< 1 Kings 7 >

1 Solomon was building his own house thirteen years, and he finished all his house.
Ilimchukua Sulemani miaka kumi na tatu kujenga ikulu yake.
2 For he built the house of the forest of Lebanon; its length was one hundred seventy-two feet and three inches, and its breadth eighty-six feet and two inches, and its height fifty-one feet and eight inches, on four rows of cedar pillars, with cedar beams on the pillars.
Aliijenga ikulu iliyoitwa mwitu wa Lebanoni. Urefu wake ulikuwa mita 46, na upanawake ulikuwa mita 23, na kimo chake kilikuwa mita 14. Nayo ilikuwa na safu nne ya nguzo za mierezi na mithili ya mwerezi juu ya nguzo.
3 It was covered with cedar above atop the beams which were on the pillars, and the pillars numbered forty-five; fifteen in a row.
Paa la ikulu lilikuwa la mwerezi ambalo lilikaa juu ya mihimili. Mihili hiyo ilikuwa imeshikiliwa na nguzo. Kulikuwa na mihimili arobaini na tano, ambayo ilikuwa katika safu kumi na tano.
4 There were beams in three rows, and window was over against window in three ranks.
Nayo mihimili ilikuwa safu tatu, na kila dirisha lilikabili dirisha lingine katika madaraja matatu.
5 All the doors and posts were made square with beams: and window was over against window in three ranks.
Milango yote na miimo ilitengenezwa kwa mraba, na madirisha yalikuwa yakikabiliana katika madaraja matatu
6 He made the porch of pillars; its length was eighty-six feet and two inches, and its breadth fifty-one feet and eight inches; and a porch before them; and pillars and a threshold before them.
Akatengeneza baraza lenye uerfu wa mita 23 na upana wa mita 14. Mbele yake kulikuwa na ukumbi ulioezekwa.
7 He made the porch of the throne where he was to judge, even the porch of judgment: and it was covered with cedar from floor to rafters.
Sulemani akajenga baraza yenye kiti cha enzi ambacho alitolea hukumu ya haki. Nayo ilikuwa imeezekwa kwa mwerezi kutoka sakafu moja hadi nyingine.
8 His house where he was to dwell, the other court within the porch, was of the like work. He made also a house for Pharaoh's daughter (whom Solomon had taken as wife), like this porch.
Nyumba ya Sulemani ambayo alikusudia kuishi, katika behewa nyingine ndani ya sehemu ya chini ya ikulu, ilitengenezwa kwa kazi hiyo hiyo. Pia alimjengea binti wa Farao nyumba kama hii, ambaye alikuwa mke wake
9 All these were of costly stones, even of cut stone, according to measure, sawed with saws, inside and outside, even from the foundation to the coping, and so on the outside to the great court.
Majengo haya yalipmbwa kwa vitu vya thamaini, mawe ya thamani, yaliyochongwa na kukatwa kwa msimeno kufuata vipimo sahihi na kulainishwa pande zote. Mawe ya namna hii ndiyo yale yaliyotumika kuanzia kwenye msingi hadi juu, pia na nje hadi kwenye baraza.
10 The foundation was of costly stones, even great stones, stones of seventeen feet and three inches, and stones of thirteen feet and nine inches.
Msingi ulijengwa kwa mawe makubwa sana na ya thamani yenye urefu wa mita 3. 7 na mengine mita 4. 8.
11 Above were costly stones, even cut stone, according to measure, and cedar wood.
Kwa juu ilipambwa kwa, mawe ya thamani yaliyochongwa sawa sawa kwa msimeno na kwa mihimili ya mierezi.
12 The great court around had three courses of cut stone, and a course of cedar beams; like as the inner court of the house of the LORD, and the porch of the house.
Na behewa kubwa iliyokuwa ikizunguka ikulu ilikuwa na safu tatu za mawe yaliyokatwa na safu moja ya mihimili ya mierezi kama ilivyo kwenye baraza la ndani la hekalu la BWANA na ule ukumbi wa hekalu.
13 King Solomon sent and fetched Hiram out of Tyre.
Mfalme Sulemani alituma watu kumleta Huramu kutoka Tiro.
