< Luke 1 >
1 Seeing that many have taken it in hand to draw up an account of those matters which have been fully established among us,
Kwa kuwa watu wengi wamekaa ili kuandika habari za mambo yaliyotukia katikati yetu,
2 just as they reported them to us, who were from beginning eye- witnesses and ministers of the word,
kama vile yalivyokabidhiwa kwetu na wale waliokuwa mashahidi walioyaona na watumishi wa Bwana,
3 it seemed good to me also accurately, from the very beginning, to write them to you in order, most excellent Theophilus,
mimi nami baada ya kuchunguza kila kitu kwa uangalifu kuanzia mwanzo, niliamua kukuandikia habari za mambo hayo, ewe mtukufu Theofilo,
4 so that you may know the certainty of the story which you have been taught by the word of mouth.
ili upate kujua ukweli kuhusu yale uliyofundishwa.
5 In the reign of Herod, King of Judea, there was a certain priest, named Zachariah, belonging to the class of Abijah. He had a wife named Elizabeth,
Wakati wa Herode mfalme wa Uyahudi, palikuwa na kuhani mmoja jina lake Zekaria, ambaye alikuwa wa ukoo wa kikuhani wa Abiya. Elizabeti mkewe alikuwa pia mzao wa Aroni.
6 who was a descendant of Aaron. They were both righteous in the sight of the Lord, walking in all the commandments and ordinances of the law, blameless.
Zekaria na Elizabeti mkewe wote walikuwa watu wanyofu mbele za Mungu, wakizishika amri zote za Bwana na maagizo yote bila lawama.
7 Now they had no child, for Elizabeth was barren, and both were far advanced in years.
Lakini walikuwa hawana watoto, kwa sababu Elizabeti alikuwa tasa; nao wote wawili walikuwa wazee sana.
8 Now while Zachariah was acting as priest before God in the due course of his class, it fell to his lot, according to the custom of priesthood,
Siku moja ilipokuwa zamu ya kikundi cha Zekaria, yeye akifanya kazi ya ukuhani Hekaluni mbele za Mungu,
9 to enter into the sanctuary of the Lord and to burn incense.
alichaguliwa kwa kura kwa kufuata desturi za ukuhani, kuingia Hekaluni mwa Bwana ili kufukiza uvumba.
10 And the whole multitude of the people were without, praying at the hour of incense.
Nao wakati wa kufukiza uvumba ulipowadia, wale wote waliokuwa wamekusanyika ili kuabudu walikuwa nje wakiomba.
11 Then there appeared to him an angel of the Lord, standing on the right side of the altar of incense.
Ndipo malaika wa Bwana, akiwa amesimama upande wa kuume wa madhabahu ya kufukizia uvumba, akamtokea Zekaria.
12 And as he saw him Zachariah was troubled, and fear fell upon him.
Zekaria alipomwona huyo malaika, akafadhaika sana, akajawa na hofu.
13 But the Angel said to him. "Do not be afraid, Zachariah, because your petition has been heard, and your wife Elizabeth will bear you a son, and you are to call him John.
Lakini malaika akamwambia, “Usiogope, Zekaria, kwa maana Mungu amesikia maombi yako. Mkeo Elizabeti atakuzalia mtoto wa kiume, nawe utamwita jina lake Yohana.
14 "And he shall be to you a joy and an exultation, and many shall rejoice over his birth.
Yeye atakuwa furaha na shangwe kwako, nao watu wengi watashangilia kwa sababu ya kuzaliwa kwake.
15 "For he shall be great in the sight of the Lord, "He shall drink neither wine nor strong drink, "He shall be filled with the Holy Spirit from the hour of his birth,
Kwa kuwa atakuwa mkuu mbele za Bwana, kamwe hataonja mvinyo wala kinywaji chochote cha kulevya, naye atajazwa Roho Mtakatifu hata kabla ya kuzaliwa kwake.
16 "And shall win many of the sons of Israel to the Lord, their God.
Naye atawageuza wengi wa wana wa Israeli warudi kwa Bwana Mungu wao.
17 "He shall go before Him in the wisdom and power of Elijah to turn the hearts of the fathers to their children and the disobedient to the wisdom of the righteous, and so to make ready for the Lord a people prepared for him."
Naye atatangulia mbele za Bwana katika roho na nguvu ya Eliya, ili kuigeuza mioyo ya baba kuwaelekea watoto wao, na wasiotii warejee katika hekima ya wenye haki, ili kuliweka tayari taifa lililoandaliwa kwa ajili ya Bwana.”
