< 1 Yochanan 2 >
1 My little children, I write these things to you so that you may not sin. If anyone sins, we have an advocate with the Father, Jesus (the) Messiah, the righteous.
Watoto wangu wapendwa, nawaandikia mambo haya kwenu ili msitende dhambi. Lakini kama mmoja wenu akitenda dhambi, tunaye wakili aliye pamoja na Baba, Yesu Kristo- ambaye ni mwenye haki.
2 And he is the atoning sacrifice for our sins, and not for ours only, but also for the whole world.
Yeye ni mpatanishi kwa dhambi zetu, na si kwa dhambi zetu pekee, lakini pia kwa ulimwengu mzima.
3 This is how we know that we know him: if we keep his commandments.
Kwa hili twajua kwamba twamjua yeye, kama tukizitunza amri zake.
4 One who says, "I know him," and does not keep his commandments, is a liar, and the truth is not in him.
Yeye asemaye, “Namjua Mungu,” lakini hazishiki amri zake, ni mwongo, na kweli haimo ndani yake.
5 But whoever keeps his word, God's love has truly been perfected in him. This is how we know that we are in him:
Lakini yeyote ashikaye neno lake, kweli katika mtu yule upendo wa Mungu umekamilishwa. Katika hili twajua kwamba tuko ndani yake.
6 he who says he remains in him ought himself also to walk just like he walked.
Yeye asemaye anaishi ndani ya Mungu anapaswa mwenyewe pia kuenenda kama vile Yesu Kristo alivyoenenda.
7 Beloved, I write no new commandment to you, but an old commandment which you had from the beginning. The old commandment is the word which you heard.
Wapenzi, siwaandikii ninyi amri mpya, bali amri ya zamani ambayo mmekwisha kuwa nayo tangu mwanzo. Amri ya zamani ni neno ambalo mlilolisikia.
8 Again, I write a new commandment to you, which is true in him and in you; because the darkness is passing away, and the true light already shines.
Hata hivyo ninawaandikia ninyi amri mpya, ambayo ni kweli katika Kristo na kwenu, kwa sababu giza linapita, na nuru ya kweli iko tayari inaangaza
9 He who says he is in the light and hates his brother, is in the darkness even until now.
Yeye asemeye yuko kwenye nuru na amchukia ndugu yake yuko katika giza hata sasa.
10 He who loves his brother remains in the light, and there is no occasion for stumbling in him.
Yeye ampendaye ndugu yake anaishi katika nuru na hakuna jambo lolote liwezalo kumkwaza.
11 But he who hates his brother is in the darkness, and walks in the darkness, and does not know where he is going, because the darkness has blinded his eyes.
Lakini yeye amchukiaye ndugu yake yuko gizani na anatembea gizani; Yeye hajui wapi aendako, kwa sababu giza limeyapofusha macho yake.
12 I write to you, little children, because your sins are forgiven you for his name's sake.
Nawaandikia ninyi, watoto wapendwa, kwa sababu mmesamehewa dhambi zenu kwa ajili ya jina lake.
13 I am writing to you, fathers, because you know him who is from the beginning. I write to you, young people, because you have overcome the evil one. I write to you, little children, because you know the Father.
Nawaandikia ninyi, akina baba, kwa sababu mnamjua yeye aliye tangu mwanzo. Nawaandikia ninyi, vijana, kwa sababu mmemshinda yule mwovu. Nimewaandikia ninyi, watoto wadogo, kwa sababu mnamjua Baba.
14 I have written to you, fathers, because you know him who is from the beginning. I have written to you, young people, because you are strong, and the word of God remains in you, and you have overcome the evil one.
Nimewaandikia ninyi, akina baba, kwa sababu mnamjua yeye aliye tangu mwanzo. Nimewaandikia ninyi, vijana, kwa sababu mko imara, na neno la Mungu linakaa ndani yenu, na mmemshinda yule mwovu.
15 Do not love the world, neither the things that are in the world. If anyone loves the world, the Father's love is not in him.
Msiipende dunia wala mambo ambayo yaliyo katika dunia. Iwapo yule ataipenda dunia, upendo wa kumpenda Baba haumo ndani yake.