14 He was the son of a widow of the tribe of Naphtali, and his father was a man of Tyre, a worker in bronze; and he was filled with wisdom and understanding and skill, to work all works in bronze. He came to king Solomon, and performed all his work.
Huramu alikuwa mwana wa mjane wa kabila ya Naftali; baba yake alikuwa mtu wa Tiro, mfua shaba. Huramu alikuwa mwingi wa hekima na ufahamu na stadi za kufanya kazi kubwa za shaba. Aliletwa kwa mfalme ili kufanya kazi zilizohusiana na shaba kwa mfalme.
15 For he cast the two pillars of bronze, thirty-one feet was the height of one pillar; and a line of twenty feet and eight inches could encompass the one pillar, and its thickness hollowed out was almost three inches; and so was the second pillar.
Huramu alizilemba zile nguzo mbili za shaba, kila moja ilikuwa na kimo cha mita 8. 3 na mzingo wa mita 5. 5.
16 He made two capitals of molten bronze, to set on the tops of the pillars: the height of the one capital was eight feet and seven inches, and the height of the other capital was eight feet and seven inches.
Akatengeneza taji mbili za shaba za kuwekwa juu ya zile nguzo. Kimo cha kila taji ilikuwa mita 2. 3.
17 There were nets of checker work, and wreaths of chain work, for the capitals which were on the top of the pillars; seven for the one capital, and seven for the other capital.
Kulikuwa na nyavu za kuwa kama kazi ya kusuka, na masongo ya mikufu, kwa ajili ya kuvipamba vile vichwa vya nguzo, nayo yailikuwa saba kwa kila kichwa.
18 So he made the pomegranates, two rows around on the one network, to cover the capitals that were on the top of the pillars; and he did so for the other capital.
Kwa hiyo Huramu akafanya safu mbili za komamanga kuzunguka vile vichwa vya nguzo ili kuvipamba vile vichwa.
19 The capitals that were on the top of the pillars in the porch were of lily work, six feet and eleven inches.
Zile taji kwenye vile vichwa vya nguzo za ukumbi zilikuwa zimepambwa kwa maua, yenye vimo vya mita 1. 8.
20 And the capitals were on the two pillars, even above and close to the rounded projection which was beside the network. And there were two hundred pomegranates in rows all around on the capital, and the same around the other capital.
Hizo taji kwenye hizo nguzo mbili kwenye vichwa vyake, karibu yake kulikuwa na makomamanga mia mbili yote yakiwa kwenye safu.
21 He set up the pillars at the porch of the temple: and he set up the right pillar, and called its name Jakin; and he set up the left pillar, and called its name Boaz.
Alisimamisha nguzo kwenye ukumbi wa hekalu. Ile nguzo ya kuume akaipa jina la Yakini, na ile ya kushoto akaipa jina la Boazi.
22 On the top of the pillars was lily work: so was the work of the pillars finished.
Na juu ya zile nguzo kulikuwa na mapambo kama maua. Hivyo ndivyo zile nguzo zilivyotengenezwa.
23 He made the molten sea of seventeen feet and three inches from brim to brim, round in compass, and its height was eight feet and seven inches; and a line of fifty-one feet and eight inches encircled it.
Tena akafanya bahari ya kusubu ya, yenye mita 2. 3 kutoka ukingo hadi ukingo, kimo chake kilikuwa mita 4. 6, mziingo wake ulikuwa mita 13. 7.
24 Under its brim around there were buds which encircled it, for seventeen feet and three inches, encircling the sea: the buds were in two rows, cast when it was cast.
Na chini ya ile bahari kulikuwa na vibuyu vilivyoizunguka, vilikuwa vibuyu kumi na nane katika kila mita, vilivyowekwa katika kila hicho kipande wakati bahari inapokuwa kalibu.
25 It stood on twelve oxen, three looking toward the north, and three looking toward the west, and three looking toward the south, and three looking toward the east; and the sea was set on them above, and all their backs were toward the center.
Bahari ikakaa juu ya makisai kumi na mbili, tatu, zilitazama kaskazini, tatu zikitazama magharibi, tatu zikitazama kusini na tatu zikitazama kaskazini. Ile bahari iliwekwa juu yao, na pande zao zote za nyuma zilikuwa ndani.
26 It was almost three inches thick: and its brim was worked like the brim of a cup, like the flower of a lily: it held two thousand baths.
