< John 4 >

1 Therefore when Yeshua knew that the Pharisees had heard, "Yeshua is making and baptizing more disciples than Yukhanan"
Mafarisayo walisikia kwamba Yesu alikuwa anabatiza na kuwapata wanafunzi wengi kuliko Yohane.
2 (although Yeshua himself did not baptize, but his disciples),
(Lakini ukweli ni kwamba Yesu hakuwa anabatiza ila wanafunzi wake.)
3 he left Yehuda, and departed again into Galila.
Basi, Yesu aliposikia hayo, alitoka Yudea akarudi Galilaya;
4 He needed to pass through Samaria.
na katika safari hiyo ilimbidi apitie Samaria.
5 So he came to a city of Samaria, called Shekar, near the parcel of ground that Yaquv gave to his son, Yauseph.
Basi, akafika Sukari, mji mmoja wa Samaria, karibu na shamba ambalo Yakobo alikuwa amempa mwanawe, Yosefu.
6 Yaquv's well was there. Yeshua therefore, being tired from his journey, sat down by the well. It was about the sixth hour.
Mahali hapo palikuwa na kisima cha Yakobo, naye Yesu, kutokana na uchovu wa safari, akaketi kando ya kisima. Ilikuwa yapata saa sita mchana.
7 A woman of Samaria came to draw water. Yeshua said to her, "Give me a drink."
Basi, mwanamke mmoja Msamaria akafika kuteka maji. Yesu akamwambia, “Nipatie maji ninywe.”
8 For his disciples had gone away into the city to buy food.
(Wakati huo wanafunzi wake walikuwa wamekwenda mjini kununua chakula.)
9 The Samaritan woman therefore said to him, "How can you, being a Jew, ask for a drink from me, a Samaritan woman?" (For Jews have no dealings with Samaritans.)
Lakini huyo mwanamke akamwambia, “Wewe ni Myahudi; mimi ni mwanamke Msamaria! Unawezaje kuniomba maji?” (Wayahudi hawakuwa na ushirikiano na Wasamaria katika matumizi ya vitu.)
10 Yeshua answered her, "If you knew the gift of God, and who it is who says to you, 'Give me a drink,' you would have asked him, and he would have given you living water."
Yesu akamjibu, “Kama tu ungalijua zawadi ya Mungu na ni nani anayekwambia: Nipatie maji ninywe, ungalikwisha mwomba, naye angekupa maji yaliyo hai.”
11 The woman said to him, "Sir, you have nothing to draw with, and the well is deep. From where do you get that living water?
Huyo mama akasema, “Mheshimiwa, wewe huna chombo cha kutekea maji, nacho kisima ni kirefu; utapata wapi maji yaliyo hai?
12 Are you greater than our father, Yaquv, who gave us the well, and drank of it himself, as did his children, and his livestock?"
Au, labda wewe wajifanya mkuu kuliko babu yetu Yakobo? Yeye alitupa sisi kisima hiki; na yeye mwenyewe, watoto wake na mifugo yake walikunywa maji ya kisima hiki.”
13 Yeshua answered her, "Everyone who drinks of this water will thirst again,
Yesu akamjibu, “Kila anayekunywa maji haya ataona kiu tena.
14 but whoever drinks of the water that I will give him will never thirst again; but the water that I will give him will become in him a well of water springing up to everlasting life." (aiōn g165, aiōnios g166)
Lakini atakayekunywa maji nitakayompa mimi, hataona kiu milele. Maji nitakayompa yatakuwa ndani yake chemchemi ya maji ya uzima na kumpatia uzima wa milele.” (aiōn g165, aiōnios g166)
15 The woman said to him, "Sir, give me this water, so that I do not get thirsty, neither come all the way here to draw."
Huyo mwanamke akamwambia, “Mheshimiwa, nipe maji hayo ili nisione kiu tena; nisije tena mpaka hapa kuteka maji.”
16 He said to her, "Go, call your husband, and come here."
Yesu akamwambia, “Nenda ukamwite mumeo uje naye hapa.”
17 The woman answered and said to him, "I have no husband." Yeshua said to her, "You said well, 'I have no husband,'
Huyo mwanamke akamwambia, “Mimi sina mume.” Yesu akamwambia, “Umesema kweli, kwamba huna mume.
18 for you have had five husbands; and he whom you now have is not your husband. This you have said truly."
