< 1 Corinthians 10 >
1 Now I would not have you ignorant, brothers, that our fathers were all under the cloud, and all passed through the sea;
Ndugu zangu, sitaki mkose kufahamu ukweli huu kwamba baba zetu walikuwa wote chini ya wingu na kwamba wote walipita katikati ya bahari.
2 and were all baptized into Moses in the cloud and in the sea;
Wote wakabatizwa kuwa wa Mose ndani ya lile wingu na ndani ya ile bahari.
3 and all ate the same spiritual food;
Wote walikula chakula kile kile cha roho,
4 and all drank the same spiritual drink. For they drank of a spiritual rock that followed them, and the rock was Christ.
na wote wakanywa kile kile kinywaji cha roho, kwa maana walikunywa kutoka ule mwamba wa roho uliofuatana nao, nao ule mwamba ulikuwa Kristo.
5 However with most of them, God was not well pleased, for they were overthrown in the wilderness.
Lakini Mungu hakupendezwa na wengi wao, kwa hiyo miili yao ilitapakaa jangwani.
6 Now these things were our examples, to the intent we should not lust after evil things, as they also lusted.
Basi mambo haya yalitokea kama mifano ili kutuzuia tusiweke mioyo yetu katika mambo maovu kama wao walivyofanya.
7 Neither be idolaters, as some of them were. As it is written, "The people sat down to eat and drink, and rose up to play."
Msiwe waabudu sanamu, kama baadhi yao walivyokuwa, kama ilivyoandikwa, “Watu waliketi chini kula na kunywa, kisha wakainuka kucheza na kufanya sherehe za kipagani.”
8 Neither let us commit sexual immorality, as some of them committed, and in one day twenty-three thousand fell.
Wala tusifanye uzinzi kama baadhi yao walivyofanya, wakafa watu 23,000 kwa siku moja.
9 Neither let us test the Christ, as some of them tested, and perished by the serpents.
Wala tusimjaribu Kristo, kama baadhi yao walivyofanya, wakafa kwa kuumwa na nyoka.
10 Neither grumble, as some of them also grumbled, and perished by the destroyer.
Msinungʼunike kama baadhi yao walivyofanya, wakaangamizwa na mharabu.
11 Now these things happened to them by way of example, and they were written for our admonition, on whom the ends of the ages have come. (aiōn )
Mambo haya yote yaliwapata wao ili yawe mifano kwa wengine, nayo yaliandikwa ili yatuonye sisi ambao mwisho wa nyakati umetufikia. (aiōn )
12 Therefore let him who thinks he stands be careful that he does not fall.
Hivyo, yeye ajidhaniaye amesimama, aangalie asianguke.
13 No temptation has taken you except what is common to humanity. God is faithful, who will not allow you to be tempted above what you are able, but will with the temptation also make the way of escape, that you may be able to endure it.
Hakuna jaribu lolote lililowapata ambalo si la kawaida kwa wanadamu. Naye Mungu ni mwaminifu; hataruhusu mjaribiwe kupita mnavyoweza. Lakini mnapojaribiwa atawapa njia ya kutokea ili mweze kustahimili.
14 Therefore, my beloved, flee from idolatry.
Kwa hiyo wapenzi wangu, zikimbieni ibada za sanamu.
15 I speak as to wise people. Judge what I say.
Nasema watu wenye ufahamu, amueni wenyewe kuhusu haya niyasemayo.
16 The cup of blessing which we bless, is it not a sharing of the blood of Christ? The bread which we break, is it not a sharing of the body of Christ?
Je, kikombe cha baraka ambacho tunakibariki, si ushirika katika damu ya Kristo? Mkate tuumegao, si ushirika wa mwili wa Kristo?
17 Because there is one loaf of bread, we, who are many, are one body; for we all partake of the one loaf of bread.
Kwa kuwa mkate ni mmoja, sisi tulio wengi tu mwili mmoja, kwa kuwa wote twashiriki mkate mmoja.