Bahari ilikuwa nene kama upana wa mkono, na ukingo wake ulikuwakama ukingo wa kikombe, kama ua la yungi huingia bathi elfu mbili za maji.
27 He made the ten bases of bronze; six feet and eleven inches was the length of one base, and six feet and eleven inches its breadth, and five feet and two inches its height.
Huramu akatengeneza makalio kumi ya shaba. Kila kalio lilkuwa na urefu wa mita 1. 8, upana wa mita 1. 8, na kimo cha mita 1. 3.
28 The work of the bases was like this: they had panels; and there were panels between the ledges;
Hivi ndivyo kazi za makalio zilivyofanywa. Yalikuwa na papi ambazo zilikaa kati kati ya vipandio,
29 and on the panels that were between the ledges were lions, oxen, and cherubim; and on the ledges there was a pedestal above; and beneath the lions and oxen were wreaths of hanging work.
na juu ya papi na vipandio kulikuwa na simba, makisai, na makerubi. Chini na juu simba kulikuwa na masongo ya kazi ya kufuliwa.
30 Every base had four bronze wheels, and axles of bronze; and the four feet of it had supports: beneath the basin were the supports molten, with wreaths at the side of each.
Kila kalio lilikuwa na magurudumu ya shaba na vipini, na pande zake nne na miguu yake minne ilikuwa na mataruma chini ya birika. Chini ya birika yalikuweko mataruma ya kusubu yenye masongo katika kila upande.
31 The mouth of it within the capital and above was twenty-one inches: and its mouth was round after the work of a pedestal, two feet and seven inches; and also on its mouth were engravings, and their panels were foursquare, not round.
Na kinywa chake kilikuwa cha kuviringana, chenye upana wa sentimita araobaini na sita, na ile taji ilikuwa na sentimita ishirini na tatu. Na kinywa chake kilikuwa na nakshi, na papi zake zilikuwa za mraba, na wala siyo za mvringo.
32 The four wheels were underneath the panels; and the axles of the wheels were in the base: and the height of a wheel was two feet and seven inches.
Yale magurudumu mawili yalikuwa chini ya papi, na mikono ya magurudumu yalikuwa ndani ya makalio. Kimo cha yale magurudumu kilikuwa sentimeta sitini na tisa.
33 The work of the wheels was like the work of a chariot wheel: their axles, and their rims, and their spokes, and their naves, were all molten.
Yale magurudumu yalikuwa kama ya gari. Mikono yake, na maduara, matindi yake, na vipande vya ndani vyote vilikuwa vya kusubu.
34 There were four supports at the four corners of each base: its supports were of the base itself.
Kulikuwa na mataruma manne katika pande zake nne za makalio, yaliyokuwa yameshikamanishwa na kalio lenyewe.
35 In the top of the base was there a round compass ten and a quarter inches high; and on the top of the base its stays and its panels were of the same.
Juu ya makalio kulikuwa na duara yenye kina cha sentimita ishirini na tatu, na juu ya makalio mashikio yake na papi zake zikiwa zimeshikamanishwa.
36 On the plates of its stays, and on its panels, he engraved cherubim, lions, and palm trees, according to the space of each, with wreaths all around.
Juu ya mabamba na papi zake Huramu akachora makerubi, simba, na mitende ambayo ilifunika nafasi ya juu, nayo ilikuwa imezungukwa na masongo.
37 In this way, he made the ten bases: all of them had one casting, one measure, and one form.
Alitengeneza makalio kumi kwa jinsi hii. Yote yalikuwa yametengenezwa kwa kufanana, na yalikuwa ya vipimo sawa, na sura inayofanana.
38 He made ten basins of bronze: one basin contained forty baths; and every basin was six feet and eleven inches; and on every one of the ten bases one basin.
Huramu akatengeneza birika kumi za shaba. Birika moja liliweza kubeba bathi arobaini za maji. Kila birika lilikuwa mita 1. 8 toka birika moja hadi jingine na kulikuwa na birika moja katika kila kalio kati ya yale kumi.
39 He set the bases, five on the right side of the house, and five on the left side of the house: and he set the sea on the right side of the house eastward, toward the south.