Maana umekuwa na waume watano, na huyo unayeishi naye sasa si mume wako. Hapo umesema kweli.”
19 The woman said to him, "Sir, I perceive that you are a prophet.
Huyo Mwanamke akamwambia, “Mheshimiwa, naona ya kuwa wewe u nabii.
20 Our fathers worshiped in this mountain, and you say that in Urishlim is the place where people ought to worship."
Babu zetu waliabudu juu ya mlima huu, lakini ninyi mwasema kwamba mahali pa kumwabudu Mungu ni kule Yerusalemu.”
21 Yeshua said to her, "Woman, believe me, the hour comes, when neither in this mountain, nor in Urishlim, will you worship the Father.
Yesu akamwambia, “Niamini; wakati unakuja ambapo hamtamwabudu Baba juu ya mlima huu, wala kule Yerusalemu.
22 You worship that which you do not know. We worship that which we know; for salvation is from the Jews.
Ninyi Wasamaria mnamwabudu yule msiyemjua, lakini sisi tunamjua huyo tunayemwabudu, kwa maana wokovu unatoka kwa Wayahudi.
23 But the hour comes, and now is, when the true worshippers will worship the Father in spirit and truth, for the Father seeks such to be his worshippers.
Lakini wakati unakuja, tena umekwisha fika, ambapo wanaoabudu kweli, watamwabudu Baba kwa nguvu ya Roho; watu wanaomwabudu hivyo ndio Baba anaotaka.
24 God is spirit, and those who worship him must worship in spirit and truth."
Mungu ni Roho, na watu wataweza tu kumwabudu kweli kwa nguvu ya Roho wake.”
25 The woman said to him, "I know that Meshikha comes," (he who is called Meshikha). "When he has come, he will declare to us all things."
Huyo mama akamwambia, “Najua kwamba Masiha, aitwaye Kristo, anakuja. Atakapokuja atatujulisha kila kitu.”
26 Yeshua said to her, "I am he, the one who speaks to you."
Yesu akamwambia, “Mimi ninayesema nawe, ndiye.”
27 At this, his disciples came. They were surprised that he was speaking with a woman; yet no one said, "What are you looking for?" or, "Why do you speak with her?"
Hapo wanafunzi wake wakarudi, wakastaajabu sana kuona anaongea na mwanamke. Lakini hakuna mtu aliyesema: “Unataka nini?” au, “Kwa nini unaongea na mwanamke?”
28 So the woman left her water pot, and went away into the city, and said to the people,
Huyo mama akauacha mtungi wake pale, akaenda mjini na kuwaambia watu,
29 "Come, see a man who told me everything that I did. Can this be the Meshikha?"
“Njoni mkamwone mtu aliyeniambia mambo yote niliyotenda! Je, yawezekana kuwa yeye ndiye Kristo?”
30 They went out of the city, and were coming to him.
Watu wakatoka mjini, wakamwendea Yesu.
31 In the meanwhile, the disciples urged him, saying, "Rabbi, eat."
Wakati huohuo wanafunzi wake walikuwa wanamsihi Yesu: “Mwalimu, ule chakula.”
32 But he said to them, "I have food to eat that you do not know about."
Lakini Yesu akawaambia, “Mimi ninacho chakula msichokijua ninyi.”
33 The disciples therefore said one to another, "Has anyone brought him something to eat?"
Wanafunzi wake wakaulizana, “Je, kuna mtu aliyemletea chakula?”
34 Yeshua said to them, "My food is to do the will of him who sent me, and to accomplish his work.
Yesu akawaambia, “Chakula changu ni kufanya anachotaka yule aliyenituma na kuitimiza kazi yake.
35 Do you not say, 'There are yet four months until the harvest?' Look, I tell you, lift up your eyes and see the fields, that they are white for harvest already.
Ninyi mwasema: Bado miezi minne tu, na wakati wa mavuno utafika! Lakini mimi nawaambieni, yatazameni mashamba; mazao yako tayari kuvunwa.
36 He who reaps receives wages, and gathers fruit to everlasting life; that both he who sows and he who reaps may rejoice together. (aiōnios g166)
Mvunaji anapata mshahara wake, na anakusanya mavuno kwa ajili ya uzima wa milele; hivyo mpandaji na mvunaji watafurahi pamoja. (aiōnios g166)
37 For in this the saying is true, 'One sows, and another reaps.'
Kwa sababu hiyo msemo huu ni kweli: Mmoja hupanda na mwingine huvuna.
