< Isaiah 52 >

1 Awake, awake, put on your strength, Zion; put on your beautiful garments, Jerusalem, the holy city, for there shall no more enter into you the uncircumcised and the unclean.
Amka, amka, vaa nguvu zako, Sayuni; vaa vazi lako zuri, mji mtakatifu; maana hakuna tena kutotahiriwa wala wasio safi kuingia kwako.
2 Shake yourself from the dust. Arise, sit up, Jerusalem. Release yourself from the bonds of your neck, captive daughter of Zion.
Jikung'ute mwenyewe kutoka mavumbini; nyanyuka na ukae, ewe Yerusalemu; ondoa shanga katika shingo yako, wafungwa, binti ya Sayuni.
3 For thus says the LORD, "You were sold for nothing; and you shall be redeemed without money."
Maana Yahwe asema hivi, umeuzwa bure, na utakombolewa pasipo pesa.''
4 For thus says the LORD, "My people went down at the first into Egypt to live there, and the Assyrian oppressed them without cause.
Maana Bwana Yahwe asema hivi, ''Hapo mwanzo watu wangu walishuka chini Misri kuishi kwa muda mfupi; Waasiria waliwanyanyasa wao hivi karibuni.
5 "Now therefore, what do I do here," says the LORD, "seeing that my people are taken away for nothing? Those who rule over them mock," says the LORD. "Because of you, my name is continually all the day blasphemed among the nations.
Sasa ni kitu gani nilicho nacho hapa- Hili ni tamko Yahwe- aonae kwamba watu wake wanachukuliwa bure tu? Wale wanowaongoza wao wanafanya mzaha-Hili ni tamko la Yahwe- jina langu linakashifiwa mchan kutwa.
6 Therefore my people shall know my name; in that day they will know that I am he who speaks; look, it is I."
Hivyo basi watu wangu watalijua jina langu; watajua kwamba siku hiyo kwamba mimi ndiye ninayesema ''Ndiyo, Ni Mimi!''
7 How beautiful on the mountains are the feet of him who brings good news, who publishes peace, who brings good news of good things, who publishes salvation, who says to Zion, "Your God reigns."
Ni kwa uzuri gani juu miliima ni miguu ya mjumbe aliyeleta habari njema, atangazae amani, aliyebeba uzuri wa ukuu, aliyetangaza wokovu, anayesema kwa Sayuni, ''Mungu wako anatawala!''
8 The voice of your watchmen. They lift up the voice, together do they sing; for they shall see eye to eye, when the LORD returns to Zion with compassion.
Sikiliza enyi walinzi nyanyueni sauti zenu, kwa pamoja pigeni kelele kwa furaha, maana mtamuona, kwa kila jicho lenu, kurejea kwa Yahwe Sayuni.
9 Break forth into joy, sing together, you waste places of Jerusalem; for the LORD has comforted his people, he has redeemed Jerusalem.
Pazeni sauti kwa kuimba kwa furaha, enyi mateka wa Yerusalemu; maana Yahwe amefariji watu wake; ameikomboa Yerusalemu.
10 The LORD has made bare his holy arm in the eyes of all the nations; and every part of the earth has seen the salvation of our God.
Yahwe amewaonyesha kwamba mkono wake mtakatifu katika macho ya mataifa yote; nchi yote itauona wokovu wa Mungu wetu.
11 Depart, depart, go out from there, and touch no unclean thing. Go out from their midst, and be separate, you who bear the vessels of the LORD.
Ondokeni, ondokeni, enendeni mbali na hapa; msiguse kitu chochote ambacho ni najisi; au kuishi katikati yake; jitakase mwenyewe, enyi mliobeba vyombo vya Yahwe.
12 For you shall not depart in haste, nor shall you leave in flight; for the LORD will go before you, and the God of Israel will be your rear guard.
Maana hautakwenda nje kwa kukimbia, wala hautaondoka kwa hofu; Maana Yahwe atakuwa mbele yako; na Mungu wa Israeli atakuwa mlinzi wako nyuma.
13 Look, my servant shall deal wisely, he shall be exalted and lifted up, and shall be very high.
Tazameni, mtumishi wangu atafanya hekima; atakuwa juu na atanyanyuliwa juu, na atapandishwa juu.
14 Just as many were astonished at you (his appearance was marred more than any man, and his form more than the sons of men),
Na wengi watamstajabia yeye- muonekano wake umekunjamana nje ya muonekano wa mwanadamu, hivyo basi upande wake ulikuwa mbali na kitu chochote ambacho ni binadamu-
15 so shall he sprinkle many nations; kings shall shut their mouths at him. For that which was not told about him, they will see, and what they have not heard, they will understand.
Na hivyo, mtumishi wangu atanyunyizia mataifa mengi na wafme watafunga midomo yao kwa sababu yake. Kana kwamba hawajawahi kuambiwa, wataona, kana kwamba hawakusikia, wataelewa.

< Isaiah 52 >