< Revelation 6 >

1 And I saw, when the Lamb opened one of the seven seals, and I heard one of the four Living Creatures say, with a voice like thunder, "Come!"
Kisha nikaangalia wakati Mwana-Kondoo akivunja ile lakiri ya kwanza miongoni mwa zile saba. Ndipo nikasikia mmoja wa wale viumbe wanne wenye uhai akisema kwa sauti kama ya radi: “Njoo!”
2 And I saw, and lo, a white horse, and he who sat on him had a bow; and there was given him a crown; and he went forth conquering, and to conquer.
Nikatazama, na hapo mbele yangu alikuwepo farasi mweupe! Yeye aliyempanda alikuwa na upinde, naye akapewa taji, akampanda akatoka akiwa kama mshindi aelekeaye katika kushinda.
3 And when he opened the second seal, I heard the second Living Creature say, "Come!"
Alipoivunja ile lakiri ya pili, nikamsikia yule kiumbe wa pili mwenye uhai akisema, “Njoo!”
4 And another horse come forth, a red horse. To him who sat on it, it was allowed to take peace from the earth, and to cause men to kill one another; and a great sword was given to him.
Ndipo akatokea farasi mwingine mwekundu sana. Yeye aliyempanda akapewa uwezo wa kuondoa amani duniani na kuwafanya watu wauane. Yeye akapewa upanga mkubwa.
5 And when he opened the third seal, I heard the third Living Creature say, "Come!" And I saw, and lo, a black horse! He who sat on him had a balance in his hand.
Mwana-kondoo alipoivunja ile lakiri ya tatu, nikamsikia yule kiumbe wa tatu mwenye uhai akisema, “Njoo!” Nikatazama, na mbele yangu alikuwepo farasi mweusi! Yeye aliyempanda alikuwa na mizani mkononi mwake.
6 And I heard the semblance of a voice in the midst of the four Living Creatures, saying. "A quart of wheat for a shilling, and three quarts of barley for a shilling; but do not harm the oil and the wine."
Ndipo nikasikia kile kilichokuwa kama sauti katikati ya wale viumbe wanne wenye uhai ikisema, “Kipimo kimoja cha ngano kwa mshahara wa kibarua wa siku moja, na vipimo vitatu vya shayiri kwa mshahara wa kibarua cha siku moja. Lakini usiharibu mafuta wala divai!”
7 And when he opened the fourth seal, I heard the voice of the fourth Living Creature calling, "Come!"
Alipovunja ile lakiri ya nne, nikasikia sauti ya yule kiumbe wa nne mwenye uhai ikisema, “Njoo!”
8 So I liked, and lo, a pale horse; and he who sat on him was named Death; and Hades was following after him. To them was given authority over the fourth part of the earth, to kill with the sword, and with famine, and with death, and with the wild beasts of the earth. (Hadēs g86)
Nikatazama, na hapo mbele yangu alikuwepo farasi mwenye rangi ya kijivujivu! Yeye aliyempanda aliitwa Mauti, naye Kuzimu alikuwa akimfuata nyuma yake kwa karibu. Wakapewa mamlaka juu ya robo ya dunia, kuua kwa upanga, njaa, tauni na kwa wanyama wakali wa dunia. (Hadēs g86)
9 And when he opened the fifth seal, I saw underneath the altar the souls of those who had been slain for the word of God, and for the testimony which they bore.
Mwana-kondoo alipoivunja ile lakiri ya tano, nikaona chini ya madhabahu, roho za wale waliochinjwa kwa ajili ya neno la Mungu na kwa ajili ya ushuhuda walioutunza.
10 And with a loud voice they cried, saying, "O Master, holy and true, How long dost thou not judge And avenge our blood On those who dwell on the earth?"
Wakalia kwa sauti kuu, wakisema, “Hata lini, Ee Bwana Mwenyezi, uliye mtakatifu na mwaminifu, hutawahukumu na kulipiza kisasi juu ya watu waishio duniani kwa ajili ya damu yetu?”
11 And there was given to each one of them a white robe; and they were told that they should rest for yet a little time, until the number should be completed by their fellow slaves and their brethren who were about to be put to death as they had been.
Kisha kila mmoja wao akapewa joho jeupe na wakaambiwa wangoje kwa muda kidogo zaidi, mpaka idadi ya ndugu zao na watumishi wenzao watakaouawa kama wao walivyouawa, itakapotimia.
12 And I looked when he opened the sixth seal, and there was a great earthquake; and the sun became black, like sackcloth, and the full moon became like blood;
Nikatazama akiivunja ile lakiri ya sita. Pakatokea tetemeko kuu la nchi, na jua likawa jeusi kama nguo ya gunia iliyotengenezwa kwa singa za mbuzi, na mwezi wote ukawa mwekundu kama damu.
13 and the stars of the sky fell to earth, as a fig tree shaken by a gale drops its unripe figs.
Nyota zilizo angani zikaanguka ardhini kama vile matunda ya mtini yasiyokomaa yaangukavyo wakati mti wake unapotikiswa na upepo mkali.
14 And the sky parted asunder like a rolled-up scroll; and every mountain and island was moved out of its place;
Anga ikatoweka kama vile karatasi isokotwavyo, na kila mlima na kila kisiwa kikaondolewa mahali pake.
15 and the kings of the earth, and the princes, and the generals, the rich and the mighty, both slaves and freemen, every one of them hid themselves in the caves and among the rocks of the mountains.
Ndipo wafalme wa dunia, wakuu wote, majemadari, matajiri, wenye nguvu na kila mtu, mtumwa na mtu huru, wakajificha katika mapango na kwenye miamba ya milima.
16 And they began to say to the mountains and to the rocks. "Fall upon us and hide us From the face of him who is seated upon the throne, And from the wrath of the Lamb;
Wakaiita milima na miamba wakisema, “Tuangukieni, mkatufiche na uso wake yeye aketiye kwenye kiti cha enzi, na mkatuepushe na ghadhabu ya Mwana-Kondoo!
17 For the Great Day of their wrath has come, And who is able to stand?"
Kwa maana siku ile kuu ya ghadhabu yao imewadia. Je, ni nani awezaye kustahimili?”

< Revelation 6 >