< Jude 1 >
1 Jude, a slave of Jesus Christ, and a brother of James. To those who are in God, the Father beloved, kept for Jesus Christ, and called.
Yuda, mtumwa wa Yesu Kristo na nduguye Yakobo: Kwa wale walioitwa, wapendwa katika Mungu Baba na kuhifadhiwa salama ndani ya Yesu Kristo:
2 May mercy and peace and love be multiplied to you.
Rehema, amani na upendo viwe kwenu kwa wingi.
3 Beloved, although I was making all haste to write to you in regard to our common salvation, I am compelled to write you an appeal to defend the faith once for all committed to the saints.
Wapendwa, ingawa nilikuwa ninatamani sana kuwaandikia kuhusu wokovu ambao tunaushiriki sisi sote, niliona imenipasa kuwaandikia na kuwasihi kwamba mwitetee imani iliyokabidhiwa watakatifu kwa nafasi moja itoshayo.
4 For certain men have crept in stealthily - men predestined in ancient prophecies for this condemnation - impious ones! They pervert the grace of our God into licentiousness, and deny Jesus Christ, our sole Master and Lord.
Kwa kuwa kuna watu waliojipenyeza kwa siri katikati yenu, watu walioandikiwa tangu zamani hukumu hii, waovu, wapotoshao neema ya Mungu wetu kuwa ufisadi wakimkana yeye aliye Bwana wetu wa pekee, Bwana Yesu Kristo.
5 I wish to remind you of what you already know right well, that although the Lord once saved a people out of the land of Egypt, he afterward destroyed those who did not believe;
Ingawa mmekwisha kujua haya yote, nataka niwakumbushe kuwa Bwana akiisha kuwaokoa watu wake kutoka nchi ya Misri, baadaye aliwaangamiza wale ambao hawakuamini.
6 while the angels who did not keep their first domain but left their proper abode, are held by him in blank darkness, in everlasting chains, in preparation for the judgment of the Great Day. (aïdios )
Nao malaika ambao hawakulinda nafasi zao, lakini wakayaacha makao yao, hawa amewaweka katika giza, wakiwa wamefungwa kwa minyororo ya milele kwa ajili ya hukumu Siku ile kuu. (aïdios )
7 So also Sodom and Gomorrah and the near-by cities which in like manner glutted themselves in sensuality and unnatural vice, are exhibited as a warning of the eternal fire, in the punishment they undergo. (aiōnios )
Vivyo hivyo, Sodoma na Gomora na pia ile miji iliyokuwa kandokando, ambayo kwa jinsi moja na hao, walijifurahisha kwa uasherati na kufuata tamaa za mwili zisizo za asili, waliwekwa wawe mfano kwa kuadhibiwa katika moto wa milele. (aiōnios )
8 Yet in just the same way these dreamers also defile the flesh, while they set at naught dominion and scoff at dignities.
Vivyo hivyo, hawa waotao ndoto huutia mwili unajisi, hukataa kuwa chini ya mamlaka na kunena mabaya juu ya wenye mamlaka.
9 But Michael, the Archangel, when in contending with the devil, he was disputing about the body of Moses, did not dare to pronounce sentence for blasphemy, but said, "The Lord rebuke you."
Lakini hata malaika mkuu Mikaeli alipokuwa anashindana na ibilisi juu ya mwili wa Mose, hakuthubutu kumlaumu, bali alimwambia, “Bwana na akukemee!”
10 Yet these men blaspheme about matters of which they know nothing, while they use such things as they do understand by instinct (like the animals who have no reason) for their own destruction.
Lakini watu hawa hunena mabaya dhidi ya mambo wasiyoyafahamu. Na katika mambo yale wanayoyafahamu kwa hisia kama wanyama wasio na akili, hayo ndiyo hasa yanayowaharibu.
11 Alas for them! They have walked in the path of Cain; for the sake of gain they have rushed headlong into Balaam’s error, and have perished in Korah’s rebellion.
Ole wao! Kwa kuwa wanaifuata njia ya Kaini, wamekimbilia faida katika kosa la Balaamu na kuangamia katika uasi wa Kora.
