< Mark 10 >

1 He arose from there and came into the borders of Judea and beyond the Jordan. Crowds came together to him again. As he usually did, he was again teaching them.
Yesu aliondoka eneo hilo na akaenda katika mkoa wa Uyahudi na eneo la mbele ya Mto Yorodani, na makutano walimfuata tena. Aliwafundisha tena, kama ilivyokuwa kawaida yake kufanya.
2 Pharisees came to him testing him, and asked him, "Is it lawful for a man to divorce his wife?"
Na Mafarisayo walikuja kumjaribu na wakamuuliza, “Ni halali kwa mwanamume kuachana na mke wake?”
3 He answered, "What did Moses command you?"
Yesu akawajibu, “Musa aliwaamuru nini?”
4 They said, "Moses allowed a certificate of divorce to be written, and to divorce her."
Wakasema, “Musa aliruhusu kuandika cheti cha kuachana na kisha kumfukuza mwanamke.”
5 But Jesus said to them, "Because of your hardness of heart, he wrote you this commandment.
“Ni kwa sababu ya mioyo yenu migumu ndiyo maana aliwaandikia sheria hii,” Yesu aliwaambia.
6 But from the beginning of the creation, he made them male and female.
“Lakini kutoka mwanzo wa uumbaji, 'Mungu aliwaumba mwanamume na mwanamke.'
7 For this cause a man will leave his father and mother, and will join to his wife,
Kwa sababu hii mwanamume atamwacha baba yake na mama yake na ataungana na mke wake,
8 and the two will become one flesh, so that they are no longer two, but one flesh.
na hao wawili watakuwa mwili mmoja; Kwa kuwa si wawili tena, bali mwili mmoja.
9 What therefore God has joined together, let no one separate."
Kwa hiyo alichokiunganisha Mungu, mwanadamu asikitenganishe.”
10 In the house, the disciples asked him again about the same matter.
Walipokuwa ndani ya nyumba, wanafunzi wake wakamwuliza tena kuhusu hili.
11 He said to them, "Whoever divorces his wife, and marries another, commits adultery against her.
Akawaambia, “Yeyote amwachaye mke wake na kumwoa mwanamke mwingine, anafanya uzinzi dhidi yake.
12 If she herself divorces her husband, and marries another, she commits adultery."
Mwanamke naye akimwacha mme wake na kuolewa na mwanamme mwingine, anafanya uzinzi.”
13 They were bringing to him little children, that he should touch them, but the disciples rebuked them.
Nao walimletea watoto wao wadogo ili awaguse, lakini wanafunzi wakawakemea.
14 But when Jesus saw it, he was moved with indignation, and said to them, "Allow the little children to come to me. Do not forbid them, for the kingdom of God belongs to such as these.
Lakini Yesu alipotambua hilo, hakufurahishwa nalo kabisa akawaambia, “Waruhusuni watoto wadogo waje kwangu, na msiwazuie, kwa sababu walio kama hawa ufalme wa Mungu ni wao.
15 Truly I tell you, whoever will not receive the kingdom of God like a little child, he will in no way enter into it."
Ukweli nawaambia, yeyote asiyeupokea ufalme wa Mungu kama mtoto mdogo hakika hawezi kuingia katika ufalme wa Mungu.
16 And he took them in his arms, laying his hands on them, and blessed them.
Kisha akawachukua watoto mikononi mwake na akawabariki akiwawekea mikono yake juu yao.
17 As he was going out into the way, one ran to him, knelt before him, and asked him, "Good Teacher, what must I do that I may inherit everlasting life?" (aiōnios g166)
Na alipoanza safari yake mtu mmoja alimkimbilia na akapiga magoti mbele yake, akamwuliza, “Mwalimu Mwema, nifanye nini ili niweze kurithi uzima ya milele?” (aiōnios g166)
18 Jesus said to him, "Why do you call me good? No one is good except one—God.
Na Yesu akasema, “Kwa nini unaniita mwema? Hakuna aliye mwema, isipokuwa Mungu peke yake.
19 You know the commandments: 'Do not commit adultery,' 'Do not murder,' 'Do not steal,' 'Do not give false testimony,' 'Do not defraud,' 'Honor your father and mother.'"
Unazijua amri: 'Usiue, usizini, usiibe, usishuhudie uongo, usidanganye, mheshimu baba na mama yako'.”
20 And he said to him, "Teacher, I have kept all these things from my youth."
Mtu yule akasema, “Mwalimu, haya yote nimeyatii tangu nikiwa kijana.”
