< Luke 4 >
1 Then Jesus, full of the Holy Spirit, came back from the Jordan, and was led by the Spirit into the desert for forty days, all the time tempted by the devil.
Yesu, akiwa amejaa Roho Mtakatifu, akarudi kutoka Yordani. Akaongozwa na Roho Mtakatifu hadi nyikani,
2 He ate nothing during these days, and at the close of them he was hungry.
mahali ambako kwa siku arobaini alikuwa akijaribiwa na ibilisi. Kwa siku zote hizo hakula chochote, hivyo baada ya muda huo akaona njaa.
3 The devil said to him, "If you are the Son of God tell this stone to become bread."
Ibilisi akamwambia, “Ikiwa wewe ni Mwana wa Mungu, amuru jiwe hili liwe mkate.”
4 And Jesus answered him, saying, "It is written that not by bread alone shall man live."
Yesu akajibu akamwambia, “Imeandikwa: ‘Mtu haishi kwa mkate tu.’”
5 And the devil led him up and showed him all the kingdoms of the inhabited earth in an instant of time, and the devil said to him.
Ibilisi akampeleka hadi juu ya mlima mrefu akamwonyesha milki zote za dunia kwa mara moja.
6 "To you will I give all this authority and this glory; for it has been handed over to me, and I give it to whomever I wish.
Akamwambia, “Nitakupa mamlaka juu ya milki hizi na fahari zake zote, kwa maana zimekabidhiwa mkononi mwangu nami ninaweza kumpa yeyote ninayetaka.
7 "If then you will worship me, it shall all be yours."
Hivyo ikiwa utanisujudia na kuniabudu, vyote vitakuwa vyako.”
8 "It is written," answered Jesus, "Thou shalt worship the Lord, thy God, and him only shalt thou serve."
Yesu akamjibu, “Imeandikwa: ‘Mwabudu Bwana Mungu wako na umtumikie yeye peke yake.’”
9 Then he brought him to Jerusalem, and caused him to stand upon the Temple roof, and said to him. "If you really are the Son of God throw yourself down here;
Kisha ibilisi akampeleka mpaka Yerusalemu, akamweka juu ya mnara mrefu wa Hekalu, akamwambia, “Kama wewe ndiwe Mwana wa Mungu, jitupe chini kutoka hapa,
10 for it is written, "He shall give his angels charge of thee, to guard thee safely;
kwa maana imeandikwa: “‘Atakuagizia malaika zake ili wakulinde;
11 "They will bear thee up in their hands, Lest thou dash thy food against a stone."
nao watakuchukua mikononi mwao, usije ukajikwaa mguu wako katika jiwe.’”
12 "It has been said," replied Jesus, "Thou shalt not tempt the Lord, thy God."
Yesu akamjibu, “Imesemwa, ‘Usimjaribu Bwana Mungu wako.’”
13 So, after exhausting on him every kind of temptation, the devil left him for a time.
Ibilisi alipomaliza kila jaribu, akamwacha Yesu mpaka wakati mwingine ufaao.
14 Then Jesus returned in the power of the Spirit to Galilee, and his fame spread throughout all the surrounding country,
Kisha Yesu akarudi mpaka Galilaya, akiwa amejaa nguvu za Roho Mtakatifu, nazo habari zake zikaenea katika sehemu zote za nchi za kandokando.
15 and he began to teach in their synagogues, and was glorified by all.
Akaanza kufundisha kwenye masinagogi yao, na kila mmoja akamsifu.
16 Then he came to Nazareth where he had been brought up. and, as was his custom, he entered into the synagogue on the Sabbath Day, and stood up to read.
Yesu akaenda Nazareti, alipolelewa, na siku ya Sabato alikwenda katika sinagogi kama ilivyokuwa desturi yake. Akasimama ili asome,
17 And there was handed him the roll of the prophet Isaiah; and unrolling it he found the place where it was written,
naye akapewa kitabu cha nabii Isaya, akakifungua na kukuta mahali palipoandikwa:
18 The Spirit of the Lord is upon me Because He has anointed me to preach the gospel to the poor, He has sent me to proclaim release to the prisoners, And recovery of sight to the blind; To set at liberty those that are bruised,
“Roho wa Bwana yu juu yangu, kwa sababu amenitia mafuta kuwahubiria maskini habari njema. Amenituma kuwatangazia wafungwa kufunguliwa kwao, na vipofu kupata kuona tena, kuwaweka huru wanaoonewa,
19 To proclaim the acceptable year of the Lord.
na kutangaza mwaka wa Bwana uliokubalika.”
20 Then rolling up the papyrus, he gave it back to the attendant and sat down.
Kisha akakifunga kitabu, akamrudishia mtumishi na akaketi. Watu wote waliokuwamo katika sinagogi wakamkazia macho.
21 The eyes of all in the synagogue were fixed on him, and he began to say to them, "Today is this scripture fulfilled in your hearing."
Ndipo akaanza kwa kuwaambia, “Leo Andiko hili limetimia mkiwa mnasikia.”
22 And they all spoke well of him, and marveled at the words of charm that fell from his lips. "Is not this the son of Joseph?" they asked.
Wote waliokuwako wakamsifu na kuyastaajabia maneno yake yaliyojaa neema, wakaulizana, “Je, huyu si mwana wa Yosefu?”
23 Jesus answered. "Doubtless you will quote the proverb to me, "Physician, heal thyself! Do also here in your own country all that we hear that you have done in Capernaum."
Yesu akawaambia, “Bila shaka mtatumia mithali hii: ‘Tabibu, jiponye mwenyewe! Mambo yale tuliyosikia kwamba uliyafanya huko Kapernaumu, yafanye na hapa kwenye mji wako.’”
