< Revelation 4 >

1 After this, in my vision, I saw a door opened in heaven! And the first voice that I heard speaking with me was like a trumpet, saying, "Come up hither, and I will show you the things that must come to pass hereafter."
Baada ya hayo nilitazama nikaona mlango umefunguliwa mbinguni. Na ile sauti niliyoisikia pale awali ambayo ilikuwa kama sauti ya tarumbeta, ikasema, “Njoo hapa juu nami nitakuonyesha mambo yatakayotukia baadaye.”
2 Immediately I was in the Spirit; and behold, there stood a throne in heaven, and upon the throne One sat;
Mara nikachukuliwa na Roho. Kumbe, huko mbinguni kuna kiti cha enzi na juu yake ameketi mmoja.
3 and he who sat was in appearance like a jasper stone and a sardius; and there was a rainbow round about the throne, like an emerald to look upon.
Huyo aliyeketi juu yake alikuwa kama almasi na jiwe zuri jekundu. Upinde wa mvua ulikuwa unang'aa kama zumaridi na ulikizunguka kiti cha enzi pande zote.
4 And round about the throne were four and twenty Elders seated, who were clothed in white raiment, with golden crowns upon their heads.
Kulikuwa na duara la viti ishirini na vinne kukizunguka kiti cha enzi, na juu ya viti hivyo wazee ishirini na wanne walikuwa wameketi wamevaa mavazi meupe na taji za dhahabu vichwani.
5 From the throne issued lightning and voices and thunders. Seven blazing lamps were burning before the throne; these are the seven Spirits of God.
Umeme, sauti na ngurumo, vilikuwa vinatoka kwenye hicho kiti cha enzi. Taa saba za moto zilikuwa zinawaka mbele ya hicho kiti cha enzi. Taa hizo ni roho saba za Mungu.
6 And in front of the throne as it seemed, a glassy sea like crystal; and in the midst of the throne and encircling it are four Living Creatures, full of eyes before and behind.
Mbele ya kiti cha enzi kulikuwa na kitu kama bahari ya kioo, angavu kama jiwe linga'aalo sana. Katika pande zote za hicho kiti cha enzi na kukizunguka, kilikuwa na viumbe hai vinne. Viumbe hivyo vilikuwa vimejaa macho mbele na nyuma.
7 The first creature was like a lion, and the second like a calf, and the third creature had a face like a man’s, and the fourth creature was like an eagle flying.
Kiumbe cha kwanza kulikuwa kama simba, cha pili kama ng'ombe, cha tatu kilikuwa na sura kama mtu, na cha nne kilikuwa kama tai anayeruka.
8 And the four Living Creatures, each one with six wings, are full of eyes round about and within; day and night they are chanting ceaselessly. "Holy, holy, holy is the Lord God, the Almighty. Who was, and who is, and who is to come."
Viumbe hivyo vinne vilikuwa na mabawa sita kila kimoja, na vilikuwa vimejaa macho, ndani na nje. Usiku na mchana, bila kupumzika huimba: “Mtakatifu, mtakatifu, mtakatifu ni Bwana, Mungu Mwenye Uwezo, aliyekuwako, aliyeko na anayekuja!”
9 And whenever the Living Creatures give glory and honor and thanks to Him who sits on the throne, to Him who lives forever and ever, (aiōn g165)
Kila mara viumbe vinne vilipoimba nyimbo za kumtukuza, kumheshimu na kumshukuru huyo aliyeketi juu ya kiti cha enzi, ambaye anaishi milele na milele, (aiōn g165)
10 the four and twenty Elders fall down before Him who sits on the throne, and worship Him who lives forever and ever, and cast their crowns before the throne, saying. (aiōn g165)
wale wazee ishirini na wanne hujiangusha mbele ya huyo aliyeketi juu ya kiti cha enzi na kumwabudu huyo ambaye anaishi milele na milele; na huziweka taji zao mbele ya kiti cha enzi wakisema: (aiōn g165)
11 "Worthy art thou, our Lord and our God, To receive the glory and the honor and the power; For thou didst create all things, And because of thy will they came into being And were created."
“Wewe ni Bwana na Mungu wetu, unastahili utukufu na heshima na nguvu; maana wewe uliumba vitu vyote, na kwa matakwa yako kila kitu kimepewa uhai na uzima.”

< Revelation 4 >