18 "How shall I be sure of this?" said Zachariah to the Angel. "For I am an old man and my wife is advanced in years."
Zekaria akamuuliza malaika, “Jambo hilo linawezekanaje? Mimi ni mzee na mke wangu pia ana umri mkubwa.”
19 "I am Gabriel," answered the angel, "who stand in the presence of God; and I have been sent to speak to you and to bring and to bring you this good news.
Malaika akamjibu, akamwambia, “Mimi ni Gabrieli, nisimamaye mbele za Mungu, nami nimetumwa kwako ili nikuambie habari hizi njema.
20 "And now you shall be silent and unable to speak until the day the day when this has taken place; because you did not believe my words - Words which will be fulfilled at their appointed time."
Basi sasa kwa kuwa hujaamini maneno yangu ambayo yatatimizwa kwa wakati wake, utakuwa bubu hadi siku ile mambo haya yatakapotukia.”
21 Meanwhile the people were waiting for Zachariah and wondering why he stayed so long in the sanctuary.
Wakati huo watu walikuwa wanamngojea Zekaria nje huku wakishangaa kukawia kwake mle Hekaluni.
22 And when he came out he could not speak to them, and then they knew that he had seen a vision in the sanctuary. He kept making signs to them and remained dumb.
Alipotoka akawa hawezi kusema nao, wao wakatambua kuwa ameona maono ndani ya Hekalu. Lakini kwa kuwa alikuwa bubu, akawa anawaashiria kwa mikono.
23 As soon as his term of priestly service was ended he went home;
Muda wake wa kuhudumu Hekaluni ulipomalizika, akarudi nyumbani kwake.
24 and after those days Elizabeth, his wife, Conceived, and she hid herself five months, saying.
Baada ya muda usio mrefu, Elizabeti mkewe akapata mimba, naye akajitenga kwa miezi mitano.
25 "This has the Lord done for me. He has now deigned to take the away my reproach among men."
Akasema, “Hili ndilo Bwana alilonitendea aliponiangalia kwa upendeleo na kuniondolea aibu yangu mbele ya watu.”
26 Six months later the angel Gabriel was sent by God to a town in Galilee, called Nazareth,
Mwezi wa sita baada ya Elizabeti kupata mimba, Mungu alimtuma malaika Gabrieli aende Galilaya katika mji wa Nazareti,
27 to a maiden betrothed to a man named Joseph, a descendant of David. Her name was Mary.
kwa mwanamwali bikira aliyekuwa ameposwa na mtu mmoja jina lake Yosefu wa nyumba ya Daudi. Jina la huyu mwanamwali bikira ni Maria.
28 The angel went in and said to her. "Joy to you, highly favored one! "The Lord is with you."
Naye malaika akaja kwake akamwambia: “Salamu, wewe uliyebarikiwa, Bwana yu pamoja nawe!”
29 Mary was greatly agitated at his word, and was revolving in her mind what this salutation could mean.
Maria akafadhaishwa sana na maneno haya, akajiuliza moyoni, “Salamu hii ni ya namna gani?”
30 when the angel said to her. "Fear not Mary, for you have found grace with God.
Ndipo malaika akamwambia, “Usiogope, Maria, umepata kibali kwa Mungu.
31 "And behold, you shall conceive in your womb and bear a son; and you shall call his name Jesus.
Tazama, utachukua mimba, nawe utamzaa mtoto mwanaume na utamwita jina lake Yesu.
32 "He shall be great, and shall be called the Son of the Most High. "And the Lord God will give him the throne of his forefather David,
Yeye atakuwa mkuu, naye ataitwa Mwana wa Aliye Juu Sana. Bwana Mungu atampa kiti cha enzi cha Daudi baba yake.
33 "and he shall reign over the House of Jacob forever; and of his kingdom there shall be no end." (aiōn )
Ataimiliki nyumba ya Yakobo milele, na ufalme wake hautakuwa na mwisho.” (aiōn )
34 And Mary said to the angel. "How can this be? For I have no husband?"
Maria akamuuliza huyo malaika, “Maadamu mimi ni bikira, jambo hili litawezekanaje?”
35 "The Holy Spirit shall come upon you," said the angel, "and the power of the most High shall overshadow you, and therefore the holy offspring which is born, shall be called the son of God.
Malaika akamjibu, “Roho Mtakatifu atakujilia juu yako, nazo nguvu zake Yeye Aliye Juu Sana zitakufunika kama kivuli. Kwa hiyo mtoto atakayezaliwa atakuwa mtakatifu, naye ataitwa Mwana wa Mungu.