24 "I tell you in solemn truth," he added, "that no prophet is acceptable in his own country.
Yesu akasema, “Amin, nawaambia, hakuna nabii anayekubalika katika mji wake mwenyewe.
25 In very truth I tell you there were many widows in Israel in the days of Elijah, when the heavens were closed for three years and six months, when a great famine came over all the land;
Lakini ukweli ni kwamba palikuwa na wajane wengi katika Israeli wakati wa Eliya, mbingu zilipofungwa kwa miaka mitatu na miezi sita pakawa na njaa kuu katika nchi nzima.
26 "yet Elijah was not sent to any one of them, but only to a widow in Zarephath in Sidon.
Hata hivyo Eliya hakutumwa hata kwa mmoja wao, bali kwa mjane mmoja wa Sarepta katika nchi ya Sidoni.
27 "And there were many lepers in Israel in the days of the prophet Elisha, yet none of them was cleansed but only Naaman the Syrian."
Pia palikuwa na wengi wenye ukoma katika Israeli katika siku za nabii Elisha, lakini hakuna hata mmoja wao aliyetakaswa, isipokuwa Naamani mtu wa Shamu.”
28 When they had heard these words, those in the synagogue were filled with fury;
Watu wote katika sinagogi waliposikia maneno haya, wakakasirika sana.
29 they rose, hurried him outside the town, and brought him to the brow of the hill on which their city was built, intending to cast him down headlong.
Wakasimama, wakamtoa nje ya mji, wakamchukua hadi kwenye kilele cha mlima mahali ambapo mji huo ulikuwa umejengwa, ili wamtupe chini kutoka kwenye mteremko mkali.
30 But he, passing through the midst of them, took his departure.
Lakini yeye akapita papo hapo katikati ya huo umati wa watu akaenda zake.
31 Then he went down to Capernaum, a city of Galilee, and continued to teach the people on the Sabbath Days.
Kisha Yesu akashuka kwenda Kapernaumu, mji wa Galilaya, na katika siku ya Sabato akawa anafundisha.
32 They were deeply impressed by his teaching because his speech was with authority.
Wakashangazwa sana na mafundisho yake, maana maneno yake yalikuwa na mamlaka.
33 And there was in the synagogue a man possessed by the spirit of a foul demon. He cried out, in a loud voice, saying.
Ndani ya sinagogi palikuwa na mtu aliyekuwa amepagawa na pepo mchafu. Naye akapiga kelele kwa nguvu akisema,
34 "Ha! Jesus of Nazareth, what business have you with us? Are you come to destroy us? I know you who you are, you holy one of God!"
“Tuache! Tuna nini nawe, Yesu wa Nazareti? Je, umekuja kutuangamiza? Ninakujua wewe ni nani. Wewe ndiwe Aliye Mtakatifu wa Mungu!”
35 And Jesus rebuked him, saying. "Be quiet! Come out of him." And when the demon had thrown the man down before them, he came out of him without doing him any harm.
Basi Yesu akamkemea yule pepo mchafu, akisema, “Nyamaza kimya! Nawe umtoke!” Yule pepo mchafu akamwangusha yule mtu chini mbele yao wote, akatoka pasipo kumdhuru.
36 All were amazed, and began to ask one another, saying. "What is this word? For with authority and power he commands the unclean spirits and they come out."
Watu wote wakashangaa, wakaambiana, “Mafundisho haya ni ya namna gani? Anawaamuru pepo wachafu kwa mamlaka na nguvu, nao wanatoka!”
37 And the talk about him spread into every locality in the surrounding country.
Habari zake zikaanza kuenea kila mahali katika sehemu ile.
38 Now when he rose and left the synagogue, he entered into the house of Simon, where Simon’s mother-in-law lay sick of a great fever. And they kept entreating him for her.
Yesu akatoka katika sinagogi, akaenda nyumbani kwa Simoni. Basi huko alimkuta mama mkwe wa Simoni akiwa ameshikwa na homa kali, nao wakamwomba Yesu amsaidie.
39 And he stood over her and rebuked the fever, and it left her; and at once she arose and ministered unto them.
Hivyo Yesu akamwinamia na kukemea ile homa, nayo ikamwacha. Akaamka saa ile ile, naye akaanza kuwahudumia.
40 At sunset all they who had any sick with any sort of disease brought them to him; and he laid his hands on every one of them and healed them.
Jua lilipokuwa linatua, watu wakamletea Yesu watu wote waliokuwa na maradhi mbalimbali, naye akaweka mikono yake juu ya kila mgonjwa, naye akawaponya.
41 Demons also came out of many, screaming and saying, "You are the Son of God." But he rebuked them, and did not permit them to speak, because they knew that he was the Christ.
Pepo wachafu pia wakawatoka watu wengi, nao walipokuwa wakitoka wakapiga kelele, wakisema: “Wewe ni Mwana wa Mungu!” Lakini Yesu akawakemea na kuwazuia wasiseme, kwa maana walimjua kuwa yeye ndiye Kristo.
42 And when it was daybreak he left the town, and went away to a solitary place; and the crowd kept seeking him. Coming at length upon him, they attempted to detain him so that he should not leave them.
Kesho yake, kulipopambazuka, Yesu alikwenda mahali pa faragha. Watu wengi wakawa wanamtafuta kila mahali, nao walipomwona wakajaribu kumzuia asiondoke.
43 But he said to them. "I must preach the gospel of the kingdom of God to the other towns also; for that is what I was sent to do."
Lakini yeye akawaambia, “Imenipasa kuhubiri habari njema za Ufalme wa Mungu katika miji mingine pia, kwa maana kwa kusudi hili nilitumwa.”
44 So he continued to preach in the synagogues of Galilee.
Naye aliendelea kuhubiri katika masinagogi ya Uyahudi.