18 Consider Israel according to the flesh. Do not those who eat the sacrifices participate in the altar?
Waangalieni watu wa Israeli: Je, wale wote walao dhabihu si ni wale watendao kazi madhabahuni?
19 What am I saying then? That a thing sacrificed to idols is anything, or that an idol is anything?
Je, nina maana kwamba kafara iliyotolewa kwa sanamu ni kitu chenye maana yoyote? Au kwamba sanamu ni kitu chenye maana yoyote?
20 But I say that the things which pagans sacrifice, they sacrifice to demons, and not to God, and I do not desire that you would have fellowship with demons.
La hasha! Lakini kafara za watu wasiomjua Mungu hutolewa kwa mashetani, wala si kwa Mungu. Nami sitaki ninyi mwe na ushirika na mashetani.
21 You cannot both drink the cup of the Lord and the cup of demons. You cannot both partake of the table of the Lord, and of the table of demons.
Hamwezi kunywa katika kikombe cha Bwana na cha mashetani pia. Hamwezi kuwa na sehemu katika meza ya Bwana na katika meza ya mashetani pia.
22 Or do we provoke the Lord to jealousy? Are we stronger than he?
Je, tunataka kuamsha wivu wa Bwana? Je, sisi tuna nguvu kuliko yeye?
23 "All things are lawful," but not all things are profitable. "All things are lawful," but not all things build up.
“Vitu vyote ni halali,” lakini si vitu vyote vilivyo na faida. “Vitu vyote ni halali,” lakini si vyote vinavyojenga.
24 Let no one seek his own, but his neighbor's good.
Mtu yeyote asitafute yaliyo yake mwenyewe, bali kila mtu atafute yale yanayowafaa wengine.
25 Whatever is sold in the butcher shop, eat, asking no question for the sake of conscience,
Kuleni chochote kinachouzwa sokoni, bila kuuliza swali lolote kwa ajili ya dhamiri.
26 for "the earth is the Lord's, and its fullness."
Kwa maana, “Dunia na vyote vilivyomo ni mali ya Bwana.”
27 But if one of those who do not believe invites you to a meal, and you are inclined to go, eat whatever is set before you, asking no questions for the sake of conscience.
Kama ukikaribishwa chakula na mtu asiyeamini nawe ukikubali kwenda, kula kila kitu kitakachowekwa mbele yako bila kuuliza maswali kwa ajili ya dhamiri.
28 But if anyone says to you, "This was offered to idols," do not eat it for the sake of the one who told you, and for the sake of conscience.
Lakini kama mtu yeyote akikuambia, “Hiki kimetolewa kafara kwa sanamu,” basi usikile kwa ajili ya huyo aliyekuambia na kwa ajili ya dhamiri.
29 Conscience, I say, not your own, but the other's conscience. For why is my liberty judged by another conscience?
Nina maana dhamiri ya huyo aliyekuambia, wala si kwa ajili ya dhamiri yako. Lakini kwa nini uhuru wangu uhukumiwe na dhamiri ya mtu mwingine?
30 If I partake with thankfulness, why am I denounced for that for which I give thanks?
Kama nikila kwa shukrani, kwa nini nashutumiwa kwa kile ambacho kwa hicho ninamshukuru Mungu?
31 Whether therefore you eat, or drink, or whatever you do, do all to the glory of God.
Basi, lolote mfanyalo, kama ni kula au kunywa, fanyeni yote kwa utukufu wa Mungu.
32 Give no occasions for stumbling, either to Jews, or to Greeks, or to the church of God;
Msiwe kikwazo kwa mtu yeyote, wawe Wayahudi au Wayunani, au kwa kanisa la Mungu,
33 even as I also please all people in all things, not seeking my own profit, but the profit of the many, that they may be saved.
kama hata mimi ninavyojaribu kumpendeza kila mtu kwa kila namna. Kwa maana sitafuti mema kwa ajili yangu mwenyewe bali kwa ajili ya wengi, ili waweze kuokolewa.