< Psalms 116 >

1 I love Jehovah, because he listens to my voice, and my cries for mercy.
Ninampenda Bwana kwa maana amesikia sauti yangu; amesikia kilio changu ili anihurumie.
2 Because he has turned his ear to me, therefore I will call on him as long as I live.
Kwa sababu amenitegea sikio lake, nitamwita siku zote za maisha yangu.
3 The cords of death surrounded me, the pains of Sheol got a hold of me. I found trouble and sorrow. (Sheol h7585)
Kamba za mauti zilinizunguka, maumivu makuu ya kuzimu yalinipata, nikalemewa na taabu na huzuni. (Sheol h7585)
4 Then I called on the name of Jehovah: "Jehovah, I beg you, deliver my soul."
Ndipo nikaliitia jina la Bwana: “Ee Bwana, niokoe!”
5 Jehovah is Gracious and righteous. Yes, our God is merciful.
Bwana ni mwenye neema na haki, Mungu wetu ni mwingi wa huruma.
6 Jehovah preserves the simple. I was brought low, and he saved me.
Bwana huwalinda wanyenyekevu, nilipokuwa katika shida kubwa, aliniokoa.
7 Return to your rest, my soul, for Jehovah has dealt bountifully with you.
Ee nafsi yangu, tulia tena, kwa kuwa Bwana amekuwa mwema kwako.
8 For you have delivered my soul from death, my eyes from tears, and my feet from falling.
Kwa kuwa wewe, Ee Bwana, umeniokoa nafsi yangu na mauti, macho yangu kutokana na machozi, miguu yangu kutokana na kujikwaa,
9 I will walk before Jehovah in the land of the living.
ili niweze kutembea mbele za Bwana, katika nchi ya walio hai.
10 I believed, therefore I said, "I am greatly afflicted."
Niliamini, kwa hiyo nilisema, “Mimi nimeteseka sana.”
11 I said in my haste, "All men are liars."
Katika taabu yangu nilisema, “Wanadamu wote ni waongo.”
12 What will I give to Jehovah for all his benefits toward me?
Nimrudishie Bwana nini kwa wema wake wote alionitendea?
13 I will take the cup of salvation, and call on the name of Jehovah.
Nitakiinua kikombe cha wokovu na kulitangaza jina la Bwana.
14 I will pay my vows to Jehovah, yes, in the presence of all his people.
Nitazitimiza nadhiri zangu kwa Bwana mbele za watu wake wote.
15 Precious in the sight of Jehovah is the death of his faithful ones.
Kifo cha watakatifu kina thamani machoni pa Bwana.
16 Jehovah, truly I am your servant. I am your servant, the son of your handmaid. You have freed me from my chains.
Ee Bwana, hakika mimi ni mtumishi wako, mimi ni mtumishi wako, mwana wa mjakazi wako; umeniweka huru toka katika minyororo yangu.
17 I will offer to you the sacrifice of thanksgiving, and will call on the name of Jehovah.
Nitakutolea dhabihu ya kukushukuru na kuliita jina la Bwana.
18 I will pay my vows to Jehovah, yes, in the presence of all his people,
Nitazitimiza nadhiri zangu kwa Bwana mbele za watu wake wote,
19 in the courts of Jehovah's house, in the midst of you, Jerusalem. Praise JAH.
katika nyua za nyumba ya Bwana, katikati yako, ee Yerusalemu. Msifuni Bwana.

< Psalms 116 >