36 "And behold your kinswoman, Elizabeth, she also has conceived a son in her old age, and this was the sixth month with her that was called barren.
Tazama, jamaa yako Elizabeti amechukua mimba katika uzee wake, na huu ni mwezi wake wa sita, yeye aliyeitwa tasa.
37 "For no word of God shall be void of power."
Kwa maana kwa Mungu hakuna lisilowezekana.”
38 Then Mary said. "Behold I am Lord’s slave. Let it be to me as you have said." Then the angel departed from her.
Maria akasema, “Tazama, mimi ni mtumishi wa Bwana. Na iwe kwangu kama ulivyosema.” Kisha malaika akaondoka, akamwacha.
39 Soon after this Mary set out and hastened unto the hill-country to a town in Judah;
Wakati huo Maria akajiandaa, akaharakisha kwenda katika mji mmoja kwenye vilima vya Uyahudi.
40 and there she came into the house of Zachariah, and greeted Elizabeth.
Akaingia nyumbani kwa Zekaria na kumsalimu Elizabeti.
41 And when Elizabeth heard her salutation, the babe leaped in her womb, and Elizabeth herself was filled with the Holy Spirit,
Naye Elizabeti aliposikia salamu ya Maria, mtoto aliyekuwa tumboni mwake akaruka. Elizabeti akajazwa na Roho Mtakatifu,
42 and called out with a loud cry. "Blessed are you among women, and blessed is your unborn child!
akapaza sauti kwa nguvu akasema, “Umebarikiwa wewe miongoni mwa wanawake, naye mtoto utakayemzaa amebarikiwa.
43 "But why is this honor done me, that the mother of my Lord should come me?
Lakini ni kwa nini mimi nimepata upendeleo kiasi hiki, hata mama wa Bwana wangu afike kwangu?
44 "For behold when the sound of your salutation reached my ears, the babe leaped with joy within my womb.
Mara tu niliposikia sauti ya salamu yako, mtoto aliyeko tumboni mwangu aliruka kwa furaha.
45 "And blessed is she who believed that the Lord’s words spoken to her would be fulfilled."
Amebarikiwa yeye aliyeamini kwamba lile Bwana alilomwambia litatimizwa.”
46 And Mary said. "My soul doth magnify the Lord,
Naye Maria akasema: “Moyo wangu wamwadhimisha Bwana,
47 "My spirit exults in the God, who is my Saviour,
nayo roho yangu inamfurahia Mungu Mwokozi wangu,
48 "For he has regarded the humiliation of his slave, And from this hour all ages will count me blessed.
kwa kuwa ameangalia kwa fadhili unyonge wa mtumishi wake. Hakika tangu sasa vizazi vyote vitaniita aliyebarikiwa,
49 "For he who is mighty has done great things for me; And holy is his name.
kwa maana yeye Mwenye Nguvu amenitendea mambo ya ajabu: jina lake ni takatifu.
50 "His mercy is unto generations and generations on those who reverence him.
Rehema zake huwaendea wale wamchao, kutoka kizazi hadi kizazi.
51 "He has showed strength with his arm. "He has scattered proud in the imagination of their hearts;
Kwa kuwa ametenda mambo ya ajabu kwa mkono wake; amewatawanya wale wenye kiburi ndani ya mioyo yao.
52 "he has put down princes from their thrones, and has exalted those of low degree.
Amewashusha watawala toka kwenye viti vyao vya enzi, lakini amewainua wanyenyekevu.
53 "The hungry he has filled with good things, But the rich he has sent empty away.
Amewashibisha wenye njaa kwa vitu vizuri, bali matajiri amewafukuza mikono mitupu.
54 "He has helped Israel, his servant, that he might remember mercy,
Amemsaidia mtumishi wake Israeli, kwa kukumbuka ahadi yake ya kumrehemu
55 "As he spoke to our forefathers, to Abraham and his offspring forever." (aiōn )
Abrahamu na uzao wake milele, kama alivyowaahidi baba zetu.” (aiōn )
56 So Mary stayed with Elizabeth about three months and returned home.
Maria akakaa na Elizabeti karibu miezi mitatu, kisha akarudi nyumbani kwake.
57 Now when the time of Elizabeth’s delivery was come, she gave birth to a son;
Ulipowadia wakati wa Elizabeti kujifungua, alizaa mtoto mwanaume.
58 and her neighbors and kinsfolk heard that the Lord had magnified his mercy toward her; and they rejoiced with her,
Majirani zake na jamii zake wakasikia jinsi Bwana alivyomfanyia rehema kuu, nao wakafurahi pamoja naye.
