< Luke 2 >

1 Now it happened in those days, that a decree went out from Caesar Augustus that the whole empire should be enrolled.
Siku zile Kaisari Augusto alitoa amri kwamba watu wote waandikishwe katika ulimwengu wa Kirumi.
2 This was the first enrollment made when Quirinius was governor of Syria.
(Orodha hii ndiyo ya kwanza iliyofanyika wakati Krenio alikuwa mtawala wa Shamu).
3 All went to enroll themselves, everyone to his own city.
Kila mtu alikwenda kuandikishwa katika mji wake alikozaliwa.
4 Joseph also went up from Galilee, out of the city of Nazareth, into Judea, to the city of David, which is called Bethlehem, because he was of the house and family of David;
Hivyo Yosefu akapanda kutoka mji wa Nazareti ulioko Galilaya kwenda Uyahudi, mpaka Bethlehemu, mji wa Daudi, kwa sababu yeye alikuwa wa ukoo na wa nyumba ya Daudi.
5 to enroll himself with Mary, who was pledged to be married to him, being pregnant.
Alikwenda huko kujiandikisha pamoja na Maria, ambaye alikuwa amemposa naye alikuwa mjamzito.
6 It happened, while they were there, that the day had come that she should give birth.
Wakiwa Bethlehemu, wakati wa Maria wa kujifungua ukawa umetimia,
7 And she gave birth to her firstborn son, and wrapped him with pieces of cloth, and placed him in a feeding trough, because there was no guest room available for them.
naye akamzaa mwanawe, kifungua mimba. Akamfunika nguo za kitoto na kumlaza katika hori ya kulia ngʼombe, kwa sababu hapakuwa na nafasi katika nyumba ya wageni.
8 There were shepherds in the same country staying in the field, and keeping watch by night over their flock.
Katika eneo lile walikuwako wachungaji waliokuwa wakikaa mashambani, wakilinda makundi yao ya kondoo usiku.
9 And look, an angel of the Lord stood by them, and the glory of the Lord shone around them, and they were terrified.
Ghafula tazama, malaika wa Bwana akawatokea, nao utukufu wa Bwana ukawangʼaria kotekote, wakaingiwa na hofu.
10 The angel said to them, "Do not be afraid, for see, I bring you good news of great joy which will be to all the people.
Lakini malaika akawaambia: “Msiogope. Kwa maana tazama nawaletea habari njema za furaha itakayokuwa kwa watu wote.
11 For there is born to you, this day, in the city of David, a Savior, who is Christ, the Lord.
Leo katika mji wa Daudi kwa ajili yenu amezaliwa Mwokozi, ndiye Kristo Bwana.
12 This is the sign to you: you will find a baby wrapped in strips of cloth, lying in a feeding trough."
Hii ndiyo itakayokuwa ishara kwenu: Mtamkuta mtoto mchanga amefunikwa nguo za kitoto na kulazwa katika hori ya kulia ngʼombe.”
13 Suddenly, there was with the angel a multitude of the heavenly army praising God, and saying,
Ghafula pakawa na jeshi kubwa la mbinguni pamoja na huyo malaika wakimsifu Mungu wakisema,
14 "Glory to God in the highest, and on earth peace, good will toward humankind."
“Atukuzwe Mungu juu mbinguni, na duniani iwe amani kwa watu aliowaridhia.”
15 And it happened that when the angels went away from them into the sky, the shepherds said one to another, "Let us go to Bethlehem, now, and see this thing that has happened, which the Lord has made known to us."
Hao malaika walipokwisha kuondoka na kwenda zao mbinguni, wale wachungaji wakasemezana wao kwa wao, “Twendeni Bethlehemu tukaone mambo haya ya ajabu yaliyotukia, ambayo Bwana ametuambia habari zake.”
16 They came with haste, and found both Mary and Joseph, and the baby was lying in the feeding trough.
Hivyo wakaenda haraka Bethlehemu, wakawakuta Maria na Yosefu na yule mtoto mchanga akiwa amelala katika hori la kulia ngʼombe.
17 When they saw it, they made known the saying which was spoken to them about this child.
Walipomwona yule mtoto, wakawaeleza yale waliyokuwa wameambiwa kuhusu huyo mtoto.
18 All who heard it wondered at the things which were spoken to them by the shepherds.
Nao wote waliosikia habari hizi wakastaajabia yale waliyoambiwa na wale wachungaji wa kondoo.