21 Jesus looking at him loved him, and said to him, "One thing you lack. Go, sell whatever you have, and give to the poor, and you will have treasure in heaven; and come, follow me, taking up the cross."
Yesu alimwangalia na kumpenda. Akawambia, “Unapungukiwa kitu kimoja. Unapaswa kuuza vyote ulivyo navyo na uwape masikini, na utakuwa na hazina mbinguni. Ndipo uje unifuate.”
22 But his face fell at that saying, and he went away sorrowful, for he was one who had great possessions.
Lakini alikata tamaa kwa sababu ya maelezo haya; aliondoka akiwa mwenye huzuni, kwa kuwa alikuwa na mali nyingi.
23 Jesus looked around, and said to his disciples, "How difficult it is for those who have riches to enter into the kingdom of God."
Yesu akatazama pande zote na kuwaambia wanafunzi wake, “Ni jinsi gani ilivyo vigumu kwa tajiri kuingia katika ufalme wa Mungu!
24 The disciples were amazed at his words. But Jesus answered again and said to them, "Children, how hard it is for those who trust in riches to enter the kingdom of God.
Wanafunzi walishangazwa kwa maneno haya. Lakini Yesu akawaambia tena, “Watoto, ni jinsi gani ilivyo vigumu kuingia katika ufalme wa Mungu!
25 It is easier for a camel to go through a needle's eye than for a rich person to enter into the kingdom of God."
Ni rahisi kwa ngamia kupita kwenye tundu la sindano, kuliko mtu tajiri kuingia katika ufalme wa Mungu.”
26 They were exceedingly astonished, saying to him, "Then who can be saved?"
Walishangazwa sana na wakasemezana, “Hivyo nani ataokoka”
27 Jesus, looking at them, said, "With humans it is impossible, but not with God, for all things are possible with God."
Yesu akawaangalia na kusema, “Kwa binadamu haiwezekani, lakini sio kwa Mungu. Kwa kuwa katika Mungu yote yanawezekana.”
28 Peter began to tell him, "Look, we have left everything, and have followed you."
“Petro akaanza kuzungumza naye, “Angalia tumeacha vyote na tumekufuata.”
29 Jesus said, "Truly I tell you, there is no one who has left house, or brothers, or sisters, or mother, or father, or children, or land, for my sake, and for the sake of the Good News,
Yesu akasema, “Ukweli nawaambia ninyi, hakuna aliyeacha nyumba, au kaka, au dada, au mama, au baba, au watoto, au ardhi, kwa ajili yangu, na kwa ajili ya Injili,
30 but he will receive one hundred times more now in this time, houses, brothers, sisters, mothers, children, and land, with persecutions; and in the age to come, everlasting life. (aiōn g165, aiōnios g166)
ambaye hatapokea mara mia zaidi ya sasa hapa duniani: nyumba, kaka, dada, mama, watoto, na ardhi, kwa mateso, na ulimwengu ujao, uzima wa milele. (aiōn g165, aiōnios g166)
31 But many who are first will be last; and the last first."
Lakini wengi walio wa kwanza watakuwa wa mwisho na walio wa mwisho watakuwa wa kwanza.”
32 They were on the way, going up to Jerusalem; and Jesus was going in front of them, and they were amazed; and those who followed were afraid. He again took the twelve, and began to tell them the things that were going to happen to him.
Walipokuwa njiani, kwenda Yerusalemu, Yesu alikuwa amewatangulia mbele yao. Wanafunzi walishangaa, na wale waliokuwa wanafuata nyuma waliogopa. Ndipo Yesu akawatoa pembeni tena wale kumi na wawili na akaanza kuwaambia ambacho kitamtokea hivi karibuni:
33 "Look, we are going up to Jerusalem. The Son of Man will be delivered to the chief priests and the scribes. They will condemn him to death, and will deliver him to foreigners.
“Tazama, tunakwenda mpaka Yerusalemu, na Mwana wa Adamu atafikishwa kwa makuhani wakuu na waandishi. Watamhukumu afe na watamtoa kwa watu wa Mataifa.
34 They will mock him, spit on him, scourge him, and kill him. After three days he will rise again."
Watamdhihaki, watamtemea mate, watampiga fimbo, na watamwua. Lakini baada ya siku tatu atafufuka.”
35 James and John, the sons of Zebedee, came near to him, and said to him, "Teacher, we want you to do for us whatever we will ask."
Yakobo na Yohana, wana wa Zebedayo, walikuja kwake na kusema, “Mwalimu, tunakuhitaji utufanyie chochote tukuombacho.”
