< Psalms 113 >
1 Praise JAH. Praise, you servants of Jehovah, praise the name of Jehovah.
Msifuni Bwana. Enyi watumishi wa Bwana msifuni, lisifuni jina la Bwana.
2 Blessed be the name of Jehovah, from this time forth and forevermore.
Jina la Bwana na lisifiwe, sasa na hata milele.
3 From the rising of the sun to the going down of the same, Jehovah's name is to be praised.
Kuanzia mawio ya jua hadi machweo yake, jina la Bwana linapaswa kusifiwa.
4 Jehovah is high above all nations, his glory above the heavens.
Bwana ametukuka juu ya mataifa yote, utukufu wake juu ya mbingu.
5 Who is like Jehovah, our God, who has his seat on high,
Ni nani aliye kama Bwana Mungu wetu, Yeye ambaye ameketi juu kwenye kiti cha enzi,
6 Who stoops down to see in heaven and in the earth?
ambaye huinama atazame chini aone mbingu na nchi?
7 He raises up the poor out of the dust. Lifts up the needy from the ash heap;
Huwainua maskini kutoka mavumbini, na kuwanyanyua wahitaji kutoka kwenye jalala,
8 that he may set him with princes, even with the princes of his people.
huwaketisha pamoja na wakuu, pamoja na wakuu wa watu wake.
9 He settles the barren woman in her home, as a joyful mother of children. Praise JAH.
Humjalia mwanamke tasa kutulia nyumbani mwake, akiwa mama watoto mwenye furaha. Msifuni Bwana.