< Colossians 3 >

1 If then you were raised together with Christ, seek the things that are above, where Christ is, seated on the right hand of God.
Basi, ikiwa mmefufuka pamoja na Kristo, panieni mambo ya juu, kule Kristo aliko, ameketi upande wa kulia wa Mungu.
2 Set your mind on the things that are above, not on the things that are on the earth.
Muwe na hamu ya mambo ya huko juu, na siyo mambo ya hapa duniani.
3 For you died, and your life is hidden with Christ in God.
Maana ninyi mmekufa na uzima wenu umefichwa pamoja na Kristo katika Mungu.
4 When Christ, your life, is revealed, then you will also be revealed with him in glory.
Uzima wenu halisi ni Kristo, na wakati atakapotokea ndipo nanyi pia mtakapotokea pamoja naye katika utukufu.
5 Put to death, therefore, whatever is worldly in you: sexual immorality, impurity, lust, evil desire, and covetousness, which is idolatry.
Basi, komesheni kabisa kila kitu kilicho ndani yenu ambacho chahusika na mambo ya kidunia: uasherati, uchafu, shauku, tamaa mbaya na uchu (ambao ni sawa na kuabudu sanamu).
6 Because of these, the wrath of God is coming on the children of disobedience.
Kwa sababu ya mambo hayo hasira ya Mungu huwajia wote wanaomwasi.
7 You also once walked in those, when you lived in them;
Wakati mmoja ninyi pia mliishi kufuatana na mambo hayo, mlipotawaliwa nayo.
8 but now you also put them all away: anger, wrath, malice, slander, and shameful speaking out of your mouth.
Lakini sasa mnapaswa kuachana na mambo haya yote: hasira, tamaa, uovu; kufuru au maneno yasiyofaa yasitoke kamwe vinywani mwenu.
9 Do not lie to one another, seeing that you have put off the old self with its practices,
Msiambiane uongo, kwani ninyi mmekwisha vua ule utu wa kale pamoja na matendo yake yote,
10 and have put on the new self, who is being renewed in knowledge after the image of his Creator,
mkavaa utu mpya. Huu unaendelea kurekebishwa na Mungu, Muumba wake, kadiri ya mfano wake, ili mpate kumjua Mungu kwa ukamilifu.
11 where there cannot be Greek and Jew, circumcision and uncircumcision, barbarian, Scythian, slave, freeman; but Christ is all, and in all.
Katika hali hii, hakuna tena tofauti kati ya Mgiriki na Myahudi, aliyetahiriwa na asiyetahiriwa, msomi na asiye msomi, mtumwa na mtu aliye huru. Kristo ni kila kitu, na yumo katika yote.
12 Put on therefore, as God's chosen ones, holy and beloved, a heart of compassion, kindness, gentleness, humility, and patience;
Ninyi ni watu wake Mungu; yeye aliwapenda na kuwateua. Kwa hiyo basi, vaeni moyo wa huruma, wema, unyenyekevu, upole na uvumilivu.
13 bearing with one another, and forgiving each other, if anyone has a complaint against another; even as the Lord forgave you, so you also do.
Vumilianeni na kusameheana iwapo mmoja wenu analo jambo lolote dhidi ya mwenzake. Mnapaswa kusameheana kama Bwana alivyowasamehe ninyi.
14 Above all these things, walk in love, which is the bond of perfection.
Zaidi ya hayo yote, zingatieni upendo kwani upendo huunganisha kila kitu katika umoja ulio kamili.
15 And let the peace of Christ rule in your hearts, to which also you were called in one body; and be thankful.
Nayo amani ya Kristo itawale mioyoni mwenu; maana kwa ajili hiyo ninyi mmeitwa katika mwili huo mmoja. Tena muwe na shukrani!
16 Let the word of Christ dwell in you richly; in all wisdom teaching and admonishing one another with psalms, hymns, and spiritual songs, singing with grace in your heart to God.
Ujumbe wa Kristo ukae ndani yenu pamoja na utajiri wake wote. Fundishaneni na kushauriana kwa hekima yote. Imbeni zaburi, nyimbo na tenzi za kiroho; mwimbieni Mungu mioyoni mwenu kwa shukrani.
17 Whatever you do, in word or in deed, do all in the name of the Lord Jesus, giving thanks to God the Father, through him.
Na, kila mfanyacho kwa neno au tendo, fanyeni vyote kwa jina la Bwana Yesu na kumshukuru Mungu Baba kwa njia yake.
18 Wives, be in subjection to your husbands, as is fitting in the Lord.
Enyi akina mama, watiini waume zenu, kwani ndivyo apendavyo Bwana.
19 Husbands, love your wives, and do not be bitter against them.
Nanyi waume, wapendeni wake zenu, na msiwe wakali kwao.
20 Children, obey your parents in all things, for this pleases the Lord.
Enyi watoto, watiini wazazi wenu daima maana hiyo humpendeza Bwana.
21 Fathers, do not provoke your children, so that they won't be discouraged.
Nanyi wazazi, msiwachukize watoto wenu, la sivyo watakata tamaa.
22 Servants, obey in all things those who are your masters according to the flesh, not just when they are looking, as people-pleasers, but in singleness of heart, fearing the Lord.
Enyi watumwa, watiini wakuu wenu wa kidunia katika mambo yote, na si tu wakati wanapowatazama kwa kuwa mnataka kujipendekeza kwao; ila fanyeni hivyo kwa moyo wote, kwa sababu ya kumcha Bwana.
23 And whatever you do, work heartily, as for the Lord, and not for people,
Kila mfanyalo, fanyeni kwa moyo wote, kwa sababu ya Bwana na si kwa ajili ya mtu.
24 knowing that from the Lord you will receive the reward of the inheritance; for you serve the Lord Christ.
Kumbukeni kwamba atawapeni tuzo lile alilowawekea watu wake. Mtumikieni Kristo Bwana!
25 But he who does wrong will receive again for the wrong that he has done, and there is no partiality.
Atendaye mabaya atalipwa kufuatana na ubaya wake; Mungu hana ubaguzi.

< Colossians 3 >