19 But Mary kept all these sayings, pondering them in her heart.
Lakini Maria akayaweka mambo haya yote moyoni mwake na kuyatafakari.
20 The shepherds returned, glorifying and praising God for all the things that they had heard and seen, just as it was told them.
Wale wachungaji wakarudi, huku wakimtukuza Mungu na kumsifu kwa ajili ya mambo yote waliyokuwa wameambiwa na kuyaona.
21 When eight days were fulfilled to circumcise him, his name was called Jesus, which was given by the angel before he was conceived in the womb.
Hata zilipotimia siku nane, ulikuwa ndio wakati wa kumtahiri mtoto, akaitwa Yesu, jina alilokuwa amepewa na malaika kabla hajatungwa mimba.
22 When the days of their purification according to the Law of Moses were fulfilled, they brought him up to Jerusalem, to present him to the Lord
Ulipotimia wakati wa utakaso wake Maria kwa mujibu wa Sheria ya Mose, basi Yosefu na Maria walimpeleka mtoto Yerusalemu, ili kumweka wakfu kwa Bwana
23 (as it is written in the Law of the Lord, "Every male who opens the womb will be called holy to the Lord"),
(kama ilivyoandikwa katika Sheria ya Bwana, kwamba, “Kila mtoto wa kiume kifungua mimba atawekwa wakfu kwa Bwana”),
24 and to offer a sacrifice according to that which is said in the Law of the Lord, "A pair of turtledoves, or two young pigeons."
na pia kutoa dhabihu kulingana na yale yaliyonenwa katika Sheria ya Bwana: “Hua wawili au makinda mawili ya njiwa.”
25 And look, there was a man in Jerusalem whose name was Simeon. This man was righteous and devout, looking for the consolation of Israel, and the Holy Spirit was on him.
Basi alikuwako huko Yerusalemu mtu mmoja jina lake Simeoni, ambaye alikuwa mwenye haki na mcha Mungu, akitarajia faraja ya Israeli, na Roho Mtakatifu alikuwa juu yake.
26 It had been revealed to him by the Holy Spirit that he should not see death before he had seen the Lord's Christ.
Roho Mtakatifu alikuwa amemfunulia kuwa hatakufa kabla hajamwona Kristo wa Bwana.
27 He came in the Spirit into the temple. When the parents brought in the child, Jesus, that they might do concerning him according to the requirement of the Law,
Simeoni, akiwa ameongozwa na Roho Mtakatifu, alikwenda Hekaluni. Wazazi walipomleta mtoto Yesu ili kumfanyia kama ilivyokuwa desturi ya Sheria,
28 then he received him into his arms, and blessed God, and said,
ndipo Simeoni akampokea mtoto mikononi mwake na kumsifu Mungu, akisema:
29 "Now you are releasing your servant, Lord, according to your word, in peace;
“Bwana Mwenyezi, kama ulivyoahidi, sasa wamruhusu mtumishi wako aende zake kwa amani.
30 for my eyes have seen your salvation,
Kwa maana macho yangu yameuona wokovu wako,
31 which you have prepared before the face of all peoples;
ulioweka tayari machoni pa watu wote,
32 a light for revelation to the nations, and the glory of your people Israel."
nuru kwa ajili ya ufunuo kwa watu wa Mataifa na kwa ajili ya utukufu kwa watu wako Israeli.”
33 And his father and his mother were marveling at the things which were spoken concerning him,
Naye Yosefu na mama yake mtoto wakastaajabu kwa yale yaliyokuwa yamesemwa kumhusu huyo mtoto.
34 and Simeon blessed them, and said to Mary, his mother, "Look, this child is set for the falling and the rising of many in Israel, and for a sign which is spoken against.
Kisha Simeoni akawabariki, akamwambia Maria mama yake, “Mtoto huyu amewekwa kwa makusudi ya kuanguka na kuinuka kwa wengi katika Israeli. Atakuwa ishara ambayo watu watanena dhidi yake,
35 Yes, a sword will pierce through your own soul, that the thoughts of many hearts may be revealed."
ili mawazo ya mioyo mingi yadhihirike. Nao upanga utauchoma moyo wako.”
