vivyo hivyo na kanzo, Sasa ile kanzu haikuwa imeshonwa bali ilkuwa imefumwa yote tokea juu.
24 Then they said to one another, "Let us not tear it, but cast lots for it to decide whose it will be," that the Scripture might be fulfilled, which says, "They divided my clothes among themselves, and for my clothing they cast a lot." Therefore the soldiers did these things.
Kisha wakasemezana wao kwa wao, “Tusiipasue, bali tupigeni kura ili kuona itakuwa ya nani.” Hili lilitokea ili lile andiko litimizwe, lile lisemalo waligawanya nguo zangu, na vazi langu wakalipigia kura.”
25 But there were standing by the cross of Jesus his mother, and his mother's sister, Mary the wife of Cleopas, and Mary Magdalene.
Askari walifanya mambo haya. Mama yake Yesu, dada wa mama yake, Mariamu mke wa Kleopa na Mariamu Magdalena - wanawake hawa walikuwa wamesimama karibu na msalaba wa Yesu.
26 Therefore when Jesus saw his mother, and the disciple whom he loved standing there, he said to his mother, "Woman, look, your son."
Yesu alipomwona mama yake pamoja na yule mwanafunzi aliyempenda wakisimama karibu, akamwambia mama yake, “Mwanamke, tazama, ona mwanao huyu hapa!”
27 Then he said to the disciple, "Look, your mother." From that hour, the disciple took her to his own home.
Kisha akamwambia yule mwanfunzi, “Tazama, huyu hapa mama yako. “Tokea saa hiyo yule mwanafunzi akamchukua kwenda nyumbani kwake.
28 After this, Jesus, knowing that all things were now finished, that the Scripture might be fulfilled, said, "I am thirsty."
Baada ya hilo, Hali Yesu akijua kuwa yote yamekwisha kumalizika ili kutimiza maandiko, akasema, “Naona kiu.”
29 A vessel full of sour wine was set there; so they put a sponge full of the vinegar on hyssop, and held it at his mouth.
Chombo kilichokuwa kimejaa Siki kilikuwa kimewekwa pale, kwa hiyo wakaweka sifongo iliyojaa siki juu ya ufito wa hisopo, wakamwekea mdomoni mwake.
30 When Jesus therefore had received the vinegar, he said, "It is finished." He bowed his head, and gave up his spirit.
Naye Yesu alipoionja hiyo, akasema, “Imekwisha.” Kisha akainamisha kichwa chake, akaikabidhi roho yake.
31 Therefore the Jewish leaders, because it was the Preparation Day, so that the bodies would not remain on the cross on the Sabbath (for that Sabbath was a special one), asked of Pilate that their legs might be broken, and that they might be taken away.
Kwa vile ilikuwa ni wakati wa maandalio, na kwa sababu miili haikutakiwa kubaki juu ya msalaba wakati wa Sabato (kwa kuwa Sabato ilikuwa siku ya muhimu), wayahudi walimwomba Pilato kuwa miguu yao wale wliokuwa wamesulibishwa ivunjwe, na kwamba miili yao ishushwe.
32 Therefore the soldiers came, and broke the legs of the first, and of the other who was crucified with him;
Ndipo askari walipokuja na kuvunja miguu ya mtu wa kwanza na wa pili aliyekuwa amesulibiwa pamoja na Yesu.
33 but when they came to Jesus, and saw that he was already dead, they did not break his legs.
Walipomfikia Yesu, walimkuta tayari alikuwa amekwisha kufa, kwa hiyo hawakuvunja miguu yake.
34 However one of the soldiers pierced his side with a spear, and immediately blood and water came out.
Hata hivyo, mmoja wa askari alimchoma Yesu ubavuni kwa mkuki, na mara yakatoka maji na damu.
35 He who has seen has testified, and his testimony is true. He knows that he tells the truth, that you may believe.
Naye aliyeona hili ametoa ushuhuda, na ushuhuda wake ni wa kweli. Yeye anajua kuwa alichokisema ni cha kweli ili nanyi pia muamini.
36 For these things happened, that the Scripture might be fulfilled, "A bone of him will not be broken."
Mambo haya yalikuwa ili lile neno lililonenwa lipate kutimia, “Hakuna hata wake mmoja utakaovunjwa.”
37 Again another Scripture says, "They will look on him whom they pierced."
Tena andiko lingine husema, “Watamtazama yeye waliyemchoma”
38 After these things, Joseph of Arimathea, being a disciple of Jesus, but secretly for fear of the Jewish leaders, asked of Pilate that he might take away the body of Jesus. Pilate gave him permission. He came therefore and took away his body.
Baada ya mambo haya Yusufu wa Arimathaya, kwa vile alikuwa mwanafunzi wa Yesu, lakini kwa siri kwa kuwaogopa Wayahudi, alimwomba Pilato kwamba auchukue mwili wa Yesu. Naye Pilato akampa ruhusa. Kwa hiyo Yusufu akaja kuuondoa mwili wa Yesu.
39 Nicodemus, who at first came to Jesus by night, also came bringing a mixture of myrrh and aloes, about seventy-five pounds.
Naye Nicodemo ambaye hapo awali alimfuata Yesu usiku naye akaja. Yeye alileta mchanganyiko wa manemane na udi, yapata uzito wa ratili mia moja.
40 So they took the body of Jesus, and bound it in linen cloths with the spices, according to Jewish burial practice.
Kwa hiyo wakauchukua mwili wa Yesu wakaufanga kwenye sanda ya kitani na pamoja na yale manukato, kama ilivyokuwa desturi ya wayahudi wakati wa kuzika.
41 Now in the place where he was crucified there was a garden. In the garden was a new tomb in which no one had ever yet been placed.
Mahali ambapo Yesu alisulibiwa kulikuwa na bustani; ndani ya ile bustani kulikuwa na kaburi jipya ambalo hakuna mtu alikuwa amawahi kuzikwa humo.
42 Then because of the Jewish Preparation Day (for the tomb was nearby) they put Jesus there.
Basi, kwa kuwa ilikuwa siku ya maandalio kwa Wayahudi, na kwa vile lile kaburi lilikuwa karibu, basi wakamlaza Yesu ndani yake.

< Yochanan 19 >