12 These are they who are stains upon your love-feasts; when they feast sumptuously without scruple, looking after none but themselves. They are clouds without water, driven along by the winds; trees of autumn, fruitless, doubly dead, torn up by the roots,
Watu hawa ni dosari katika karamu zenu za upendo, wakila pamoja nanyi bila hofu, wakijilisha pasipo hofu. Wao ni mawingu yasiyokuwa na maji, yakichukuliwa na upepo, miti isiyo na matunda wakati wa mapukutiko, ambayo hunyauka, iliyokufa mara mbili na kungʼolewa kabisa.
13 wild waves of the sea, foaming out their own shame; wandering stars, for whom is reserved the blackness of darkness forever. (aiōn )
Wao ni mawimbi makali ya bahari, yakitoa povu la aibu yao wenyewe, ni nyota zipoteazo, ambao weusi wa giza ndio akiba waliowekewa milele. (aiōn )
14 It was to these, too, that Enoch, the "seventh in descent from Adam," prophesied, saying, "Lo! the Lord is come with myriads of his saints,
Enoki, mtu wa saba kuanzia Adamu alitoa unabii kuhusu watu hawa, akisema: “Tazama, Bwana anakuja pamoja na maelfu kwa maelfu ya watakatifu wake,
15 to execute judgment upon all, and to convict all the ungodly of all the ungodly deeds which in their ungodliness they have committed; and of all the hard things which they have spoken against Him, ungodly sinners that they are!"
ili kumhukumu kila mmoja na kuwapatiliza wote wasiomcha Mungu kwa matendo yao yote ya uasi waliyoyatenda, pamoja na maneno yote ya kuchukiza ambayo wenye dhambi wamesema dhidi yake.”
16 For these are murmurers, always complaining. They always go where their passions lead, and their mouth speaks great swelling words, while they pay court to men for the sake of the advantage they can get.
Watu hawa ni wenye kunungʼunika na wenye kutafuta makosa; wao hufuata tamaa zao mbaya, hujisifu kwa maneno makuu kuhusu wao wenyewe na kuwasifu mno watu wenye vyeo kwa ajili ya kujipatia faida.
17 But as for you, dearly beloved, remember the words spoken before by the apostles of our Lord Jesus Christ,
Lakini ninyi wapenzi, kumbukeni yale mitume wa Bwana Yesu Kristo waliyonena zamani.
18 how they used to say to you, "In the last times there will be scoffers who will be led only by their godless passions."
Kwa kuwa waliwaambia, “Siku za mwisho kutakuwa na watu wenye kudhihaki, watakaofuata tamaa zao wenyewe za upotovu.”
19 These are the men, sensual and unspiritual, who cause divisions.
Hawa ndio watu wanaowagawa ninyi, wafuatao tamaa zao za asili, wala hawana Roho.
20 But you, beloved, continually building yourselves up on your most holy faith, and ever praying in the Holy Spirit,
Lakini ninyi wapendwa, jijengeni katika imani yenu iliyo takatifu sana tena ombeni katika Roho Mtakatifu.
21 must keep yourselves in the love of God, while waiting for the mercy of our Lord Jesus Christ, which ends in life eternal. (aiōnios )
Jilindeni katika upendo wa Mungu mkitazamia kwa furaha rehema ya Bwana wetu Yesu Kristo ili awalete katika uzima wa milele. (aiōnios )
22 Pity some who are wavering, and save by dragging them out of the fire;
Wahurumieni walio na mashaka;
23 others pity, but with caution, hating even the garment spotted by the flesh.
wengine waokoeni kwa kuwanyakua kutoka kwenye moto; nao wengine wahurumieni mkiwa na hofu, mkichukia hata vazi lenye mawaa na kutiwa unajisi na mwili.
24 Now unto Him who has power to guard you from stumbling, and to make you stand in the presence of his glory, faultless and exultant,
Kwake yeye awezaye kuwalinda ninyi msianguke na kuwaleta mbele za utukufu wake mkuu bila dosari na kwa furaha ipitayo kiasi:
25 to the only God, our Saviour, through Jesus Christ our Lord, be ascribed glory, majesty, might, and authority, as it was before time began, is now, and ever shall be to all the ages. Amen. (aiōn )
kwake yeye Mungu pekee Mwokozi wetu, kwa Yesu Kristo Bwana wetu, utukufu, ukuu, uweza na mamlaka ni vyake tangu milele, sasa na hata milele! Amen. (aiōn )