59 and came on the eighth day to circumcise the child. They were about to call him "Zachariah," after his father,
Siku ya nane wakaja kumtahiri mtoto, wakataka yule mtoto aitwe Zekaria, ambalo ndilo jina la baba yake.
60 when his mother said, "No, he is to be called John."
Lakini mama yake akakataa na kusema, “Hapana! Jina lake ataitwa Yohana.”
61 Said they, "You have no relatives of that name!"
Wakamwambia, “Hakuna mtu yeyote katika jamaa yako mwenye jina kama hilo.”
62 Then they asked his father by signs what he wished to call the child.
Basi wakamfanyia Zekaria baba yake ishara ili kujua kwamba yeye angependa kumpa mtoto jina gani.
63 So he asked for a writing tablet and wrote down, "His name is John."
Akaomba wampe kibao cha kuandikia na kwa mshangao wa kila mtu akaandika: “Jina lake ni Yohana.”
64 Every one was surprised, and at once his mouth was opened and his tongue loosed, and he spoke, blessing God.
Papo hapo kinywa chake kikafunguliwa na ulimi wake ukaachiwa, akawa anaongea akimsifu Mungu.
65 And there came a great fear upon all in the neighborhood; and throughout the hill country of Judea all these sayings were much talked about.
Majirani wote wakajawa na hofu ya Mungu, na katika nchi yote ya vilima vya Uyahudi watu walikuwa wakinena juu ya mambo haya yote.
66 All the story laid it up in their hearts, saying "What, then, will this child be?" For the Lord’s hands was with him.
Kila aliyesikia habari hizi alishangaa akauliza, “Je, mtoto huyu atakuwa mtu wa namna gani?” Maana mkono wa Bwana ulikuwa pamoja naye.
67 And his father, Zachariah, was filled with the Holy Spirit and prophesied, saying.
Zekaria, baba yake, akajazwa na Roho Mtakatifu, naye akatoa unabii, akisema:
68 "Blessed be the Lord, the God of Israel, For he has visited and redeemed his people,
“Ahimidiwe Bwana, Mungu wa Israeli, kwa kuwa amewajilia watu wake na kuwakomboa.
69 "And has raised up a mighty Deliverer for us In the house of his servant David,
Naye ametusimamishia pembe ya wokovu katika nyumba ya Daudi mtumishi wake,
70 "As he spake by the mouth of his holy Prophets Which have been since the world began (aiōn )
kama alivyonena kwa vinywa vya manabii wake watakatifu tangu zamani, (aiōn )
71 To deliver us from our enemies, and from the power Of all who hate us.
kwamba atatuokoa kutoka kwa adui zetu, na kutoka mikononi mwao wote watuchukiao:
72 "He showed mercy to our forefathers, He remembered his holy covenant,
ili kuonyesha rehema kwa baba zetu na kukumbuka Agano lake takatifu,
73 "The oath which he swore to Abraham, our forefather,
kiapo alichomwapia baba yetu Abrahamu:
74 "That he we should be delivered out of the Hand of our enemies, And should serve him without fear,
kutuokoa kutoka mikononi mwa adui zetu, tupate kumtumikia yeye pasipo hofu
75 "In holiness and righteousness before him All our days.
katika utakatifu na haki mbele zake, siku zetu zote.
76 "And thou, child, shalt be called the Prophet of the Most High, For thou shalt go before the Lord to prepare the way
“Nawe mtoto wangu, utaitwa nabii wa Aliye Juu Sana; kwa kuwa utamtangulia Bwana na kuandaa njia kwa ajili yake,
77 "To give to his people a knowledge of salvation Through the remission of their sins,
kuwajulisha watu wake juu ya wokovu utakaopatikana kwa kusamehewa dhambi zao,
78 "Through the heart of mercy of our God, Whereby the Dayspring from on high shall visit us,
kwa ajili ya wingi wa rehema za Mungu wetu, nuru itokayo juu itatuzukia
79 "To give light to those who sit in darkness and in the shadow of death, And to guide our feet into the paths of peace."
ili kuwaangazia wale waishio gizani na katika uvuli wa mauti, kuiongoza miguu yetu katika njia ya amani.”
80 And the child grew, and became strong in the Spirit, and remained in the desert till the day of his showing to Israel.
Yule mtoto akakua na kuongezeka nguvu katika roho; akaishi nyikani hadi siku ile alipojionyesha hadharani kwa Waisraeli.