< 2 Kings 2 >

1 It happened, when the LORD would take up Elijah by a whirlwind into heaven, that Elijah went with Elisha from Gilgal.
Hivyo ilipokuja kuhusu, wakati Yahwe alipokuwa akienda kumchukua Eliya kwenda mbinguni kwa uvumi, ambapo Eliya aliondoka pamoja na Elisha kutoka Gigali.
2 Elijah said to Elisha, "Please wait here, for the LORD has sent me as far as Bethel." Elisha said, "As the LORD lives, and as your soul lives, I will not leave you." So they went down to Bethel.
Eliya akamwambia Elisha, '“kaa hapa, tafadhali, kwa sababu Yahwe alinituma kwa Betheli.'” Elisha akajibu, “Kama Yahwe aishivyo, na kama uishivyo, sintokuacha.'” Hivyo wakashuka chini kulekea Betheli.
3 The sons of the prophets who were at Bethel came out to Elisha, and said to him, "Do you know that the LORD will take away your master from your head today?" He said, "Yes, I know it; hold your peace."
Wana wa manabii ambao walikuwa Betheli walikuja kwa Elisha na kumwambia, je unajua kwamba Yahwe atamwondoa bwana wako kuanzia leo?”' Elisha akajibu, “Ndiyo, nalijua hilo, ila msizungumze kuhusu hilo.”'
4 Elijah said to him, "Elisha, please wait here, for the LORD has sent me to Jericho." He said, "As the LORD lives, and as your soul lives, I will not leave you." So they came to Jericho.
Eliya akamwambia, “Elisha, subiri hapa, tafadhali, kwa kuwa Yahwe amenituma niende Yeriko.” Kisha Elisha akajibu, '“Kama Yahwe aishivyo, na kama uishivyo, sintokuacha.” Hivyo wakaenda Yeriko.
5 The sons of the prophets who were at Jericho came near to Elisha, and said to him, "Do you know that the LORD will take away your master from your head today?" He answered, "Yes, I know it. Hold your peace."
Kisha wana wa manabii ambao walikuwa Yeriko wakaja kwa Elisha na kumwambia, “'Je unajua kwamba Yahwe atamwondoa bwana wako kutoka kwako leo?” Elisha akajibu, “Ndiyo, nalijua hilo, lakini msilizungumzie hilo.”
6 Elijah said to him, "Please wait here, for the LORD has sent me to the Jordan." He said, "As the LORD lives, and as your soul lives, I will not leave you." They both went on.
Kisha Eliya akamwambia, '“kaa hapa, tafadhali, kwa kuwa Yahwe amenituma kwenda Yeriko.” Elisha akajibu, “Kama Yahwe ishivyo, na kama uishivyo, sintokuacha.” Hivyo wawili wakaenda mbele.
7 Fifty men of the sons of the prophets went, and stood opposite them at a distance; and they both stood by the Jordan.
Baadaye watu hamsini wa watoto wa wale manabii wakasimama kuwakabili kwa mbali kidogo wale wawili wakasimama karibu na Yordani.
8 Elijah took his cloak, and wrapped it together, and struck the waters, and they were divided here and there, so that the two of them went over on dry ground.
Eliya akachukua vazi lake, akaliviringisha, na kuyapiga maji kwa kutumia lile vazi. Ule mto ukagawanyika katika sehemu mbili hivyo basi wawili hao wakatembea hadi nchi kavu.
9 It happened, when they had gone over, that Elijah said to Elisha, "Ask what I shall do for you, before I am taken from you." Elisha said, "Please let a double portion of your spirit be on me."
Ilitokea, walipokwisha kuvuka, kwamba Eliya akamwambia Elisha, “Niambie unachotaka nifanye kwako kabla sijaondolewa kutoka kwako.” Elisha akajibu, “Naomba sehemu kubwa ya roho yako ije kwangu.
10 He said, "You have asked a hard thing. If you see me when I am taken from you, it shall be so for you; but if not, it shall not be so."
Eliya akajibu, “Umeomba jambo gumu. Hata hivyo, kama ukiniona wakati nitakapoondolewa kutoka kwako, hii itatokea kwako, lakini kama sivyo, haitatokea.”
11 It happened, as they still went on, and talked, that look, a chariot of fire and horses of fire separated them; and Elijah went up by a whirlwind into heaven.
Ikawa walipokuwa bado wakienda mbele na kuzungumza, gari la kukokotwa na farasi lenye moto na farasi wa moto ikatokea, ambapo iliwatenga wale watu wawili kutoka kila mmoja, na Eliya akaenda juu kwa uvumi wa upepo kwenda mbinguni.
12 Elisha saw it, and he cried, "My father, my father, the chariots of Israel and its horsemen." He saw him no more: and he took hold of his own clothes, and tore them in two pieces.