38 I sent you to reap that for which you have not labored. Others have labored, and you have entered into their labor."
Mimi nimewatuma mkavune mavuno ambayo hamkuyatolea jasho, wengine walifanya kazi, lakini ninyi mnafaidika kutokana na jasho lao.”
39 From that city many of the Samaritans believed in him because of the word of the woman, who testified, "He told me everything that I did."
Wasamaria wengi wa kijiji kile waliamini kwa sababu ya maneno aliyosema huyo mama: “Ameniambia mambo yote niliyofanya.”
40 So when the Samaritans came to him, they asked him to stay with them. He stayed there two days.
Wasamaria walimwendea Yesu wakamwomba akae nao; naye akakaa hapo siku mbili.
41 Many more believed because of his word.
Watu wengi zaidi walimwamini kwa sababu ya ujumbe wake.
42 They said to the woman, "Now we believe, not because of your speaking; for we have heard for ourselves, and know that this is indeed the Savior of the world."
Wakamwambia yule mama, “Sisi hatuamini tu kwa sababu ya maneno yako; sisi wenyewe tumesikia, na tunajua kwamba huyu ndiye kweli Mwokozi wa ulimwengu.”
43 After the two days he departed from there to Galila.
Baada ya siku mbili Yesu aliondoka hapo, akaenda Galilaya.
44 For Yeshua himself testified that a prophet has no honor in his own country.
Maana Yesu mwenyewe alisema waziwazi kwamba, “Nabii hapati heshima katika nchi yake.”
45 So when he came into Galila, the Galilaye received him, having seen all the things that he did in Urishlim at the feast, for they also went to the feast.
Basi, alipofika Galilaya, Wagalilaya wengi walimkaribisha. Maana nao pia walikuwa kwenye sikukuu ya Pasaka, wakayaona mambo yote Yesu aliyotenda huko Yerusalemu wakati wa sikukuu hiyo.
46 Yeshua came therefore again to Qatne of Galila, where he made the water into wine. There was a certain nobleman whose son was sick at Kepharnakhum.
Yesu alifika tena huko mjini Kana, mkoani Galilaya, mahali alipogeuza maji kuwa divai. Kulikuwa na ofisa mmoja aliyekuwa na mtoto mgonjwa huko Kafarnaumu.
47 When he heard that Yeshua had come out of Yehuda into Galila, he went to him, and pleaded with him that he would come down and heal his son, for he was close to death.
Basi, huyo ofisa aliposikia kuwa Yesu alikuwa ametoka Yudea na kufika Galilaya, alimwendea akamwomba aende kumponya mtoto wake aliyekuwa mgonjwa mahututi.
48 Yeshua therefore said to him, "Unless you see signs and wonders, you will in no way believe."
Yesu akamwambia, “Msipoona ishara na maajabu hamtaamini!”
49 The nobleman said to him, "Sir, come down before my child dies."
Huyo ofisa akamwambia, “Mheshimiwa, tafadhali twende kabla mwanangu hajafa.”
50 Yeshua said to him, "Go your way. Your son lives." The man believed the word that Yeshua spoke to him, and he went his way.
Yesu akamwambia, “Nenda tu, mwanao yu mzima.” Huyo mtu akaamini maneno ya Yesu, akaenda zake.
51 As he was now going down, his servants met him, saying that his son was alive.
Alipokuwa bado njiani, watumishi wake walikutana naye, wakamwambia kwamba mwanawe alikuwa mzima.
52 So he inquired of them the hour when he began to get better. They said therefore to him, "Yesterday at one in the afternoon, the fever left him."
Naye akawauliza saa mtoto alipopata nafuu; nao wakamwambia, “Jana saa saba mchana, homa ilimwacha.”
53 So the father knew that it was at that hour in which Yeshua said to him, "Your son lives." He believed, as did his whole house.
Huyo baba akakumbuka kwamba ilikuwa ni saa ileile ambapo Yesu alimwambia: “Mwanao yu mzima.” Basi, yeye akaamini pamoja na jamaa yake yote.
54 This is again the second sign that Yeshua did, having come out of Yehuda into Galila.
Hii ilikuwa ishara ya pili aliyoifanya Yesu alipokuwa anatoka Yudea kwenda Galilaya.

< John 4 >