36 There was one Anna, a prophetess, the daughter of Penuel, of the tribe of Asher (she was of a great age, having lived with a husband seven years from her virginity,
Tena alikuwako Hekaluni nabii mmoja mwanamke, jina lake Ana binti Fanueli, wa kabila la Asheri. Alikuwa mzee sana; naye alikuwa ameolewa na kuishi na mume kwa miaka saba tu, kisha mumewe akafa.
37 and she had been a widow for about eighty-four years), who did not depart from the temple, worshipping with fastings and petitions night and day.
Hivyo alikuwa mjane na umri wake ulikuwa miaka themanini na minne. Yeye hakuondoka humo Hekaluni usiku wala mchana, bali alikuwa akimwabudu Mungu, akifunga na kuomba.
38 Coming up at that very hour, she gave thanks to God, and spoke of him to all those who were looking for the redemption of Jerusalem.
Wakati huo huo, Ana alikuja akaanza kusifu, akimshukuru Mungu na kusema habari za huyo mtoto kwa watu wote waliokuwa wakitarajia ukombozi wa Yerusalemu.
39 When they had accomplished all things that were according to the Law of the Lord, they returned into Galilee, to their own city, Nazareth.
Yosefu na Maria walipokuwa wamekamilisha mambo yote yaliyotakiwa na Sheria ya Bwana, walirudi mjini kwao Nazareti huko Galilaya.
40 The child was growing, and was becoming strong, being filled with wisdom, and the favor of God was upon him.
Naye yule mtoto akakua na kuongezeka nguvu, akiwa amejaa hekima, na neema ya Mungu ilikuwa juu yake.
41 His parents went every year to Jerusalem at the feast of the Passover.
Kila mwaka Yosefu na Maria mama yake Yesu walikuwa na desturi ya kwenda Yerusalemu kwa ajili ya Sikukuu ya Pasaka.
42 When he was twelve years old, they went up according to the custom of the feast,
Yesu alipokuwa na umri wa miaka kumi na miwili, walipanda kwenda kwenye Sikukuu hiyo kama ilivyokuwa desturi.
43 and when they had fulfilled the days, as they were returning, the boy Jesus stayed behind in Jerusalem. His parents did not know it,
Baada ya Sikukuu kumalizika, wakati Yosefu na Maria mama yake walipokuwa wakirudi nyumbani, Yesu alibaki Yerusalemu lakini hawakutambua.
44 but supposing him to be in the company, they went a day's journey, and they looked for him among their relatives and acquaintances.
Wao wakidhani kuwa yuko miongoni mwa wasafiri, walienda mwendo wa kutwa nzima. Ndipo wakaanza kumtafuta miongoni mwa jamaa zao na marafiki.
45 When they did not find him, they returned to Jerusalem, looking for him.
Walipomkosa walirudi Yerusalemu ili kumtafuta.
46 It happened after three days they found him in the temple, sitting in the midst of the teachers, both listening to them, and asking them questions.
Baada ya siku tatu wakamkuta ndani ya Hekalu, akiwa ameketi katikati ya walimu wa sheria, akiwasikiliza na kuwauliza maswali.
47 All who heard him were amazed at his understanding and his answers.
Wote waliomsikia walistaajabishwa na uwezo wake mkubwa wa kuelewa, na majibu aliyoyatoa.
48 When they saw him, they were astonished, and his mother said to him, "Son, why have you treated us this way? Look, your father and I were anxiously looking for you."
Yosefu na Maria mama yake walipomwona walishangaa. Mama yake akamuuliza, “Mwanangu, mbona umetufanyia hivi? Tazama, mimi na baba yako tumekuwa tukikutafuta kwa wasiwasi mkubwa kila mahali.”
49 He said to them, "Why were you looking for me? Did you not know that I must be doing the works of my Father?"
Yesu akawaambia, “Kwa nini kunitafuta? Hamkujua kwamba imenipasa kuwa katika nyumba ya Baba yangu?”
50 They did not understand the saying which he spoke to them.
Lakini wao hawakuelewa maana ya lile alilowaambia.
51 And he went down with them, and came to Nazareth. He was subject to them, and his mother kept all these sayings in her heart.
Ndipo akashuka pamoja nao hadi Nazareti, naye alikuwa mtiifu kwao. Lakini mama yake akayaweka moyoni mwake mambo haya yote.
52 And Jesus increased in wisdom and stature, and in favor with God and people.
Naye Yesu akakua katika hekima na kimo, akimpendeza Mungu na wanadamu.

< Luke 2 >