16 For all that is in the world, the lust of the flesh, the lust of the eyes, and the pride of life, is not the Father's, but is the world's.
Kwani kila kitu kilichomo katika dunia- tamaa ya mwili, tamaa ya macho, na kiburi cha uzima- havitokani na Baba lakini vinatokana na dunia.
17 The world is passing away with its lusts, but he who does God's will remains forever. (aiōn )
Dunia na tamaa zake zinapita. Bali yeye afanyaye mapenzi ya Mungu huyo adumu milele. (aiōn )
18 Little children, these are the end times, and as you heard that the antimessiah is coming, even now many antimessiahs have arisen. By this we know that it is the final hour.
Watoto wadogo, ni wakati wa mwisho. Kama ambavyo mmesikia kwamba mpinga kristo anakuja, hata sasa wapinga kristo wamekuja, kwa hali hii tunajua kwamba ni wakati wa mwisho.
19 They went out from us, but they did not belong to us; for if they had belonged to us, they would have continued with us. But they left, that they might be revealed that none of them belong to us.
Walikwenda zao kutoka kwetu, kwani hawakuwa wa kwetu. Kama vile wangekuwa wa kwetu wangeendelea kuwa pamoja nasi. Lakini wakati walipo kwenda zao, hicho kilionyesha hawakuwa wa kwetu.
20 But you have an anointing from the Holy One, and you know all things.
Lakini mumetiwa mafuta na yule Mtakatifu, nanyi nyote mnaijua kweli.
21 I have not written to you because you do not know the truth, but because you know it, and because no lie is of the truth.
Sikuwaandikia ninyi kwa sababu hamuijui kweli, bali kwa sababu mnaijua na kwa sababu hakuna uongo wa ile kweli
22 Who is the liar but he who denies that Jesus is the Messiah? This is the antimessiah, he who denies the Father and the Son.
Nani ni mwongo bali ni yeye anayepinga kwamba Yesu ni Kristo? Huyu mtu ni mpinga kristo, pale anapo mpinga Baba na Mwana.
23 Whoever denies the Son, the same does not have the Father. He who confesses the Son has the Father also.
Hakuna anaye mpinga Mwana akawa na Baba. Yeyote anaye mkiri Mwana anaye Baba pia.
24 As for you, let that remain in you which you heard from the beginning. If that which you heard from the beginning remains in you, you also will remain in the Son, and in the Father.
Kama kwa ajili yenu, kile mlichosikia toka mwanzo acha kiendelee kuwa ndani yenu. Kama kile mlichosikia toka mwanzo kitakaa ndani yenu, pia, mtakaa ndani ya Mwana na Baba.
25 This is the promise which he promised us, the everlasting life. (aiōnios )
Na hii ni ahadi aliyotupatia sisi: uzima wa milele. (aiōnios )
26 These things I have written to you concerning those who would lead you astray.
Nimewaandikia haya ninyi kuhusu wale ambao wangewaongoza ninyi katika upotevu.
27 As for you, the anointing which you received from him remains in you, and you do not need for anyone to teach you. But as his anointing teaches you concerning all things, and is true, and is no lie, and even as it taught you, you remain in him.
Na kwa ajili yenu, yale mafuta mliyoyapokea kutoka kwake yanakaa ndani yenu, na hamtahitaji mtu yeyote kuwafundisha. bali kama mafuta yake yanawafundisha kuhusu mambo yote na ni kweli na siyo uongo, na hata kama yameshawafundisha, kaeni ndani yake.
28 Now, little children, remain in him, that when he appears, we may have boldness, and not be ashamed before him at his coming.
Na sasa, watoto wapendwa, kaeni ndani yake, ili wakati atakapotokea, tuweze kuwa na ujasiri na siyo kujisikia aibu mbele yake katika kuja kwake.
29 If you know that he is righteous, you know that everyone also who practices righteousness is born of him.
Kama mnajua kuwa yeye ni mwenye haki, mnajua kwamba kila mmoja atendaye haki amezaliwa na yeye.