< Mark 1 >

1 Beginning of the gospel of Jesus Christ, the Son of God;
Mwanzo wa Injili ya Yesu Kristo, Mwana wa Mungu.
2 even as it is written in the prophet Isaiah, Behold, I am sending my messenger before your face to prepare your way.
Kama ilivyoandikwa katika kitabu cha nabii Isaya: “Tazama, nitamtuma mjumbe wangu mbele yako, atakayetengeneza njia mbele yako”:
3 The voice of one crying aloud. In the desert make ready a road for the Lord. Make his paths straight.
“sauti ya mtu aliaye nyikani. ‘Itengenezeni njia ya Bwana, yanyoosheni mapito yake.’”
4 In the desert came Johnwho baptized, and preached a baptism of repentance for the remission of sins;
Yohana alikuja, akibatiza huko nyikani, akihubiri ubatizo wa toba kwa ajili ya msamaha wa dhambi.
5 and all the land of Judea, and all the people of Jerusalem, kept going out to him, and were baptized by him in the Jordan river, confessing their sins.
Watu kutoka Uyahudi wote na sehemu zote za Yerusalemu walikuwa wakimwendea. Nao wakaziungama dhambi zao, akawabatiza katika Mto Yordani.
6 And Johnwas clothed with camel’s hair, and he had a leather girdle round his loins, and he ate locusts, and "honey of the wood."
Yohana alivaa mavazi yaliyotengenezwa kwa singa za ngamia na mkanda wa ngozi kiunoni mwake. Chakula chake kilikuwa nzige na asali ya mwitu.
7 He made proclamation. "There is One mightier than I coming after me, and I am not worthy to stoop down and unfasten his sandal strap;
Naye alihubiri akisema, “Baada yangu atakuja yeye aliye na uwezo kuniliko mimi, ambaye sistahili hata kuinama na kulegeza kamba za viatu vyake.
8 I have baptized you in water, but he shall baptize you in the Holy Spirit."
Mimi nawabatiza kwa maji, lakini yeye atawabatiza kwa Roho Mtakatifu.”
9 It was at that time that Jesus came from Nazareth of Galilee, and was baptized by Johnin the Jordan;
Wakati huo Yesu akaja kutoka Nazareti ya Galilaya, naye akabatizwa na Yohana katika Mto Yordani.
10 and as soon as he rose from the water he saw the sky cleft asunder, and the Spirit like a dove descending upon him,
Yesu alipokuwa akitoka ndani ya maji, aliona mbingu zikifunguka na Roho akishuka juu yake kama hua.
11 and a voice from the sky. "Thou art my Son, my beloved; in thee is my delight."
Nayo sauti kutoka mbinguni ikasema, “Wewe ni Mwanangu mpendwa; nami nimependezwa nawe sana.”
12 Then the Spirit drove him at once into the desert,
Wakati huo huo, Roho akamwongoza Yesu kwenda nyikani,
13 and he remained in the desert for forty days, tempted by Satan; and he was among the wild beasts, but the angels were ministering to him.
naye akawa huko nyikani kwa muda wa siku arobaini, akijaribiwa na Shetani. Alikaa na wanyama wa mwituni, nao malaika wakamhudumia.
14 After Johnhad been thrown into prison Jesus came into Galilee preaching the gospel of God.
Baada ya Yohana kukamatwa na kutiwa gerezani, Yesu aliingia Galilaya akaanza kuhubiri habari njema ya Mungu,
15 "The time is now come," he said, "and the kingdom of God is near! Repent and believe the gospel."
akisema, “Wakati umewadia, Ufalme wa Mungu umekaribia. Tubuni na kuiamini Habari Njema.”
16 And as he was passing along by the sea of Galilee he saw Simon and Andrew, Simon’s brother, casting their net into the sea, for they were fishermen;
Yesu alipokuwa akitembea kando ya Bahari ya Galilaya, aliwaona Simoni na Andrea nduguye wakizitupa nyavu zao baharini, kwa kuwa wao walikuwa wavuvi.
17 so Jesus said to them, "Come after me, and I will make you to become fishers of men."
Yesu akawaambia, “Njooni, nifuateni nami nitawafanya mwe wavuvi wa watu.”
18 At once they left their nets and followed him.
Mara wakaacha nyavu zao, wakamfuata.
19 As he went a little farther on he saw James, the son of Zebedee, and Johnhis brother, who also were in their boat mending the nets.
Alipokwenda mbele kidogo, akamwona Yakobo mwana wa Zebedayo na Yohana nduguye, wakiwa kwenye mashua yao wakizitengeneza nyavu zao.
20 Straightway he called them, and they left their father Zebedee in the ship with the hired servants and went after him.
Papo hapo akawaita, nao wakamwacha Zebedayo baba yao kwenye mashua pamoja na watumishi wa kuajiriwa, nao wakamfuata Yesu.
21 So they came to Capernaum, and as soon as the Sabbath Day came he went into the synagogue and began to teach.
Wakaenda mpaka Kapernaumu. Ilipofika siku ya Sabato, mara Yesu akaingia sinagogi, akaanza kufundisha.
22 They were astonished at his teaching, for he was teaching them with authority, not like the Scribes.
Watu wakashangaa sana kwa mafundisho yake, kwa maana aliwafundisha kama yeye aliye na mamlaka, wala si kama walimu wa sheria.