Elisha akaiona akalia kwa sauti, “Baba yangu, baba yangu, gari la kukokotwa na farasi la Israeli na waendesha farasi!'” Hakumwona Eliya tena, na akashikilia nguo zake mwenyewe na kugawanya kwenye vipande viwili.
13 And he picked up the cloak of Elijah that fell from him, and went back, and stood by the bank of the Jordan.
Akachukua vazi la Eliya lililokuwa limemwangukia, na kurudi kusimama kwenye ukingo wa Yordani.
14 And he took the cloak of Elijah that fell from him, and struck the water, and it did not divide. And he said, "Where is the LORD, the God of Elijah, even he?" And he struck the water a second time, and they divided to the one side and to the other; and Elisha crossed over.
Akayapiga maji pamoja na lile vazi la Eliya alilokuwa ameliangusha na kusema, “Yahwe yuko wapi, Mungu wa Eliya?'” Wakati alipoyapiga yale maji, yaligawanyika katika pande mbili na Elisha akavuka.
15 When the sons of the prophets who were at Jericho over against him saw him, they said, "The spirit of Elijah rests on Elisha." They came to meet him, and bowed themselves to the ground before him.
Wakati hao wana wa manabii ambao walitoka Yeriko walipomuona akikatiza kwao, wakasema, “roho ya Eliya imepumzika kwa Elisha!” Hivyo wakaja kuonana naye, na wakasujudu aridhini mbele yake.
16 And they said to him, "See now, there are with your servants fifty strong men. Please let them go and seek your master. Perhaps the Spirit of the LORD has taken him up and thrown him into the Jordan, or on some mountain, or into some valley." And he said, "Do not send them."
Wakamwambia, “Ona sasa, miongoni mwa watumishi wako kuna watu hamsini hodari. Tunakuomba Waache waende, na kumtafuta bwana wako, endapo huyo Roho wa Yahwe alipomchukua juu na kumtupa juu ya mlima mmoja au kwenye bonde moja.” Elisha akajibu, “Hapana, msiwatume.”
17 When they urged him until he was ashamed, he said, "Send them." They sent therefore fifty men; and they searched for three days, but did not find him.
Lakini walimsihi Elisha hadi akaona aibu, akasema, “Watume.”Ndipo wakawatuma watu hamsini, na wakatafuta kwa mda wa siku tatu, lakini hawakumpata.
18 They came back to him, while he stayed at Jericho; and he said to them, "Did I not tell you not to go?"
Wakarudi kwa Elisha, wakati alipokuwa bado yuko Yeriko, na akasema, “Je sikusema, 'msiende'?”
19 The men of the city said to Elisha, "Look, please, the situation of this city is pleasant, as my lord sees; but the water is bad, and the land miscarries."
Watu wa mjini wakamwambia Elisha, “Ona, tunakuomba, hali ya mjini hapa ni pazuri, kama bwana wangu awezavyo kuona, lakini maji ni mabaya na hiyo nchi haiwezi kuzaa matunda.”
20 He said, "Bring me a new jar, and put salt in it." They brought it to him.
Elisha akajibu, “Nileteeni bakuli jipya na muweke chumvi ndani ya hilo bakuli,” hivyo wakamletea.
21 He went out to the spring of the waters, and threw salt into it, and said, "Thus says the LORD, 'I have healed these waters. There shall not be from there any more death or miscarrying.'"
Elisha akaenda hadi kwenye chemichemi za maji na kutupia chumvi ndani; halafu akasema, “Yahwe asema hivi, 'Nimeyaponya haya maji. Kuanzia mda huu, hakutakuwa na kifo au nchi isiyozaa matunda.
22 So the waters were healed to this day, according to the word of Elisha which he spoke.
“Hivyo hayo maji yakaponya hata leo, kwa lile neno ambalo Elisha aliongea.
23 He went up from there to Bethel. As he was going up by the way, some youths came out of the city and mocked him, and said to him, "Go up, you baldy. Go up, you baldhead."
Ndipo Elisha akapanda kutoka pale mpaka Betheli. Naye alipokuwa akienda hadi kwenye barabara, wakatokea vijana nje ya mji na kumtania, wakamwambia, “Panda juu, wewe mwenye kipara! Panda juu, wewe mwenye kipara!”
24 He looked behind him and saw them, and cursed them in the name of the LORD. Two female bears came out of the woods, and mauled forty-two of those youths.
Elisha alipotazama nyuma yake na kuwaona; alimwambia Yahwe awalaani. Ndipo dubu wa kike wawili wakatokea kichakani na kuwajeruhi vijana arobaini na mbili.
25 He went from there to Mount Carmel, and from there he returned to Samaria.
Ndipo Elisha alipoondoka pale na kuelekea Mlima Karmeli, na kutoka huko alirudi samaria.

< 2 Kings 2 >