< Ephesians 6 >
1 Children, obey your parents in the Lord, for this is right.
Enyi watoto, watiini wazazi wenu Kikristo maana hili ni jambo jema.
2 "Honor your father and mother," which is the first commandment with a promise:
“Waheshimu Baba na mama yako,” hii ndiyo amri ya kwanza ambayo imeongezewa ahadi, yaani,
3 "that it may be well with you, and that you may live long in the land."
“Upate fanaka na miaka mingi duniani.”
4 And fathers, do not provoke your children to anger, but nurture them in the discipline and instruction of the Lord.
Nanyi akina baba, msiwachukize watoto wenu ila waleeni katika nidhamu na mafundisho ya Kikristo.
5 Servants, be obedient to those who according to the flesh are your masters, with fear and trembling, in singleness of your heart, as to Christ;
Enyi watumwa, watiini mabwana zenu hapa duniani kwa hofu na tetemeko; fanyeni hivyo kwa unyofu wa moyo kana kwamba mnamtumikia Kristo.
6 not in the way of service only when eyes are on you, as people-pleasers; but as servants of Christ, doing the will of God from the heart;
Fanyeni hivyo si tu wakati wanapowatazama ili mjipendekeze kwao, bali tumikieni kwa moyo kama atakavyo Mungu kwa sababu ninyi ni watumishi wa Kristo.
7 with good will doing service, as to the Lord, and not to people;
Muwe radhi kutumikia kwa ajili ya Bwana na si kwa ajili ya watu.
8 knowing that whatever good thing each one does, he will receive the same again from the Lord, whether he is bound or free.
Kumbukeni kwamba kila mtu mwenye kutenda mema, awe mtumwa au mtu huru, atapokea tuzo lake kutoka kwa Bwana.
9 You masters, do the same things to them, and give up threatening, knowing that he who is both their Master and yours is in heaven, and there is no partiality with him.
Nanyi mnaotumikiwa, watendeeni vivyo hivyo watumwa wenu, na acheni kutumia vitisho. Kumbukeni kwamba ninyi pia kama vile wao, mnaye Bwana yuleyule mbinguni, kwake cheo cha mtu si kitu.
10 Finally, be strong in the Lord, and in the strength of his might.
Hatimaye, nawatakeni muwe imara katika kuungana na Bwana na kwa msaada wa nguvu yake kuu.
11 Put on the whole armor of God, that you may be able to stand against the schemes of the devil.
Vaeni silaha anazowapeni Mungu mpate kuzipinga mbinu mbaya za Ibilisi.
12 For our wrestling is not against flesh and blood, but against the rulers, against the powers, against the world's rulers of this darkness, and against the spiritual forces of wickedness in the heavenly places. (aiōn )
Maana vita vyenu si vita kati yetu na binadamu, bali ni vita dhidi ya jeshi ovu la ulimwengu wa roho; tunapigana na watawala, wakuu na wenye nguvu wanaomiliki ulimwengu huu wa giza. (aiōn )
13 Therefore, put on the whole armor of God, that you may be able to withstand in the evil day, and, having done all, to stand.
Kwa sababu hiyo, vaeni silaha za Mungu ili siku ile itakapofika muweze kuyapinga mashambulio ya adui; na mkisha pigana mpaka mwisho, muwe bado thabiti.
14 Stand therefore, having the belt of truth buckled around your waist, and having put on the breastplate of righteousness,
Basi, simameni imara! Ukweli uwe kama ukanda kiunoni mwenu, uadilifu uwe kama vazi la kujikinga kifuani,
15 and having fitted your feet with the preparation of the Good News of peace;
na hamu ya kutangaza Habari Njema ya amani iwe kama viatu miguuni mwenu.
16 above all, taking up the shield of faith, with which you will be able to quench all the fiery darts of the evil one.
Zaidi ya hayo yote, imani iwe daima kama ngao mikononi mwenu, iwawezeshe kuizima mishale ya moto ya yule Mwovu.
17 And take the helmet of salvation, and the sword of the Spirit, which is the spoken word of God;
Upokeeni wokovu kama kofia yenu ya chuma, na neno la Mungu kama upanga mnaopewa na Roho Mtakatifu.
18 with all prayer and requests, praying at all times in the Spirit, and being watchful to this end in all perseverance and requests for all the saints:
Salini daima, mkiomba msaada wa Mungu. Salini kila wakati kwa nguvu ya Roho. Kesheni bila kuchoka mkisali kwa ajili ya watu wote wa Mungu.
19 on my behalf, that utterance may be given to me in opening my mouth, to make known with boldness the mystery of the Good News,
Niombeeni nami pia ili niongeapo Mungu anijalie cha kusema, niweze kuwajulisha watu fumbo la Habari Njema kwa uthabiti.
20 for which I am an ambassador in chains; that in it I may speak boldly, as I ought to speak.
Mimi ni balozi kwa ajili ya Habari Njema hiyo ingawa sasa niko kifungoni. Ombeni, basi, ili niweze kuwa hodari katika kuitangaza kama inipasavyo.
21 But that you also may know my affairs, how I am doing, Tychicus, the beloved brother and faithful servant in the Lord, will make known to you all things;
Tukiko, ndugu yetu mpenzi na mtumishi mwaminifu wa Bwana, atawapeni habari zangu zote mpate kujua ninachofanya.
22 whom I have sent to you for this very purpose, that you may know our state, and that he may comfort your hearts.
Namtuma kwenu awapeni habari zetu mpate kuwa na moyo.
23 Peace be to the brothers, and love with faith, from God the Father and the Lord Jesus Christ.
Ninawatakieni ninyi ndugu amani, upendo na imani kutoka kwa Mungu Baba na kutoka kwa Bwana Yesu Kristo.
24 Grace be with all those who love our Lord Jesus Christ with incorruptible love.
Nawatakia neema ya Mungu wote wanaompenda Bwana wetu Yesu Kristo kwa mapendo yasiyo na mwisho.