23 And at that very moment, there in their synagogue, a man in the grip of an unclean spirit shrieked out.
Wakati huo huo katika sinagogi lao palikuwa na mtu aliyekuwa amepagawa na pepo mchafu,
24 "What business have you with us, you Jesus of Nazareth? Are you come to destroy us? I know you who you are, the Holy One of God."
naye akapiga kelele akisema, “Tuna nini nawe, Yesu wa Nazareti? Je, umekuja kutuangamiza? Ninakujua wewe ni nani. Wewe ndiwe Aliye Mtakatifu wa Mungu!”
25 But Jesus rebuked him, saying. "Be quit! Come out of him."
Lakini Yesu akamkemea, akamwambia, “Nyamaza kimya! Nawe umtoke!”
26 So the unclean spirit, after tearing him, came out of him with a loud cry;
Yule pepo mchafu akamtikisatikisa huyo mtu kwa nguvu, kisha akamtoka akipiga kelele kwa sauti kubwa.
27 and every one was amazed so that they began questioning among themselves. "What does this mean? A new teaching with authority? He lays commands even upon unclean spirits and they obey him."
Watu wote wakashangaa, hata wakaulizana wao kwa wao, “Haya ni mambo gani? Ni mafundisho mapya, tena yenye mamlaka! Anaamuru hata pepo wachafu, nao wanamtii!”
28 And at once his fame spread everywhere through that part of Galilee.
Sifa zake zikaanza kuenea haraka katika eneo lote la karibu na Galilaya.
29 On leaving the synagogue they went at once with Jamesand Johnto the house of Simon and Andrew.
Mara walipotoka katika sinagogi, walikwenda pamoja na Yakobo na Yohana hadi nyumbani kwa Simoni na Andrea.
30 Now Simon’s mother-in-law lay sick of fever, and without delay they told him about her.
Mama mkwe wa Simoni alikuwa kitandani, ana homa, nao wakamweleza Yesu habari zake.
31 So he came and took her hand and raised her up. The fever left her at once, and she began to wait upon them.
Hivyo Yesu akamwendea, akamshika mkono na kumwinua. Kisha homa ikamwacha, naye akaanza kuwahudumia.
32 At evening when the sun had set, people came and brought to him all the sick and demon-possessed,
Jioni ile baada ya jua kutua, watu wakamletea Yesu wagonjwa wote na waliopagawa na pepo wachafu.
33 and the whole town was gathered at the door.
Mji wote ukakusanyika mbele ya nyumba hiyo.
34 He cured many who were ill with various diseases, and drove out many demons. But he did not allow the demons to speak, because they knew who he was.
Yesu akawaponya watu wengi waliokuwa na magonjwa ya aina mbalimbali. Akawatoa pepo wachafu wengi, lakini hakuwaacha hao pepo wachafu waseme, kwa sababu walimjua yeye ni nani.
35 In the morning he rose a great while before day and went out to a desert place, and there prayed.
Alfajiri na mapema sana kulipokuwa bado kuna giza, Yesu akaamka, akaondoka, akaenda mahali pa faragha ili kuomba.
36 And Simon and his companions hunted him up,
Simoni na wenzake wakaenda kumtafuta,
37 and told him, "Every one is looking for you."
nao walipomwona, wakamwambia, “Kila mtu anakutafuta!”
38 "Let us go away," he answered, "to the neighboring country towns, that I may preach there, too; because for that purpose I came forth."
Yesu akawajibu, “Twendeni mahali pengine kwenye vijiji jirani, ili niweze kuhubiri huko pia, kwa sababu hicho ndicho nilichokuja kukifanya.”
39 So he went throughout Galilee, preaching in the synagogues and driving out demons.
Kwa hiyo akazunguka Galilaya kote, akihubiri katika masinagogi yao na kutoa pepo wachafu.
40 One day a leper cane to him and besought him as he knelt down to him, saying, "If you choose, you are able to cleanse me."
Mtu mmoja mwenye ukoma alimjia Yesu, akamwomba akipiga magoti, akamwambia, “Ukitaka, waweza kunitakasa.”
41 Jesus, moved with compassion, put out his hand and touched him, saying, "I do choose, be clean!"
Yesu, akiwa amejawa na huruma, akanyoosha mkono wake akamgusa, akamwambia, “Nataka. Takasika!”
42 The leprosy at once left him, and he was made clean.
Mara ukoma ukamtoka, naye akatakasika.
43 Jesus immediately sent him away, charging him sternly and saying.
Baada ya Yesu kumwonya vikali, akamruhusu aende zake
44 "See you say nothing to any one; but go your way, show yourself to the priest, and offer for your purification what Moses commanded for a testimony to them."
akimwambia, “Hakikisha humwambii mtu yeyote habari hizi, bali nenda ukajionyeshe kwa kuhani, na ukatoe sadaka alizoagiza Mose kwa utakaso wako, ili kuwa ushuhuda kwao.”
45 But he went out and began to tell every one and to publish it broadcast, so that Jesus could no longer enter any town openly; but he had to remain outside in lonely places, and people kept coming to him from every quarter.
Lakini yule mtu akaenda akaanza kutangaza habari za kuponywa kwake waziwazi. Kwa hiyo, Yesu hakuweza tena kuingia katika miji waziwazi lakini alikaa sehemu zisizo na watu. Hata hivyo watu wakamfuata huko kutoka kila upande.

< Mark 1 >