< Daniel 8 >

1 In the third year of the reign of king Belshazzar a vision appeared to me, Daniel, after that which appeared to me previously.
Katika mwaka wa tatu wa utawala wa mfalme Belshaza, mimi Danieli niliona maono (baada ya maono ya awali yaliyonipata).
2 And I saw in the vision, and when I looked, I was in the citadel of Shushan, which is in the province of Elam. And I saw in the vision, and I was by the river Ulai.
Nilipokuwa nikiangalia katika ndoto, niliona kwamba nilikuwa katika mji wa Shushani wenye ngome katika jimbo la Elamu. Niliona katika ndoto kuwa nilikuwa karibu na mfereji wa Ulai.
3 Then I lifted up my eyes, and saw, and look, there stood before the river a ram which had two horns. And the two horns were long, but one was longer than the other, and the longer one came up last.
Nilitazama juu na nikaona mbele yangu kondoo dume lenye mapembe mawili, limesimama pembeni mwa mfereji. Pembe moja lilikuwa refu kuliko jingine, lakini pembe ndefu ilikuwa inakua pole pole kuliko ile fupi na pembe fupi ilirefuka na kuizidi nyingine.
4 I saw the ram pushing westward, and northward, and southward; and no animals could stand before him, neither was there any who could deliver out of his hand. But he did according to his will, and became great.
Niliona kondoo mme akiishambulia magharibi, kisha kaskazini, na baadaye kusini; hakuna mnyama mwingine aliyeweza kusimama mbele yake. Hakuna yeyote aliyeweza kumwokoa yeyote katika mkono wake. Alifanya chochote kile alichokitaka, na alikuwa mtu mkubwa sana.
5 As I was considering, look, a male goat came from the west over the surface of the whole earth, and did not touch the ground. And the goat had a prominent horn between his eyes.
Na nilipokuwa natafakari juu ya haya, niliona beberu akitoka magharibi, na kuvuka katika uso wa dunia yote, akikimbia kwa kasi kana kwamba hakuonekana kama aligusa ardhini. Mbuzi huyo alikuwa na pembe kubwa katikati ya macho yake.
6 He came to the ram that had the two horns, which I saw standing before the river, and rushed at him in the fury of his power.
Alienda mpaka kwa kondoo aliyekuwa na pembe mbili, nilikuwa nimemwona kondoo dume amesimama katika ukingo wa mfereji na mbuzi alikimbia kumwelekea kondoo dume kwa hasira kali.
7 I saw him come close to the ram, and he was moved with anger against him, and struck the ram, and broke his two horns. And there was no power in the ram to stand before him, but he threw him down to the ground and trampled on him, and there was no one who could deliver the ram from his power.
Niliiona mbuzi ikija karibu na kondoo. Mbuzi alikuwa na hasira na kondoo, alimpiga kondoo na alizivunja pembe zake mbili. Kondoo hakuwa na nguvu za kusimama mbele zake. Mbuzi alimgonga kondoo akaanguka chini na akamkanyaga. Hapakuwa na yeyote wa kumwokoa kutoka katika nguvu zake.
8 The male goat became very strong. But when he was strong, the large horn was broken; and instead of it there came up four prominent horns toward the four winds of heaven.
Ndipo mbuzi alikua akawa mkubwa, lakini alipokuwa na nguvu, pembe kubwa ilivunjwa, na katika sehemu yake zilichipuka na kukua pembe nne kubwa zilizochomoza kuelekea pepo nne za mbingu.
9 Out of one of them came forth a little horn, which grew exceeding great, toward the south, and toward the east, and toward the beautiful land.
Kutoka katika pembe moja ilichipuka pembe nyingine, ilikuwa ndogo hapo awali, lakini baadaye ilikuwa pembe kubwa upande wa kusini, na mashariki, na katika nchi ya uzuri.
10 It grew so great that it reached to the host of heaven, and some of the host and of the stars it cast down to the ground, and trampled on them.
Pembe ilikuwa kubwa na matokeo yake iliinua vita dhidi ya jeshi la mbinguni. Baadhi ya jeshi na nyota kadhaa zilitupwa chini duniani, na zilikanyagwa.
11 And it magnified itself, even against the Prince of the host; and it took away from him the daily sacrifice, and the place of his sanctuary was thrown down.
Alizidi kuwa mkubwa, mkubwa kama kamanda wa jeshi la kimungu. Sadaka za kuteketezwa za kila siku ziliondolewa mbali na yeye, na sehemu yake takatifu zilitiwa unajisi.
12 The host was given over to it together with the daily sacrifice because of transgression. And it cast down truth to the ground, and kept prospering.
Kwasababu ya uasi, pembe ya mbuzi ilipewa jeshi, na sadaka za kuteketezwa zitasitishwa. Pembe itautupa ukweli chini ardhini, na itafanikiwa katika kila jambo ilifanyalo.
13 Then I heard a holy one speaking; and another holy one said to that certain one who spoke, "How long shall be the vision concerning the daily sacrifice, and the transgression that makes desolate, to give both the sanctuary and the host to be trampled?"
