< Jacob 2 >
1 My brothers, do not hold the faith of our Lord Jesus (the) Messiah of glory with partiality.
Ndugu zangu, kama waaminio katika imani ya Bwana wetu Yesu Kristo, Bwana wa utukufu, msiwe na upendeleo kwa watu.
2 For if someone with a gold ring, in fine clothing, comes into your synagogue, and a poor person in filthy clothing also comes in;
Kwa maana kama akija mtu katika kusanyiko lenu akiwa amevaa pete ya dhahabu na mavazi mazuri, pia akaingia mtu maskini mwenye mavazi yaliyochakaa,
3 and you pay special attention to the one who wears the fine clothing, and say, "Sit here in a good place;" but you tell the poor person, "Stand there," or "Sit by my footstool."
nanyi mkampa heshima yule aliyevaa mavazi mazuri na kumwambia, “Keti hapa mahali pazuri,” lakini yule maskini mkamwambia, “Wewe simama pale,” au “Keti hapa sakafuni karibu na miguu yangu,”
4 Have you not discriminated among yourselves, and become judges with evil thoughts?
je, hamjawabagua na kuwa mahakimu mioyoni mwenu mkihukumu kwa mawazo yenu maovu?
5 Listen, my beloved brothers. Did not God choose those who are poor in this world to be rich in faith, and heirs of the Kingdom which he promised to those who love him?
Ndugu zangu, sikilizeni: Je, Mungu hakuwachagua wale walio maskini machoni pa ulimwengu kuwa matajiri katika imani na kuurithi Ufalme aliowaahidi wale wampendao?
6 But you have dishonored the poor person. Do not the rich oppress you, and personally drag you before the courts?
Lakini ninyi mmemdharau yule aliye maskini. Je, hao matajiri si ndio wanaowadhulumu na kuwaburuta mahakamani?
7 Do not they blaspheme the honorable name by which you are called?
Je, si wao wanaolikufuru Jina lile lililo bora sana mliloitiwa?
8 However, if you fulfill the royal law, according to the Scripture, "You are to love your neighbor as yourself," you do well.
Kama kweli mnaitimiza ile sheria ya kifalme inayopatikana katika Maandiko isemayo, “Mpende jirani yako kama unavyoipenda nafsi yako,” mnafanya vyema.
9 But if you show partiality, you commit sin, being convicted by the law as transgressors.
Lakini kama mnakuwa na upendeleo kwa watu, mnatenda dhambi, na sheria inawahukumu kuwa ninyi ni wakosaji.
10 For whoever keeps the whole law, and yet stumbles in one point, he has become guilty of all.
Kwa maana mtu yeyote anayeishika sheria yote lakini akajikwaa katika kipengele kimoja tu, ana hatia ya kuivunja sheria yote.
11 For he who said, "Do not commit adultery," also said, "Do not commit murder." Now if you do not commit adultery, but murder, you have become a transgressor of the law.
Kwa sababu yeye aliyesema, “Usizini,” alisema pia, “Usiue.” Basi kama huzini lakini unaua, umekuwa mvunjaji wa sheria.
12 So speak, and so do, as those who are to be judged by a law of freedom.
Hivyo semeni na kutenda kama watu watakaohukumiwa kwa sheria ile iletayo uhuru.
13 For judgment is without mercy to him who has shown no mercy. Mercy triumphs over judgment.
Kwa kuwa hukumu bila huruma itatolewa kwa mtu yeyote asiyekuwa na huruma. Huruma huishinda hukumu.
14 What good is it, my brothers, if someone says he has faith, but has no works? Can faith save him?
Ndugu zangu, yafaa nini ikiwa mtu atadai kuwa anayo imani lakini hana matendo? Je, imani kama hiyo yaweza kumwokoa?
15 And if a brother or sister is poorly clothed and may be lacking in daily food,
Ikiwa ndugu yako au dada hana mavazi wala chakula,
16 and one of you tells them, "Go in peace, be warmed and filled;" and yet you did not give them the things the body needs, what good is it?
mmoja wenu akamwambia, “Enenda zako kwa amani, ukaote moto na kushiba,” pasipo kumpatia yale mahitaji ya mwili aliyopungukiwa, yafaa nini?
17 Even so faith, if it has no works, is dead in itself.
Vivyo hivyo, imani peke yake kama haikuambatana na matendo, imekufa.
18 But someone will say, "You have faith, and I have works." Show me your faith without works, and I by my works will show you my faith.
Lakini mtu mwingine atasema, “Wewe unayo imani; mimi ninayo matendo.” Nionyeshe imani yako pasipo matendo nami nitakuonyesha imani yangu kwa matendo.
19 You believe that God is one. You do well. The demons also believe, and shudder.
Unaamini kwamba kuna Mungu mmoja. Vyema! Hata mashetani yanaamini hivyo na kutetemeka.
20 But do you want to know, foolish person, that faith apart from works is useless?
Ewe mpumbavu! Je, wataka kujua kwamba imani bila matendo haifai kitu?
21 Wasn't Abraham our father justified by works, in that he offered up Isaac his son on the altar?
Je, Abrahamu baba yetu hakuhesabiwa haki kwa kile alichotenda, alipomtoa mwanawe Isaki madhabahuni?
22 You see that faith worked with his works, and by works faith was perfected;
Unaona jinsi ambavyo imani yake na matendo yake vilikuwa vinatenda kazi pamoja, nayo imani yake ikakamilishwa na kile alichotenda.
23 and the Scripture was fulfilled which says, "And Abraham believed God, and it was credited to him as righteousness;" and he was called the friend of God.
Kwa njia hiyo yakatimizwa yale Maandiko yasemayo, “Abrahamu alimwamini Mungu na ikahesabiwa kwake kuwa haki,” naye akaitwa rafiki wa Mungu.
24 You see that a person is justified by works and not by faith alone.
Mnaona ya kwamba mtu huhesabiwa haki kwa yale anayotenda wala si kwa imani peke yake.
25 In like manner was not Rahab the prostitute also justified by works, in that she received the messengers, and sent them out another way?
Vivyo hivyo, hata Rahabu, yule kahaba, hakuhesabiwa haki kwa yale aliyotenda alipowapokea wale wapelelezi na kuwaambia waende njia nyingine?
26 For as the body apart from the spirit is dead, even so faith apart from works is dead.
Kama vile ambavyo mwili pasipo roho umekufa, kadhalika nayo imani pasipo matendo imekufa.