36 He said to them, "What do you want me to do for you?"
Aliwaambia, “Mnataka niwatendee nini?”
37 They said to him, "Grant to us that we may sit, one at your right hand, and one at your left hand, in your glory."
Wakasema, “Turuhusu tukae nawe katika utukufu wako, mmoja katika mkono wako wa kuume na mwingine mkono wako wa kushoto.”
38 But Jesus said to them, "You do not know what you are asking. Are you able to drink the cup that I drink, or to be baptized with the baptism that I am baptized with?"
Lakini Yesu aliwajibu, “Hamjui mnachoomba. Mnaweza kukinywea kikombe ambacho nitakiywea au kustahimili ubatizo ambao nitabatizwa?”
39 And they said to him, "We are able." And Jesus said to them, "You will drink the cup I drink, and you will be baptized with the baptism that I am baptized with;
Wakamwambia, “Tunaweza” Yesu akawaambia, “Kikombe nitakachokinywea, mtakinywea. Na ubatizo ambao kwao nimebatizwa, mtaustahimili.
40 but to sit at my right hand and at my left hand is not mine to give, but for whom it has been prepared."
Lakini atakayekaa mkono wangu wa kuume au mkono wangu wa kushoto sio mimi wa kutoa, lakini ni kwa wale ambao kwao imekwisha andaliwa.”
41 When the ten heard it, they began to be indignant towards James and John.
Wale wanafunzi wengine kumi waliposikia haya, wakaanza kuwakasirikia Yakobo na Yohana.
42 Jesus summoned them, and said to them, "You know that they who are recognized as rulers over the nations lord it over them, and their great ones exercise authority over them.
Yesu akawaita kwake na kusema, “Mnajua kuwa wale wanaodhaniwa kuwa watawala wa watu wa Mataifa huwatawala, na watu wao mashuhuri huwaonyesha mamlaka juu yao.”
43 But it will not be so among you, but whoever wants to become great among you must be your servant.
Lakini haipaswi kuwa hivi kati yenu. Yeyote atakaye kuwa mkubwa kati yenu lazima awatumikie,
44 And whoever wants to be first among you must be slave of all.
na yeyote atakaye kuwa wa kwanza kati yenu ni lazima awe mtumwa wa wote.
45 For the Son of Man also did not come to be served, but to serve, and to give his life as a ransom for many."
Kwa kuwa Mwana wa Adamu hakuja kutumikiwa bali kutumika, na kuyatoa maisha yake kuwa fidia kwa wengi.”
46 They came to Jericho. As he went out from Jericho, with his disciples and a large crowd, Bartimaeus, the son of Timaeus, a blind beggar, was sitting by the road.
Wakaja Yeriko. Alipokuwa akiondoka Yeriko na wanafunzi wake na kundi kubwa, mwana wa Timayo, Batimayo, kipofu mwombaji, alikaa kando ya barabara.
47 When he heard that it was Jesus the Nazarene, he began to cry out, and say, "Jesus, Son of David, have mercy on me."
Aliposikia kuwa ni Yesu Mnazareti, alianza kupiga kelele na kusema, “Yesu, Mwana wa Daudi, nihurumie!”
48 Many rebuked him, that he should be quiet, but he shouted all the louder, "Son of David, have mercy on me."
Wengi walimkemea yule kipofu, wakimwambia anyamaze. Lakini alilia kwa sauti zaidi, “Mwana wa Daudi, nihurumie!”
49 Jesus stood still, and said, "Call him." They called the blind man, saying to him, "Cheer up. Get up. He is calling you."
Yesu alisimama na kuamuru aitwe. Walimwita yule kipofu, wakisema, “Kuwa shujaa! Inuka! Yesu anakuita.”
50 He, casting away his coat, jumped up, and came to Jesus.
Akalitupa pembeni koti lake, akakimbia zaidi, na kuja kwa Yesu.
51 Jesus asked him, "What do you want me to do for you?" The blind man said to him, "Rabboni, that I may see again."
Yesu akamjibu na kusema, “Unataka nikufanyie nini?” Yule mwanaume kipofu akamjibu, “Mwalimu, ninataka kuona.”
52 Jesus said to him, "Go your way. Your faith has made you well." And immediately he received his sight, and followed him on the road.
Yesu akamwambia, “Nenda. Imani yako imekuponya.” Hapo hapo macho yake yakaona; na akamfuata Yesu barabarani.

< Mark 10 >