Kisha nilimsikia mtakatifu mmoja akiongea na mtakatifu mwingine akamjibu, “Mambo haya yatadumu kwa muda gani, maono haya ya sadaka ya kuteketezwa, dhambi ile iletayo uharibifu, ukabidhiajia wa sehemu takatifu, na jeshi la mbinguni kukanyagwa?
14 He said to me, "To two thousand and three hundred evenings and mornings; then shall the sanctuary be restored to its rightful state."
Aliniambia, “Itadumu kwa jioni na asubuhi zipatazo 2, 300. Baada ya hapo, mahali patakatifu patawekwa sawa.”
15 It came about when I, Daniel, had seen the vision, that I sought to understand it. And look, there stood before me someone who appeared to be a man.
Wakati mimi Danieli, nilipoona maono, nilijaribu kuyaelewa. na hapo mbele yangu alisimama yule aliyeoneakana kama mtu.
16 I heard a man's voice between the banks of the Ulai, and called out and said, "Gabriel, make this man understand the vision."
Niliisikia sauti ya mtu ikiita katikati ya kingo za mfereji wa Ulai. Alisema, “Gabrieli, msaidie mtu huyu kuelewa maono.”
17 So he came near where I stood, and when he came I was frightened, and fell prostrate. But he said to me, "Understand, son of man, that the vision belongs to the time of the end."
Basi alikuja karibu na mahali niliposimama. Na alipokuja, niliogopa na nilisujudia hadi chini. Aliniambia,”Fahamu, mwana wa mtu, kwamba maono ni kwa ajili ya wakati wa mwisho.”
18 Now as he was speaking with me, I fell into a deep sleep with my face toward the ground; but he touched me, and stood me upright.
Alipokuwa anaongea na mimi, nilipata usiingizi mzito nikiwa nimelala kifudifudi. Kisha alinishika na kunisimamisha.
19 He said, "Look, I will make you know what shall be in the latter time of wrath, for it belongs to the appointed time of the end.
Akaniambia, “Tazama, nitakuonyesha kile kitachotokea baadaye katika kipindi cha ghadhabu, kwasababu maono haya yanahusu wakati wa mwisho uliopangwa.
20 The ram which you saw, that had the two horns, they are the kings of Media and Persia.
Na kuhusu kondoo mme uliyemwona, yule mwenye pembe mbili - ni wafalme wawili wa Umedi na Uajemi.
21 The male goat is the king of Greece, and the large horn that is between his eyes is the first king.
Mbuzi dume ni mfalme wa Ugiriki. Pembe kubwa katikati ya macho yake ni mfalme wa kwanza.
22 As for that which was broken, in the place where four stood up, four kingdoms shall arise out of his nation, but not with his power.
Na kuhusu pembe iliyovunjika, ambayo katika nafasi yake pembe zingine nne zilichipuka - hizi ni falme nne zitakazoinuka kutoka katika taifa lake, lakini hazitakuwa na nguvu kubwa.
23 In the latter time of their kingdom, when the transgressions have reached their full measure, a rash and deceitful king shall arise.
Katika siku zijazo za falme hizo, wakati ambapo wahalifu watakuwa wamefikia kikomo chao, mfalme mwenye uso katili, na yeye mwenye akili sana, atainuka.
24 His power shall be great, but not by his own strength; and he shall cause terrible destruction, and shall succeed in whatever he does. And he shall destroy the mighty and the holy people.
Nguvu zake zitakuwa kubwa, lakini si kwa nguvu zake mwenyewe. Atakuwa wa kustaajabisha kwa kile atakachokuwa anakiharibu; atafanya na kufanikiwa. Atawaangamiza watu wenye nguvu, watu miongoni wa watakatifu.
25 Through his cunning he shall cause deceit to prosper by his influence, and he shall be great in his own mind, and without warning he shall destroy many. He shall also stand up against the Prince of princes; but he shall be shattered, but not by human hands.
Ataufanya udanganyifu usitawi chini ya mkono wake kwasababu ya ujanja wake. Atawaangamiza watu wengi bila kutegemea. Atainuka pia hata kinyume cha Mfalme wa wafalme, na atavunjwa, lakini si kwa mkono wowote wa binadamu.
26 The vision of the evenings and mornings which has been told is true; but seal up the vision because it refers to many days from now."
Maono kuhusu jioni na asubuhi ulizoambiwa ni ya kweli. Lakini uyafunge maono haya, kwa kuwa yanahusu siku nyingi za wakati ujao.
27 I, Daniel, was overcome, and was ill for days. Then I rose up, and carried out the king's business. And I was astonished by the vision, but there was no one to explain it.
Ndipo mimi, Danieli nilichoka sana na nikalala nikiwa dhaifu kwa siku kadhaa. Kisha nikainuka na nikaenda kufanya kazi za mfalme. Lakini nilikuwa nimetishwa sana na maono, na hapakuwa na mtu yeyote aliyeweza kuyaelewa.

< Daniel 8 >