Alitengeneza makalio tano upande wa kusini unaoelekea upande wa hekalu. Akatengeneza bahari katika upande wa mashariki, ukielekea upande wa kusini wa hekalu.
40 Hiram made the pots, and the shovels, and the basins. So Hiram made an end of doing all the work that he worked for king Solomon in the house of the LORD:
Huramu akatengeneza birika na koleo na besini la kunyunyizia. Kisha akamaliza kazi yote aliyofanya kwa mfalme Sulemani katika hekalu la BWANA:
41 the two pillars, and the two bowls of the capitals that were on the top of the pillars; and the two networks to cover the two bowls of the capitals that were on the top of the pillars;
Zile nguzo mbili, na lile besini lakawa kama taji ambalo lilikuwa juu ya zile nguzo, na nyavu mbili za mapambo za kufunika zile besini mbili za kuwa kama taji zilizokuwa juu ya nguzo.
42 and the four hundred pomegranates for the two networks; two rows of pomegranates for each network, to cover the two bowls of the capitals that were on the pillars;
Kisha akatengeneza makomamanga mia nne kwa ajili ya zile nyavu mbili za mapambo: safu mbili za makomamamanga kwa kila kazi ya nyavu kwa ajili ya kufunikia zile besini mbili kama taji iliyo juu ya nguzo,
43 and the ten bases, and the ten basins on the bases;
yale makalio kumi, na birika kumi kwenye makalio.
44 and one sea, and the twelve oxen under the sea;
Akatengeneza bahari na makisai kumi chini yake;
45 and the pots, and the shovels, and the basins: even all these vessels, which Hiram made for king Solomon, in the house of the LORD, were of burnished bronze.
na masufuria, koleo, birika na vyombo vingine vyote. Huramu akivitengeneza kwa shaba iliyosuguliwa, kwa ajili ya mfalme Sulemani, na kawa ajili ya hekalu la BWANA.
46 The king cast them in the plain of the Jordan, in the clay ground between Succoth and Zarethan.
Mfalme alivisubu katika uwanda wa Yorodani, katika udongo mfinyanzi kati ya Sukoti na Zarethani.
47 Solomon left all the vessels unweighed, because they were exceeding many: the weight of the bronze could not be found out.
Sulemani hakuvipima vyombo vyote kwa sababu vilikuwa vingi mno kuvipima, na kwa sababu uzito wa shaba ulikuwa hauwezi kupimwa.
48 Solomon made all the vessels that were in the house of the LORD: the golden altar, and the table whereupon the show bread was, of gold;
Sulemani akatengeneza mapambo yote yaliyokuwa kwenye hekalu la BWANA kwa kutumia dhahabu: Ile madhabahu ya dhahabu na ile meza ambayo iliwekwa mikate ya wonyesho.
49 and the lampstands, five on the right side, and five on the left, before the inner sanctuary, of pure gold; and the flowers, and the lamps, and the tongs, of gold;
Vile vinara vya dhahabu, ambavyo vitano vilikuwa upande wa kulia na vitano mkono wa kushoto, mbele ya chumba cha ndani, vilikuwa vya dhahabu safi, na maua, na taa na koleo zilikuwa za dhahabu.
50 and the cups, and the snuffers, and the basins, and the spoons, and the fire pans, of pure gold; and the hinges, both for the doors of the inner house, the most holy place, and for the doors of the house, of the temple, of gold.
Vile vikombe, na makasi, mabakuri, na vijiko, na vyetezo vyote vilikuwa vimetengenezwa kwa dhahabu safi. na bawaba za dhahabu za milango ya ndani, ambazoo ndio mahali patakatifu sana, na milango ya ukumbi mkubwa, vyote vilitengenezwa kwa dhahabu.
51 Thus all the work that Solomon performed in the house of the LORD was finished. Solomon brought in the things which David his father had dedicated, the silver, and the gold, and the vessels, and put them in the treasuries of the house of the LORD.
Kwa njia hii, kazi yote ambayo mfalme Sulemani alifanya kwa ajili ya hekalu ilimalizika. Kwa Sulemani akaviingiza ndani yake vitu vile vilivyokuwa vimewekwa wakfu na Daudi, baba yake, na fedha na dhahabu, na mapambo, na vile vya ndani ya hazina ya BWANA.

< 1 Kings 7 >